vurugu

Paulo Twaakyondo
No Wikipedia entry exists for this tag
  1. DuaZaMama

    PostGE2025 BAKWATA mkoa wa Morogoro yaunga mkono kufanyika kwa uchunguzi vifo vya Oktoba 29

    Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Morogoro limeunga mkono agizo la Serikali ya Awamu ya Sita kutaka vyombo vya ulinzi na usalama kuchunguza vifo vilivyotokea baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29. . Sheikh wa Mkoa huo, Twaha Kilango, amesema uchunguzi wa haraka unahitajika ili...
  2. Waufukweni

    PostGE2025 Rais Samia: Nitaunda Tume ya Maridhiano na Upatanishi ‘baada ya kujua kiini cha vurugu’

    Rais Samia amesema ataunda tume ya maridhiano na upatanishi na kuanza mchakato wa mabadiliko ya Katiba baada ya kujua kiini cha vurugu kwenye uchaguzi mkuu.
  3. Idugunde

    PostGE2025 Mwamposa kama ni Nabii wa Mungu wa kweli mbona alimuombea rais Samia na vurugu zikatokea?

    Nabii wa wa kweli kama Elia, Samwel na Elisha walikuwa wanakemea maovu. Utekaji, ufisadi kupendelea familia za watawala., Kama Mwamposa ni nabii wa kweli mbona aliomba na kumuwekea mikono Rais Samia lakini watanzania wamemkataa na kuleta vurugu? Nabii wa kweli hawezi kufumbia ufisadi...
  4. R

    Vijana wajasiriamali Dar es Salaam wahimiza vijana wenzao kulinda amani na kuepuka vurugu

    Hizi ni propaganda na miradi ya Serikali, sidhani kama ni akili zao timamu :COFFEE: Vijana kwa sasa tunapanga Disemba 9 kudai haki ------------- Vijana wajasiriamali kutoka Mkoa wa Dar Es Salaam wametoa wito kwa Vijana wengine nchini kuienzi na kuilinda amani ya Tanzania na kujiepusha na...
  5. DuaZaMama

    Polisi Kanda Maalum DAR inamshikilia Charles Gisima kwa Tuhuma za Kuchochea uvunjifu wa amani

    TAARIFA KWA UMMA Jeshi la Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam tarehe 12/11/2025 majira ya saa 8:00 mchana eneo la Madale kwa Swai Kinondoni limekamata na linamhoji Charles Gisima Werema (miaka 47), mkazi wa Madale Flamingo Kinondoni kwa tuhuma za kuhamasisha na kuchochea uvunjifu wa amani katika...
  6. R

    PostGE2025 DC Ilala ahimiza ujenzi upya wa Ofisi zilizoharibiwa wakati wa Vurugu Oktoba 29

    Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amewataka watumishi wa umma katika wilaya hiyo kuendelea kutoa huduma kwa wananchi licha ya changamoto zilizojitokeza baada ya baadhi ya ofisi zao kuharibiwa. Akizungumza wakati wa kufanya tathmini ya maeneo yaliyoharibiwa, Mpogolo alisema kuwa Serikali...
  7. R

    GE2025 Askofu Shoo: Tumesikitishwa na Matukio yaliyotokea Oktoba 29, vurugu hazijawi kuleta amani

    Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Kaskazini, Askofu Dkt. Fredrick Onael Shoo, amesema vurugu katika Taifa lolote hazijawahi kuleta amani, akirejea machafuko yaliyoshuhudiwa katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29 mwaka huu akiwaomba Watanzania kumuomba Mungu kwa bidii...
  8. Dalton elijah

    Kipi Kifanyike Nchini Tanzania Baada ya Vurugu za Uchaguzi na Maandamano Yaliyosababisha Vifo?

    Kufuatia vurugu za uchaguzi na maandamano yaliyosababisha vifo nchini Tanzania, hatua madhubuti zinahitajika kuchukuliwa ili kurejesha amani, utulivu, na kuimarisha demokrasia. Hali kama hii mara nyingi huashiria mgogoro wa kisiasa na kijamii unaohitaji mbinu za kina na shirikishi kushughulikia...
  9. Mangwea1900

    Maandamano au vurugu?

    Tuzungumze ukweli kuhusu kilichotokea ni maandamano au vurugu? Walipovunja maduka yetu na kutupora hela ilikuwa ni sehemu ya maandamano au vurugu? Kilichotokea nani alikuwa akiratibu na yeye alikuwa nasi road au? Tupeane pole ila majeraha yake yatadumu kwa muda mrefu
  10. M

    Wazazi wengi hawajawaruhusu watoto wao kwenda shuleni. Bado wana hofu ya vurugu

    Nimegundua kuwa Wazazi wamewazuia watoto wao kwenda shuleni. Hofu bado ni kubwa sana. Wanasikilizia kama kweli hali ya utulivu na amani imerudi
  11. Keynez

    Nafanya zoezi kubwa la kuwatambua waliochochea vurugu

    Niliwahi kuonya kuwa maandamano kama yale ya 29/10/2024 yangepata ugumu kufanikiwa kwa sababu wanaopanga walitangaza muda mrefu na kuwapa upande wa pili muda na nafasi ya kujipanga kwa Plan A, B, C hadi D. Nina theory moja ambayo ninayo na naendelea kuifanyia kazi inayosema kuwa baada ya vyombo...
  12. funaku

    KISAIKOLOJIA :ALIYESHIRIKI KUHARIBU MALI NA KULETA VURUGU ILIYOPELEKEA VIFO HATOISHI KWA AMANI

    Ukishashiriki katika harakati zenye kuishia katika kuharibu mali ya mtu au yenye maslahi na roho za watu basi ujue hutokaa salama kihisia na kiroho. Leo hii wapo waliopoteza ndugu zao au baba zao kisa ulishiriki kuleta vurugu hakika danu yako na vizazi vyako havitokuwa salama kiroho. Hilo ni...
  13. R

    GE2025 Hasira za wananchi kwa Media za Tanzania kukaa kimya kuhusu Mauaji na vurugu zilizokuwa zinaendelea Uchaguzi Oktoba 29

    Media za Tanzania zinapaswa kulaumiwa sanaa kwa kilichotokea na kinachoendelea kutokea haiwezekani media za nje ndiyo zitoe ripoti kuhusu maovu na mauaji yaliyotokea kwa vijana wetu, uchafu unaofanywa na serikali ya huyu mama lakini media za ndani zipo kimya kazi kupaka mafuta Kwa hali hii...
  14. gallow bird

    Waliochochea vurugu washughulikiwe

    Watu wameuawa, biashara, makazi, miundombinu imechomwa, maisha yametatizwa, nchi imechafuliwa Yote haya yanatokana na wanasiasa na wanaharakati wao kuchochea vurugu mitandaoni na kauli zao za kuhamasisha kwenye majukwaa ya kisiasa. Wanasiasa na wanaharakati wote washughulikiwe mara moja Ili...
  15. Idugunde

    Kwanini hawataki kukubali kuwa upendeleo wa familia zao na ufisadi umesababisha vurugu?

    Kwamba familia za Kikwete, Mwinyi, Rais Samia na wengineo ndio wanafaidi keki ya taifa. Huku majority wanahangaika hata kupata ugali dagaa. Leo hii wanasema waandamanaji ni vibaka. Ufisadi, kujipendelea, wizi wa mali za umma, kudharau wananchi na kuwaona wajinga ni balaa kwa taifa
  16. Lord Denning

    Papa asema mamia wameuwawa Tanzania kwa vurugu za Uchaguzi

    Kwenye Ibada ya leo. Baba Mtakatifu Papa Leo ameziombea Tanzania na Sudan na kueleza mamia ya watu wameuwawa nchini Tanzania kutokana na vurugu za Uchaguzi Samia elewa tu we jiapishe ila inyeshe mvua liwake jua sio tu sisi Watanganyika bali dunia nzima haitakuacha salama kwa kutuua Watanganyika...
  17. DuaZaMama

    GE2025 Polisi wadhibiti vurugu Ubungo Kibo, magari yakwama kwa muda

    Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam, limedhibiti vurugu zilizokuwa zinafanywa na baadhi ya watu katika eneo la Ubungo Kibo kuanzia saa 4:00 asubuhi hii ya Oktoba 29, 2025. Watu hao walianza kufunga Barabara ya Morogoro kwa kupanga mawe na kuyarushia mawe magari yaliyokuwa yakipita...
  18. Mafyangula

    GE2025 Kamanda Suleiman: Vurugu na machafuko hayatatui migogoro

    Kuna wakati kama haki hakuna na wanapaswa kutoa haki awazitoi hizo haki ni lazima itumike nguvu ya ziada ili haki ipatikane. Kwahiyo msiseme ni machafuko ni katika harakati za kutafuta haki na usawa. ==================== Wazazi Mkoani Mtwara wametakiwa kuzungumza na vijana wao juu ya umuhimu wa...
  19. M

    Mwananchi abebwa msobemsobe mahakama kuu Dar akidaiwa kupiga kelele wakati kesi ya Lissu ikisubiriwa kuanza

    Mwananchi alikitolewa katika mahakama Kuu Masjala Ndogo Dar es Salaam leo Oktoba 22, 2025, baada ya kudaiwa kuzungumza kwa sauti kubwa ndani ya mahakama wakati kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chadema, Tundu Lissu ikiendelea
  20. Zacht

    Makundi kama ISIS, Al-Qaeda ,Hamas n.k, Yametokana na vurugu za kisiasa sio dini

    Hardtimes create tough men Machafuko na vurugu za kisiasa, ukosefu wa elimu sahihi ya dini,elimu ya kiraia na mateso ya kijamii(uongozi) vilizalisha kizazi cha vijana wenye hasira waliokua kutokana na mazingira magumu vikapelekea makundi haya kuzaliwa si kwa misingi ya Qur’an. Asili ya vikundi...
Back
Top Bottom