Mbalamwezi
JF-Expert Member
- Sep 30, 2007
- 800
- 171
Taarifa za kusitikisha ni kwamba wanafunzi 12 wamefariki kwenye ajali ya moto uliounguza bweni la wanafunzi katika shule ya sekondari Idodi, Iringa. Wengine 22 wamejeruhiwa, kati yao vibaya sana.
Mazishi ya pamoja
Serikali imeamua kuwazika wanafunzi hao kwenye kaburi moja kutokana na ugumu wa kuwatambua baada ya kuungua sana.
Wanafunzi walionusurika wanasema moto ulianza baada ya
mshumaa mkuunguza chandarua wakati mwenye nao alipopitiwa na usingizi, lakini wakati wakijaribu kujinusuru, kuna mtu alikuwa (kwa maelezo, ni mwanamume mwenye nguvu 'sana' ) akisimama mlangoni na kuwazuia wasitoke, akiwaambia wale lazima wafie mle ndani.
Wakati huo huo, wanafunzi hao wanasema walisikia pia harufu ya mafuta ya petroli.
Ni nani? na kwa sababu gani hasa afanye hivyo? Je ni kweli chanzo cha moto ni mshumaa, au huyo mtu aliwasha kwa petroli? Je kuna nia gani thabiti ya kutafuta ukweli, huku taarifa za awali zikiunga mkono hoja kuwa chanzo ni mshumaa?
Je, tumejifunza nini na hatua gani tumechukua toka majanga ya moto mashuleni ya miaka ya nyuma? Kuna tahadhari gani dhidi ya ajali za moto mashuleni? tuna vifaa vya kuzimia moto mabwenini? wanafunzi wanajua kuvitumia? Tuna mafunzo ya kukimbia hatari mashuleni?
Kuna maeneo ya dharura ya kutokea wakati wa hatari?
Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo tunapaswa kujifunza kwa vitendo sasa na siku zijazo, ili tupunguze vifo vya watoto wetu kwa namna hii.
Poleni sana Watanzania.
Mazishi ya pamoja
Serikali imeamua kuwazika wanafunzi hao kwenye kaburi moja kutokana na ugumu wa kuwatambua baada ya kuungua sana.
Wanafunzi walionusurika wanasema moto ulianza baada ya
mshumaa mkuunguza chandarua wakati mwenye nao alipopitiwa na usingizi, lakini wakati wakijaribu kujinusuru, kuna mtu alikuwa (kwa maelezo, ni mwanamume mwenye nguvu 'sana' ) akisimama mlangoni na kuwazuia wasitoke, akiwaambia wale lazima wafie mle ndani.
Wakati huo huo, wanafunzi hao wanasema walisikia pia harufu ya mafuta ya petroli.
Ni nani? na kwa sababu gani hasa afanye hivyo? Je ni kweli chanzo cha moto ni mshumaa, au huyo mtu aliwasha kwa petroli? Je kuna nia gani thabiti ya kutafuta ukweli, huku taarifa za awali zikiunga mkono hoja kuwa chanzo ni mshumaa?
Je, tumejifunza nini na hatua gani tumechukua toka majanga ya moto mashuleni ya miaka ya nyuma? Kuna tahadhari gani dhidi ya ajali za moto mashuleni? tuna vifaa vya kuzimia moto mabwenini? wanafunzi wanajua kuvitumia? Tuna mafunzo ya kukimbia hatari mashuleni?
Kuna maeneo ya dharura ya kutokea wakati wa hatari?
Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo tunapaswa kujifunza kwa vitendo sasa na siku zijazo, ili tupunguze vifo vya watoto wetu kwa namna hii.
Poleni sana Watanzania.
Last edited: