Katibu wa Baraza la Vijana wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (BAVICHA) jimbo la Lupembe, Abedinego Sunday Sanga, anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana akiwa katika duka lake la madawa eneo la Matembwe, Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.
Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Njombe, Seth Vegula...
Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo Kenani Laban Kihongosi atakuwa na Mkutano na waandishi wa Habari Leo katika ukumbi wa White House CCM Makao Makuu Dodoma kuanzia saa 10:30 Jioni
https://www.youtube.com/live/X01I9hqOryk?si=sqHbFxhy5Se9-ofP
Mgombea urais kupitia chama cha mapinduzi CCM...
Wananchi wa Jiji la Dar es Salaam wamesema wako tayari kushiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, wakijitenga na ushawishi wa mitandaoni unaotaka kuwapotosha kwa maandamano au kutoshiriki kupiga kura. Wamesisitiza kuwa wanatambua vyema umuhimu wa amani na athari za vurugu...
:Uongozi ndani ya CCM si cheo, bali ni dhamana inayopatikana kwa safari ya majaribio, maumivu, subira na kujitoa bila masharti. Wapo waliogombea na wakashindwa, lakini hawakurudi nyuma wala kuhama Chama. Walitumikia chama kwa nguvu zote, wakajenga imani, na leo wamepewa tena nafasi ya kugombea...
Mgombea ubunge wa Jimbo la Temeke kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Sheikh Ponda Issa Ponda, amesema kuwa iwapo atachaguliwa kuongoza wananchi wa jimbo hilo, atahakikisha mfumo wa elimu unapewa uangalizi bora na unafanya kazi vizuri
Akizungumza Oktoba 4,2025 kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika...
WAUMINI wa Dini ya Kiislamu wameshauriwa kutoshiriki maandamano yanayohamasishwa kwenye mitandao ya kijamii yaliyopangwa kufanyika Oktoba 29, mwaka huu, na badala yake wajitokeze kupiga kura kwa amani katika Uchaguzi Mkuu wa tarehe hiyo.
Wito huo ulitolewa jana Oktoba 4,2025 na Shehe wa Msikiti...
"Nendeni mkawaambie kwamba ni nchi gani duniani inawapa watu wake mikopo isiyo na riba?. Wakaangalie, mara nyingi wanapenda ku- google vitu ambavyo vinavunja amani, wa- Google sasa vitu ambavyo vinajenga amani yetu"- amesema Mkuu wa Wilaya ya Ilala Edward Mpogolo
Octoba 4, 2025 Mkuu wa wilaya...
Mgombea ubunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kigoma Kusini, Nuru Kashakari (Kandahari), ameahidi kujenga kituo cha afya ndani ya miezi sita baada ya kuapishwa, akitumia fedha zake binafsi, ili kusogeza huduma za afya karibu na wananchi ambao kwa sasa wanalazimika kusafiri zaidi ya saa...
Wakuu, sasa hivi ni saa 4 asubuhi lakini sioni chochote kinachoendelea. Je, CCM wamemaliza kampeni zao pale Babati, Manyara? Au kile kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya CCM kimeathiri mwenendo wa kampeni? Naomba ufafanuzi.
Rais wa Jumuiya ya Wanafunzi wa Taasisi za Elimu ya Juu nchini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kampeni ya Mama Asemewe, Geofrey Kiliba, amesema kuwa mwezi wa Oktoba ni kipindi muhimu mno kwa Watanzania kuungana na kushikamana kwa dhati ili kuonesha mshikamano wa kitaifa na kuendeleza amani. Kiliba...
Mgombea Ubunge Jimbo la Kigoma Mjini Kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Clayton Chipando Maarufu Baba Levo ametoa ufafanuzi kuwa siku ya tarehe 11 na tarehe 12 Oktoba 2025 Jimbo la Kigoma Mjini linatarajia kupokea Ugeni Mkubwa wa madaktari Bingwa ambao watatoa huduma ya matibabu
Madaktari hao...
"Itakuwaje Rais wa nchi anaulizwa kuhusiana na raia wake atakwenda lini peponi huyu maana yake ana maswali ambayo ya madhambi yake mwenyewe hajayamaliza anaulizwa kuhusu watu wewe ulikuwa ikulu kuna watu kule majangwani, maporini kulikuwa kunatendeka hivi na hivi na wewe ndiye mtawala...
TAARIFA KWA UMMA
Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kati tunatoa taarifa kwa umma na kulaani kitendo cha utekaji wa kiongozi wa kata ya Ikungi anayejulikana kwa jina la Issa Hamis Kaudo na kijana wa boda boda Ndugu Paul Veslas.
Jana tarehe 03.10.2025 mnamo saa 12 jioni Issa...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro limeandaa mazoezi ya pamoja ya utayari kwa kushirikiana na vyombo vyote vya ulinzi na usalama mkoani humo. Mazoezi hayo yalilenga kuimarisha mshikamano, mawasiliano, na uwezo wa pamoja katika kutekeleza majukumu ya kulinda raia na mali zao.
Kada wa CCM Iringa ambaye hapo nyuma alikuwa ni kiongozi wa juu wa chadema ngazi ya mkoa na kanda ajikuta akiishiwa pawa na kuipiga salamu ya “Peopleeeees power” badala ya ile ya “CCM hoyeeee”
Mgombea ubunge Jimbo la Hanang kupitia CCM, Asia Halamga amesema wema alioufanya mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi CCM, Dk Samia Suluhu kwa wananchi wa Hanang utaishi milele.
Aliyewahi kuwa mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha Cecilia Paresso amesema lengo la chama cha siasa ni kushika dola kupitia uchaguzi hivyo inapotokea chama kikasusia anadai chama hicho hakifai.
"kama tunavyofahamu malengo makuu ya chama cha siasa ni kushiriki uchaguzi ili kuweza kushika dola...
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga Mjini kupitia Chama cha ACT Wazalendo, Seif Abalhassan, ameahidi kurejesha heshima ya Jiji la Tanga endapo wananchi watampa ridhaa kwenye uchaguzi ujao.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Kiongozi mstaafu wa ACT Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe...
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Ubungo kupitia CCM , Professa Kitila Mkumbo amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutambua kadhia wanayopitia wananchi juu ya usafiri wa mabasi yaendayo haraka (mwendokasi) alielekeza kuharakishwa kwa taratibu za kuondosha mabasi bandarini ili yaanze kazi haraka na...
Geofrey Kiliba, Rais wa Jumuiya ya Taasisi za Wanafunzi wa Elimu ya Juu Tanzania (TAHLISO), amesisitiza kuwa wanafunzi wa vyuo na vyuo vikuu kote nchini watashiriki kikamilifu katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.