Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana wa ACT Wazalendo Taifa, ambaye pia ni Meneja wa Kampeni wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe, Abdul Nondo, amesema miaka mitano iliyopita ya uongozi nchini imeshuhudia ongezeko la matukio ya utekaji watu bila hatua madhubuti kuchukuliwa, huku...
Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limeufungia wimbo mpya wa msanii wa Hip Hop, Roma Mkatoliki, uliopewa jinala “Teremsha Bunduki”, ikiwa ni siku chache tangu ulipotoka rasmi.
Taarifa ya BASATA ya leo Oktoba 21, 2025, imesema wimbo huo umevunja kanuni za Baraza, na kwa hivyo umezuiliwa...
Mgombea wa nafasi ya Ubunge Jimbo la Kibamba Mkoani Dar Es Salaam kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Angellah Kairuki amesema katika kipindi kifupi alichofanya kazi chini ya Rais wa awamu ya sita na Mgombea Urais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amekuwa shahidi wa huruma, imani na kujali kwa...
Tanzania inaamua
Rais wa Tanzania Suluhu ashtakiwa kwa kuwafungia washindani nje ya kinyang'anyiro siku chache kabla ya uchaguzi
-------------
Shirika la Kimataifa la Amnesty International limetoa taarifa ikieleza kuwa mamlaka za Tanzania zimeongeza ukandamizaji dhidi ya wapinzani wa kisiasa...
Viongozi wa jamii ya Kimaasai nchini Tanzania, maarufu kama Malaigwanani, wametoa tamko rasmi la kuunga mkono kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025, huku wakipinga vikali wito wa maandamano unaosambazwa katika maeneo mbalimbali nchini.
Tamko hilo limetolewa katika eneo la Donyomorwak...
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Benjamin Kuzaga Oktoba 20, 2025 amewaongoza Maafisa, Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali kufanya doria ya Magari, Miguu na Mbwa wa Polisi kuzunguka maeneo mbalimbali ya Mkoa huo.
Akizungumza mara baada ya doria...
Mgombea wa Uwakilishi Jimbo la Kiwani, Hemed Suleiman Abdulla, amesema wakati umefika kwa wananchi wa Kiwani kuchagua viongozi wanaoweza kuwatumikia na kuwaletea maendeleo jimboni humo.
Ameyasema hayo kwa nyakati tofauti alipozungumza na kuomba kura kwa wananchi wa vijiji vya Kendwa...
Malaigwanan Kilimanjaro waahidi kuwachagua walinda amani na mshikamano wa Taifa_ Viongozi wa Jamii ya Kimasai nchini Tanzania maarufu kama (Malaigwanan) wametoa tamko lao rasmi kwa nchi nzima, la kuunga Mkono kufanyika kwa uchaguzi Mkuu wa Tanzania wa Oktoba 29, 2025, wakilaani uwepo wa hamasa...
Wakuu,
Sheikh Sharifu Firdaus Al qadiri anatema cheche, lakini ajabu ameshindwa kukemea namna ambavyo Serikali imekaa kimya kwa Matukio maovu ya utekaji na watu kuuliwa pamoja na ufisadi unaofichuliwa na wakina Mange dhidi ya Serikali ya huyo Samia, yeye amekazia matusi na Maadii ya Kitanzania...
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Almachius Mchunguzi, amewahimiza wananchi wa Mkoa wa Tanga kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika tarehe 29 Oktoba 2025, akibainisha kuwa hakuna tishio lolote la amani...
Mgombea Urais wa ACT Wazalendo ahitimisha Kampeni Pemba Kwa hamasa na shangwe Mgombea Urais wa ACT Wazalendo, Othman Masoud Othman, Oktoba 20, 2025 ameanza wiki ya mwisho ya kuhitimisha rasmi kampeni za kuelekea uchaguzi mkuu wa tarehe 29 Oktoba.
Mamia ya wanachama, wapenzi na viongozi wa...
Picha mbalimbali zikimuonesha Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, SACP Safia Jongo, akikagua gwaride na kuzungumza na Maafisa, Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali katika viwanja vya Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Geita, Oktoba 20, 2025.
Ukaguzi huo ni sehemu ya tathmini ya mifumo ya utendaji...
Mimi kaniacha hoi baada ya kusema hadi mwanae kama akihama chama cha CCM na kwenda upinzani basi yeye hatohusika naye!
Yani kisa chama kweli kabisa unaikataa damu yako?
================
MKUU wa Mkoa wa Kagera, Hajat Fatma Mwassa, amekanusha madai ya kushiriki siasa katika Jimbo la Bukoba...
Mkuu wa wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro, Mhe. Hassan Bomboko amefanya ziara ya kuwatembelea na kuzungumza na maafisa wasafirishaji (waendesha bodaboda na Bajaj) Wilayani humo na baadae alipata nafasi ya kuhudhuria mkutano mkuu wa Umoja wa Bajaj uliohudhuriwa na zaidi ya madereva bajaji 650...
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imesema itamtangaza mshindi wa kiti cha Urais ndani ya muda usiozidi saa 72, baada ya zoezi la upigaji wa kura kumalizika Oktoba 29 mwaka huu, na washindi wa nafasi ya Ubunge na Udiwani, wakitarajiwa kutangazwa wakati wowote baada ya kujumlisha idadi ya...
Ndugu zangu Watanzania,
Napenda kuwaambieni ya Kuwa hakuna Mtanzania hata mmoja ambaye ataandamana hata kuzunguka tu uwanja wake au sebuleni kwake au chumbani kwake au nyumbani kwake siku ya uchaguzi.
Watanzania wote wamejiandaa kikamilifu kabisa kushiriki uchaguzi . Na kikubwa zaidi ni shauku...
GT
Ivi unaanzaje kupoteza mda kwenda kumchagua Samia.Wenye mtindio wa ubongo pekee ndiyo watapiga kura
1.Kauza Bandari na Rasilimali zingine nyingi tu
2.Kafukuza wamasai Ngorongoro kwa uonevu mkubwa.
3. Deni la Taifa Tr107 bila maendleo ya kuonekana
4. Muuaji na mtesaji.Mkubwa huyu hana...
Jamani njooni msikilizeni mzee wa protokali Steve Nyerere! Hapo kashapata posho yake ya kifisadi basi ananguvu zote za kutanua mdomo wake
===============
Watanzania wamenituma, wameniambia Nyerere tunatoka kwenda kupiga kura tunatoka kwenda kutiki, wamama wa Tanzania wamenitumia meseji Nyerere...
Kwahiyo ukiboresha maeneo ya vijiji ndio suluhu la vijana kuyasaka maisha mijini?
Hizo ni sera za uongo hakuna kitachofanikiwa! Na katika utafuta wa maisha ni maono ya mtu tu ndio maana kuna wanaotoka mjini kwenda vijijini na wakafanikiwa so kila mtu anauhuru wa kutafuta maisha popote pale...
Maendeleo ya Tanzania bado ni duni sana.
Shule nyingi vijijini zimechoka hazina vyoo, madarasa,. Zahanati nyingi vijijini zimechoka.
Alafu mgombea wa Chama tawala anazunguka na wasanii, mabasi 200, wafuasi na chawa wa chama zaidi ya 10000 kwa gharama kubwa.
Kwa nini hizo pesa zisitumike kwa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.