2002- - - 2013 oooooooh ndoa yangu

2002- - - 2013 oooooooh ndoa yangu

sony wega

JF-Expert Member
Joined
Jun 18, 2012
Posts
234
Reaction score
35
Habari wakuu mm ni mzima wa afya ila naandika uzi huu nikiwa na akili nyingine sio ile impendezayo mungu na kama ntakosea basi naomba mnisamehe , nadhani nilishawahi kuleta tatizo langu humu jamvini kuhusu mambo au mwenendo wa ndoa yangu na nikapata ushauri na wengine kukejeli bila kujali ni madhara gani ntakuja kupata ila mm lengo langu lilikuwa sio kuacha au kuharibu ndoa yangu kwani naipenda familia yangu na vile vile humu jf ni sehemu nyingine yakufaham mambo amabayo huyajui kwani kuna watu wanaweza kukupa ushauri na kufanikisha kile ambacha kina kusibu , sasa basi mm nilikuwa na tatizo la cm ya wife kuwa bize sana ktk text ya ujumbe mfupi na vile huwa cm haikai mezani au kuweka kama mm ninavyo weka cm yangu ila yake mda wote nikirudi kazini iko bize sana yani labda azime nikaja kuomba ushauri hapa kuwa cm ya wife ni nikia C3 nataka kujua au mtu anipe utalam wakujua text zote alizo kuwa anatumiwa ili nimjue anaye haribu ndoa yangu kweli nilipata ushauri na wengine kunibeza ila leo asubuhi nimeona sms ikisema kuwa ' asante bby jana umenifuhisha sana kwa penzi lako ' na ukichek jana kweli alirudi home saa 2 usiku akiwa hoi na kusema amechelewa usafiri kwa hiyo ametembea kwa mguu sasa now hakuna tena amani na cm ninayo mm na niko chumbani kwangu nimejifungia na tafakari hatma ya ndoa yangu na cm nimepiga amepokea mwanaume kwahiyo naombeni ushauri wakuu pleace pleace familia yangu inaanagamia nnawatoto wawili jamani na huyu mwanamke amenichefua sana jamaani hapa sija,mwambia ndugu yeyote na lia kwa uchungu sna
 
Pole sana Mkuu.

Ngoja kwanza nijivike uhusika wa tatizo lako
halafu nije na nasaha zenye kujenga ndoa.
 
Pole sony wega inauma sana kusalitiwa. Maumivu yake umenikumbusha maumivu yanayoanza kupona.
 
Last edited by a moderator:
pole sana aisee,wanawake wengine sijui wakoje?tupo tofauti aisee
 
kaka, naomba utulie sana, na wakati huu umuombe Mungu kuliko kipindi chochote ulichowahi kuomba katika maisha yako. Si siku nyingi nilileta uzi humu, wa kuwasisistiza watu kutokukatisha maisha sababu ya penzi. Kwa lugha nyepesi, maisha yako yana thamani sana mbele za Mungu kuliko unachokiwaza sasa. Na jifunze kuona kuwa mke wako amemkosea Mungu na siyo wewe, hivyo Mungu atamsamehe, na wewe unapaswa pia kumsamehe! Please nakuomba umsamehe mke wako, na ujismehe pia! Ni ngumu, lakini pia inawezekana!
 
nimeandika mara tatu na nikafuta..daah jamani eehh waliioooa waje watoe..ushauri wale ambao wake zao au waume zao wamekua wadanganyifu..au walifanya maana kati ya thread zote hii ni serious africa nzima yan daahh..mkuu pole sana kama angekua ni girlfriend tu.mi nigeshapotezea zamani sana..yani..ila wife nasita kutoa ushauri usio constructive..!! ila udanganyifu..ndo mwanzo wa uharibifu..!!!
 
mkuu cha kufanya fowadi hizo sms kwako then mrudishie simu yake.kumbuka kunote hizo namba za hawara zake.mchukue taratibu mwambie tunatoka out,kodi hata gari kama huna la kwako then safari yenu iishie kwao.mkabidhi kwao na waeleze kuna problem kati yenu but mpe nafasi yeye ajishtaki mwenyewe.akishindwa waachie we ondoka na mwambie hadi ameweza kusema ukweli kwao ndio anaweza kurudi nyumbani.akishasema mpe likizo ya miezi sita akae kwao.kama anajitambua atajifunza lakini kama sikio la kufa hatajirekebisha,ikiwa hivyo unatupia kwenye recycle bin unaendelea na maisha.
 
MH! Pole sana, tuliza akili na umuombe Mungu akupe hekima ya kuamua maamuzi sahihi!
 
Pole sana. Hebu kaa na Tafakari kwa makini unadhani ni kwanini mkeo afanye hivo?, je labda na wewe umewahi kutoka nje ya ndoa so na yeye anafanya revenge, je mna ugomvi unaosababisha ndoa kutotulia. Baadae kaa na mkeo mjaribu kulizungumza pia, otherwise ongea na mshenga wako katika ndoa akupe ushauri nini cha kufanya, kama ndoa yenu ni ya kikristo mshirikisheni Padri/Mchungaji aliewafungisha ndoa juu ya hilo
 
cm ni kama pm za jf
utatraaa mtupu
 
Pole sana mtu wangu ndoa inamitihani mingi sana!! narudia tena pole kwa yaliyokukuta!! najaribu kuona kama ni mimi ndio nimefanyiwa sijui moyo ungekua umechomoka au vipi? kitu cha kwanza kubali yamekufika na pamoja na kua mkeo simu yake ipo busy jaribu kuona na tabia yake,, maana wanawake wakiwa na mtu nje tena mwenye kipato kumzidi mmewe wengi hua na jeuri na utayari wa kuondoka wakati wowote!! kama sio jeuri na anajutia alichokifanya jaribu kutofikiliaa kutengana sababu ya kulinda watoto ila kama ameshaota mapembe ni bora ujiweke pembeni.. huo ni ushauri tu ila angalia mwenyewe nafsini mwako umeathirikaje na hilo jambo!!
 
Kiukweli ktk maisha hakuna chenye maumivu kama kusalitiwa ila ucmuonyeshe mkeo kwamba umegundua kuwa amekusaliti bali unapaswa kuongeza mapenzi kwake na kumfanya ajifikirie kama akiwa na akili timamu atabadilika lkn ukiongea nae sasa kuhusu hilo utakuwa ugomvi mkubwa na unaweza ukafanya kitu ambacho kutokana na hasira
 
Sijuia hata nishauri nini? Ila jamaa humu wametoa ushauri sana ila mwisho angalia utakachoamua toka moyoni, naikumbuka hii stori tena kuna mdau akakueleza utaalamu wa hiyo simu dah! Usisahau mrejesho kaka
 
Duuu pole kwa mtihan....
Niliuchangia ule uzi lakin daaaaaah!
Pole tu
 
Kwa ushauri wangu, usichukue maamuzi yoyote mbali na haya;
1. Piga magoti mwambie Mungu unapita wakati mgumu, lakini yeye ndiyr mwenye jibu sahihi
2. mwambie mke wako live, kuwa umepata hizo, meseji, mwambie wewe unaongea na Mungu, mwambie hivyo, mwambie lakini umeumia sana sana, mwambie hukutegemea, mwambie kuwa unajipa muda wa kujua itakuwaje
3. usimwambie mtu yeyote, maana baadae unaweza kusamehe kwa ajili ya mlee watoto, sasa utaona aibu mbele za uliowaambia
4. Kama unahela kidogo, aaga mwambie mke wako unaenda kupumzika kidogo siku mbili hoteleni, mwambie kabisa kuwa unahitaji uulivu wa akili
5. mwambie mke wako, katika yote, maisha yetu lazima yaendelee, kwamba hutamdhuru wala wewe hutajidhuru

HII ITAKUPA MUDA WA KUPIMA MAMBO KWA UNDANI, UKIAMUA LEO, MARA NYINGI JIBU HALIWEZE KUWA SAWA, KIKUBWA ANGALIA NAMNA YA WEWE KUJIPA RELIEF, IKIBIDI YEYE USIMWAMBIE, HATA USEME UMEENDA SAFARI, ILA KWELI MESEJI ZAKE FORWARD KWAKO, NA UCHUKUE NAMBA ZA WALIOTUMA

POLE SANA, MUNGU AKUSAIDIE
 
mkuu cha kufanya fowadi hizo sms kwako then mrudishie simu yake.kumbuka kunote hizo namba za hawara zake.mchukue taratibu mwambie tunatoka out,kodi hata gari kama huna la kwako then safari yenu iishie kwao.mkabidhi kwao na waeleze kuna problem kati yenu but mpe nafasi yeye ajishtaki mwenyewe.akishindwa waachie we ondoka na mwambie hadi ameweza kusema ukweli kwao ndio anaweza kurudi nyumbani.akishasema mpe likizo ya miezi sita akae kwao.kama anajitambua atajifunza lakini kama sikio la kufa hatajirekebisha,ikiwa hivyo unatupia kwenye recycle bin unaendelea na maisha.[/QUOTEo ].......Mkuu chicco hapa jamaa umemshauri vizuri sana....MKUU CHUKUA USHAURI HUU
 
Msamehe tu jamani, shetani atakuwa alimpitia. Toka huko ulikojifungia kwanza. Usiongee nae ukiwa na hasira. Ila kama hujawahi kumcheat toka mna-date hadi leo usimsamehe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom