2002- - - 2013 oooooooh ndoa yangu

2002- - - 2013 oooooooh ndoa yangu

Msamehe tu jamani, shetani atakuwa alimpitia. Toka huko ulikojifungia kwanza. Usiongee nae ukiwa na hasira. Ila kama hujawahi kumcheat toka mna-date hadi leo usimsamehe.

Sikubaliani na wewe Komandoo....

Watu wanacheat sana ila wanachukua hatua za umakini wa hali ya juu kuhakikisha wenzi wao hawagundui.

Kwa maelezo ya mleta mada, hii ndoa ilishavunjika siku siku nyingi...

Ameshapata ushahidi na akachukue talaka yake kwa court...

Sidhani kama kuna ndoa hapo....I stand to be corrected!

Babu DC!!
 
hapo mkuu mbona kama unahalalsha makosa? Ina maana amsamehe il aendelee kusaltiwa co! Me bnafc kwenye swala la usalt cna msamaha ulmwengu wenyewe huu wa maradh kbao thn amsamehe wtt waje kubak yatma.


Nimesikitika sana kwamba wadau wengi wanashindwa au wanaogopa maamuzi magumu...ndiyo maana hata kuongoza nchi tumeshindwa....

Mke anacheza na SMS mbele ya mumewe, na mwisho anatumiwa uchafu kama huo?

Kwangu sidhani kama nina muda wa kuhangaika na mtu wa namna hiyo hata kama tuna watoto 100...

Babu DC!!
 
Pole sana kaka! Aisee nakushauri uwapende sana watoto wako hao ndo kaka zako na dada zako wa damu hawa wanawake waone hivo hivo kwanza tambua mwanamke sio ndugu yako! siwezi kukushauri uachane na mke wako sana sana ntakwambia umsamehe bure jiulize tatizo liko wapi lililopelekea hadi akafanya hivo. Mwonyeshe kuwa unajua alichokifanya. Usitumie hasira na ukickia uanaume ndo hapo. Msamehe bure ili watoto wapate malezi yenu wote.
 
Pole sana kakaangu hadi nimesikia tumbo langu linauma juu ya kukuhurumia, haya mambo yasikie kwa mwenzio bana. kama walisema waliotangulia usijukue uwamuzi haraka nakuomba tena kakaangu, kaa tulia kwanza, pole sana.
 
kaka, naomba utulie sana, na wakati huu umuombe Mungu kuliko kipindi chochote ulichowahi kuomba katika maisha yako. Si siku nyingi nilileta uzi humu, wa kuwasisistiza watu kutokukatisha maisha sababu ya penzi. Kwa lugha nyepesi, maisha yako yana thamani sana mbele za Mungu kuliko unachokiwaza sasa. Na jifunze kuona kuwa mke wako amemkosea Mungu na siyo wewe, hivyo Mungu atamsamehe, na wewe unapaswa pia kumsamehe! Please nakuomba umsamehe mke wako, na ujismehe pia! Ni ngumu, lakini pia inawezekana!
yaani watu mnamaneno ya hekimaa,,daaa ila inataka moyo wangu
 
pole sana kaka, hayo ndio maisha ya ndoa, utakutana na mengi zaidi we acha tu...mi najua hali unayopitia sasa hivi kwani na mimi yalishawahi kunikuta hayo...yaani mtu unakuwa km upo katikati ya kifo na uhai..kwa kweli machungu ya kuchitiwa na mume/mke ni makubwa kuliko kufiwa...kwa yaliyomkuta anajua maana ya ninachosema...

kabla sijakushauri ningependa kukuuliza kama ww ulishawahi kumcheat mkeo? na je yeye mkeo aligundua hilo? nauliza hivi kwa sbb sis wanawake tulio kwny ndoa mara nyingi tunacheat baada ya kusalitiwa na waume zetu.....inakuwa km revenge hivi...yaani hata kama alikusamehe na ilipita miaka mingi toka ww umcheat ni rahisi sana na yeye kuja kukucheat baadae...
lkn kama una hakika hujawahi kumcheat kabisa tangu umemuoa, basi huyo hakufai(japo waweza msamehe) lkn posibility ya yy kuendelea na huyo hawara yake ni kubwa....atakachofanya ni kubadilisha tu staili ili asikamatwe tena...
ila km uliwahi kumcheat basi msamehe na muendelee kulea watoto, kwani kile kilichokufanya ww umcheat ndicho kilichomfanya na yy akucheat..
 
pole sana mkuu,,ila ndio hivyo just kaa chini,,mwambie ukweli,then msikilize anampango gani na wewe,,ukiona hanamuelekeo wa kukiri kosa na kuomba msamaha wa kweli,,basi unaweza kupata uamuzi sahihi mkuu,,pole sana
 
Habari wakuu mm ni mzima wa afya ila naandika uzi huu nikiwa na akili nyingine sio ile impendezayo mungu na kama ntakosea basi naomba mnisamehe , nadhani nilishawahi kuleta tatizo langu humu jamvini kuhusu mambo au mwenendo wa ndoa yangu na nikapata ushauri na wengine kukejeli bila kujali ni madhara gani ntakuja kupata ila mm lengo langu lilikuwa sio kuacha au kuharibu ndoa yangu kwani naipenda familia yangu na vile vile humu jf ni sehemu nyingine yakufaham mambo amabayo huyajui kwani kuna watu wanaweza kukupa ushauri na kufanikisha kile ambacha kina kusibu , sasa basi mm nilikuwa na tatizo la cm ya wife kuwa bize sana ktk text ya ujumbe mfupi na vile huwa cm haikai mezani au kuweka kama mm ninavyo weka cm yangu ila yake mda wote nikirudi kazini iko bize sana yani labda azime nikaja kuomba ushauri hapa kuwa cm ya wife ni nikia C3 nataka kujua au mtu anipe utalam wakujua text zote alizo kuwa anatumiwa ili nimjue anaye haribu ndoa yangu kweli nilipata ushauri na wengine kunibeza ila leo asubuhi nimeona sms ikisema kuwa ' asante bby jana umenifuhisha sana kwa penzi lako ' na ukichek jana kweli alirudi home saa 2 usiku akiwa hoi na kusema amechelewa usafiri kwa hiyo ametembea kwa mguu sasa now hakuna tena amani na cm ninayo mm na niko chumbani kwangu nimejifungia na tafakari hatma ya ndoa yangu na cm nimepiga amepokea mwanaume kwahiyo naombeni ushauri wakuu pleace pleace familia yangu inaanagamia nnawatoto wawili jamani na huyu mwanamke amenichefua sana jamaani hapa sija,mwambia ndugu yeyote na lia kwa uchungu sna
Inauma sana tena sana, kusalitiwa ni kuucharangwa moyo, Mungu tusamehe kw haya makosa, nakushauri ndugu yangu, tuliza moyo, kumbuka watoto, chakufanya chukua hatua kwa wachungaji, kama hataki au hakubali basi mwambie aamue yeye kwani hatma ya watoto iko mikononi mwa Mungu atawatunza tu.
Wenzetu wakipata nje wakotayari kuharibu nyumbani, lkn ni ubinadamu tu. Muombee kwa Mungu na wewe omba sana muda wate upate amani, lkn usichukue sheria mkononi wala usikae peke yako muda mwingi jichanganye na wengune, lkn usinywe pombe, utazidi kuchanganyikiwa nenda kanisani omba Mungu atakusikia.
 
pole sana..kweli wanawake tunatofautiana asee
 
pole sana kaka, hayo ndio maisha ya ndoa, utakutana na mengi zaidi we acha tu...mi najua hali unayopitia sasa hivi kwani na mimi yalishawahi kunikuta hayo...yaani mtu unakuwa km upo katikati ya kifo na uhai..kwa kweli machungu ya kuchitiwa na mume/mke ni makubwa kuliko kufiwa...kwa yaliyomkuta anajua maana ya ninachosema...

kabla sijakushauri ningependa kukuuliza kama ww ulishawahi kumcheat mkeo? na je yeye mkeo aligundua hilo? nauliza hivi kwa sbb sis wanawake tulio kwny ndoa mara nyingi tunacheat baada ya kusalitiwa na waume zetu.....inakuwa km revenge hivi...yaani hata kama alikusamehe na ilipita miaka mingi toka ww umcheat ni rahisi sana na yeye kuja kukucheat baadae...
lkn kama una hakika hujawahi kumcheat kabisa tangu umemuoa, basi huyo hakufai(japo waweza msamehe) lkn posibility ya yy kuendelea na huyo hawara yake ni kubwa....atakachofanya ni kubadilisha tu staili ili asikamatwe tena...
ila km uliwahi kumcheat basi msamehe na muendelee kulea watoto, kwani kile kilichokufanya ww umcheat ndicho kilichomfanya na yy akucheat..

Thx mamito kwa ujumbe mzuri,wanaume wa sasa hivi inabidi tuwe muwe na mioyo migumu na ya uvumilivu kama sie wanawake,
jamani wanawake tunavumilia mengi sana kwny ndoa mtu anakucheat waziwazi wala haogopi chochote na ukimfuma ukamuuliza anaomba msamaha wa kinafiki then anaendelea tena na mambo yake ,
jamani na sie tunachoka tena tunachoka sana kupita maelezo na ndoa zetu tunazipenda sana , sasa ili kujaribu kuishi bila stress mana waweza kufa siku zako inabidi tu mtu atafute mtu wa kumpunguzia stess huko nje .
NAJUA WANAUME MTAPINGA SANA LAKINI NYIE NDIO SABABU KUBWA YA WANAWAKE WENU KUTOKA NJE YA NDOA ZAO!!!

Sorry mtoa mada kwa kutoka nje ya mada,but kama na wewe ulishawahi toka nje ya ndoa bac nitakuwa sijatoka nje ya mada!
 
gfsonwin huwa naamini na kuheshimu sana mchango wako ndani ya hili jukwaa, sijui kama umepitia uzi huu wa sony wega na kusema chochote! Ndoa yake inataka kuteketea!
 
gfsonwin huwa naamini na kuheshimu sana mchango wako ndani ya hili jukwaa, sijui kama umepitia uzi huu wa sony wega na kusema chochote! Ndoa yake inataka kuteketea!

asante sana kaka mzuri HP kwa kuniita. Binafsi sikuwa nimeuona huu uzi ila nimeskitia sana juu ya hili linalomtokea.

ukweli ni kwamba hakuna mtu msafi ambaye anaweza kunyoosha mkono wake na kunyanyua jiwe ampige huyu mwanamke. Lakini pia hatuamini katika kutenda makosa siku zote.

HP talking from experience it pains kuwa cheated na hasa inapojulikana lakin pia hili halifanyi kuwa kosa kubwa kuliko yote ambayo mwanadamu anaweza kutenda. na hata hivyo mtu hubadilika aweza akawa mwema sana akaja kuwa shetan sana na kesho akarudi kuwa mwema kulingana tu na circumstances. Binafsi naamini katika kubadilika na hsa in a positive way na pia naamini katika msamaha.

ndoa yangu ilirudi kuwa njema baada ya mimi kusamehe na kuamini kwamba hubby angebadilika, na hata hivyo mimi kwenye makosa yangu basi hubby huamini kwenye msamaha na kwamba nitabadilika. hata kama nilikosea nikawa ibilisi jana haimaanish kwamba leo ni yule yule ibilisi, kwani bado wema wa Mungu upo ili kuturudisha kwenye msatari. Namshuru Mungu sana kwamba kwa wema wake huu nimeyaona maisha kwa namna ya tofauti sana sana kiasi kwamba hata kwenye tatizo la huyu ndugu yetu bado naona kwamba wema wa Mungu upo na upo ili kuitetea ndoa yake.

ushauri wangu, wala asiamue chochote akiwa na hasira, na wala asimwone mkewe kwamba ni mkosa kuliko binadamu wote, ila ajichukulie kwamba mkewe bado ni mwema sana kwake, hata kama kazini na mtu mwingine na kwamba bado wema wa Mungu upo ili kumbadilisha. namshauri pia ni wakati mzuri wa kufanya ibada za pamoja na kufunga kwaajili ya ndoa yao, na hata kuitolea sadaka.

ili kuweza kusamehe basi ni bora wakapeana nafasi kidogo yaani wakaseparate ili kuweza kupeana nafasi ya kutafakari kwa kina kuhusu hatima ya familia yao na hapo huwa mara nyingi inaletea familia kurudi pamoja tena. namshauri ampeleke mkewe kwa wazazi wake pasi kusema lolote amwache huko kwa muda. narudia tena ampeleke kwa wazazi wa kiume ili binti ajue kabisa kwamba mumewe kampa distance ili apate kutafakari vyema nafasi ya mahusiano yao ya mbeleni. kumpeleka kwa wazi wa kike ni hatua ya mwisho kabisa.
 
Swali kwa wanaume wanaochangia humu kua amwache mkewe jee nyinyi niwasafi???hamjawai wasaliti wake zenu???au arobaini yenu haijafika???pole sana kaka.
 
dooonh jamani ndoa hizi lakini mimi kwa upande wangu nakushairi hivi chukua mds then utafakari kwa kina je ukimuacha mkeo watoto watabaki na nani? Na je nini chanzo cha tatizo kwani huwezi kumaliza tatizo bila kujua chanzo,Katika kipindi hiki jaribu hata kutoka nae out usiongee ukiwa una jazba ongea nae kwa utaratibu sana na usijaribu kuwaeleza watu wengine kwani mambo yenu yakikaa sawa utaona aibu na watu watakuwa wanajua kuwa mkeo sio mwaminifu,Muombe na mungu akupe ujasiri katika kipindi hiki kigumu kwani inauma sana kusalitiwa
 
Tobaa... Haya mambo yasikie tu kwa watu...
Ila wanasema usipoziba ufa utajenga ukuta. Kama ni mda mrefu alikuwaga 'bize' na simu, na kama uliplan kuihack hio simu, then ulitakiwa ufanye mapema ili kupunguza madhara. On the other way, machungu yote unayopata sasa yanatokana na sio yeye kukusaliti, bali wewe kujua amekusaliti. Kama usingejua maisha yangeendelea vizuri tu...

Sasa kuwa mwanaume, acha kulia lia... Mtafute mwizi wako, mfanyie kitu mbaya. Mkeo atasikia kutoka kwake, then atajipima achukue uamuzi gani. Kwa kuanza, muandikie huyo jamaa msg mwambie kuwa umeshagundua kuwa anatembea na mkeo, na kwa sasa unatafakari tu adhabu utampa kwa njia gani. Mwambie kama ana mali, si vibaya akaanza kuandika urithi...
 
Jamani tuweni wakweli hivi kweli mtu kasalitiwa anawezaje kuonyesha huo upendo !!
 
Pole sana mkuu, ila naomba nisichangie lolote katika huu uzi, hii ni kwa manufaa ya watoto wako!
 
I see,kweli lisemwalo lipo nakumbuka kuna mwana JF mmoja alishaandika uzi kwamba unapokuwa kwenye
mahusiano yoyote usiyachukulie kama ni very serious isue,kwani kwa kufanya hivo siku ukisalitiwa utaumia sana.
Sasa ndo naelewa yule bwana alimaanisha nini !!!
 
Fanya hv mrudishie simu yake alaf usmsemeshe,wapende wanao fanya mambo yko ucmsemeshe,km ana akili hatokaa ataondoka tu,na utakua ushapata sltn,kwan km mtu anaweza kufnya usaliti wazi wazi hata ukisamehe hawez acha ameshanogewa,kna magonjwa mengi sana kwa sasa angalia msije mkawaacha watoto,Mungu akutangulie kwenye maamuzi yako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom