tcra

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (pia huitwa kwa Kiingereza: Tanzania Communications Regulatory Authority ambapo mara nyingi huitwa kwa kifupi: TCRA) ni taasisi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yenye majukumu ya kusimamia sekta za mawasiliano na utangazaji.

TCRA Ilianzishwa kwa Sheria ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Na. 12 ya mwaka 2003 kusimamia huduma za kielektroniki na posta na masafa ya mawasiliano nchini Tanzania. Mamlaka ilianza kazi tarehe 1 Novemba 2003 na inafanya shughuli za zilizokuwa Tume ya Mawasiliano Tanzania (TCC) na Tume ya Utangazaji Tanzania (TBC).

Mamlaka ya TCRA ni kusimamia sekta ya posta, mawasiliano ya kielektroniki na utangazaji katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ikiwa ni pamoja na:
  • Kuzifanya shughuli za TCRA kuwa za kisasa kwa kutumia teknolojia sahihi;kuimarisha tafiti zenye ubora katika huduma zinazodhibitiwa, uwezo na umahiri wa watumishi.
  • Kukuza ufanisi; kuaminika na kuhakikisha usalama wa miundombinu ya mawasiliano na matumizi yake.
  • Kukuza ufanisi na unafuu wa huduma za Mawasiliano na kuongeza upatikanaji wa huduma za Posta na TEHAMA katika maeneo yasiyohudumiwa ipasavyo na yale yasiyo na huduma kabisa.
  • Kulinda maslahi ya wadau na kukuza uelewa wa haki na wajibu wao.
  • Kufuatilia utendaji wa huduma zinazosimamiwa na kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na Kanuni kwa viwango vinavyostahili.
  • Kuratibu utekelezaji wa ahadi za kisekta kitaifa, kikanda na kimataifa.
  • Kufikia kiwango cha juu ya kuridhisha wateja kama ilivyoainishwa kwenye Mkataba wa Huduma kwa Mteja wa TCRA.
  • Kuendelea kuzingatia matakwa ya kisheria na kiusimamizi.

Sera zinazoathiri utendaji kazi wa TCRA ni pamoja na:
  • Sera ya Taifa ya Mawasiliano ya mwaka 1997
  • Sera ya TEHAMA ya mwaka 2003
  • Sera ya Taifa ya Posta ya mwaka 2003
  1. JamiiForums Tanzania TCRA yafuta akaunti yake ndani ya X/Twitter. Je, ni maandalizi ya kuifungia mtandao huo wa kijamii?

    Japo hatua hiyo inaweza kuwa imetokana na sababu nyingine, ukweli kwamba imetokea katika kipindi hiki cha vuguvugu kubwa kuishinikiza serikali iifungie X/Twitter unweza kuyumkinisha kuwa hizi ni dalili za awali za mtandao huo wa kijamii kufungiwa. Hata hivyo, wakati viongozi mbalimbali wakuu wa...
  2. JamiiForums Tanzania Serikali imekaa kimya kuhusu matapeli wa mtandaoni

    SERIKALI YA ZANZIBAR IMEKAA KIMYA KUHUSU HAWA MATAPELI WA MTANDAONI HII NI HATARI KWA WATU WANAOTAKA KUFANYA BIASHARA ZANZIBAR KUONA MATAPELI @soknibike WEZI WANAKUMBATIWA NA SERIKALI SASA WANANCHI WOTE KUWENI MAKINI NA HAWA SOKONI BUKE TUNAOMBA JESHI LA POLISI ZANZIBAR LIWASHULIKIE...
  3. N

    JamiiForums Tanzania TCRA Mjibuni Asha Baraka, alifanya maombi ya leseni ya redio hajajibiwa hadi leo

    Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, tunawaomba jitokezeni na kumjibu mteja wenu aliyeomba leseni ya kumiliki kituo cha redio, kwa masikitiko makubwa hakujibiwa zaidi ya kuzungushwa kutokupewa sababu ya kunyimwa. Akihojiwa kwenye kipindi cha The Classic kinachorushwa na kituo cha EFM 93.7 Mhz Asha...
  4. JamiiForums Tanzania Waziri Nape akiri kufuatilia mijadala inayoendelea kuhusu mtandao wa X kufungiwa, asema TCRA itatimiza wajibu kuhakikisha watoto wanakuwa salama

    Waziri wa Habari, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Nape Nnauye amesema wanaona mijadala yote inayoendelea (kuhusu maoni ya kama mtandao wa X ufungiwe au laah) na kusema Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), itatimiza wajibu wake wa kuhakikisha Tanzania na hususani kizazi cha Watoto kipo...
  5. C

    JamiiForums Tanzania SoC04 Changamoto ya Upatikanaji wa Taarifa Nchini Tanzania: Lianzishwe Jukwaa la Kati la Taarifa (Centralized Information Platform)

    Utangulizi Nchini Tanzania, kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa taarifa muhimu inayosababishwa na mtawanyiko wa taarifa katika vyanzo tofauti na ukosefu wa jukwaa moja linalounganisha taarifa hizi. Hii inawafanya wananchi kupata ugumu katika kufanya maamuzi sahihi ya uchaguzi wa bidhaa na...
  6. JamiiForums Tanzania Meneja Huduma za Utangazaji kutoka TCRA asema "Waandishi wengi wa Habari hawajui kusoma tarakimu"

    Meneja Huduma za Utangazaji kutoka TCRA, Inj. Andrew Kisaka, amesema asilimia kubwa ya Waandishi wa Habari hawajui kusoma tarakimu hasa wakiandikiwa ili wasome, kwani wamezoea maneno isipokuwa tarakimu za laki kwani ndizo wanacheza nazo kila wakati, hivyo hivyo ameiomba Tume Huru ya Taifa ya...
  7. JamiiForums Tanzania Watengeneza Maudhui wa Tanzania wanatumia vibaya taarifa za watu, TCRA isaidie hili

    Kuna vijana wengi wanatengeneza maudhui ili kujipatia umaarufu au fedha mtandaoni. Hii sio shida, shida inakuja pale ambapo unatumia sura ya mtu bila kuwa na idhini yake. Tulishazungumzia hili kwa ma-mc wanachukua watu video na kuweka kwenye page zao, ambazo video hizo zinakuwa zinatweza utu wa...
  8. JamiiForums Tanzania TCRA tunahitaji jibu kwenye huu uhalifu wa 'tuma kwa namba hii'

    Tunapata ujumbe au simu kutoka kwa watu wanaotumia baadhi ya mitandao ya simu, ujumbe maarufu ni wa "ile pesa tuma kwenye namba hii", tukiacha ujumbe kuna wanaotupigia simu wakijidai ni wafanyakazi wa kampuni ya simu ambao wanakuuliza kuhusu pesa zilizotumwa kwenye akaunti yangu, hawa huishia...
  9. JamiiForums Tanzania Utapeli wa ‘hiyo pesa tuma kwenye namba hii’ umeshika kasi, nimegundua mbinu ya kuwazuia, napendekeza haya yafanyike kuwakomesha

    Baada ya kugundua kila ninapojadiliana na mtu kwa simu a u meseji kuhusu masuala ya kutumiana pesa, ghafla natumiwa meseji za “hiyo pesa tuma kwenye namba hii”, napendekeza hili TCRA watunge kanuni zifuatazo za kisheria 1.) Iwe ni sharti la kisheria kwa kila mteja anayetumiwa meseji za “hiyo...
  10. JamiiForums Tanzania TCRA watangaza nafasi mbalimbali za kazi

    VACANCY ANNOUNCEMENT On behalf of Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA), Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) invites high caliber, results oriented, self-driven professionals with integrity, dynamic and suitable qualified Tanzanians to fill thirty- eight (38) vacant posts...
  11. JamiiForums Tanzania BoT, TCRA ifanye auditing kwenye mikopo ya Mpesa, Tigo na Airtel . A case of MGODI

    Rate ya BoT kwenye kampuni za kukopesha ni 3.5% as a guidance issued by BoT. A simple study imefanyika kwenye mikopo ya Vodacom kupitia Mpesa and there is huge deviation which is believed to be against BoT guideline. 1. Informant amekopa kiasi cha 84,800, Mgodi huwa wanakata kwanza riba yao...
  12. S

    JamiiForums Tanzania Enyi TCRA, siyo kosa kwa Nape kutukana mitandaoni?

    Hii ni post ya ya mhe Nape ya 23 May 2024 akimrushia tusi mwananchi. Waziri Nape anamdhalilisha sana mhe rais kwa tabia yake ya kutukana watu mitandaoni. Yeye kama waziri wa Habari na Mawasiliano alipaswa kuwa mfano mwema wa matumizi mazuri na salama ya mitandao. Lkn Nape mara nyingi amekuwa...
  13. JamiiForums Tanzania Mtaani kwangu vocha ya 500 inauzwa Tsh. 700

    Kweli hii ni maajabu. Vocha iliyoandikwa Tsh. 500 imeanza kuuzwa kwa Tsh. 700 Je, huu ni uungwana, la hasha huu si uungwana. Najaribu kujiuliza kuwa ongezeko hilo la bei limeanzia kwenye viwanda vya kuchakata vocha ama ni wafanyabishara wanafanya yao? Kama hamuhitaji tutumie vocha, basi fungeni...
  14. A

    JamiiForums Tanzania Ombi langu kwa TCRA

    Kama kichwa cha habari kinavyojieleza Hili ni ombi langu kwa mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA) Pia nimeona vyema kuleta hapa JF ili kupata maoni na ushauri kutoka kwa wadau mbalimbali Katika matumizi ya simu inaweza ikatokea mmiliki wa simu akaipoteza simu yake bahati mbaya au simu hiyo...
  15. JamiiForums Tanzania Gharama za ada ya usajili wa huduma za technolojia TCRA zinakatisha tamaa wabunifu wanaoanza (start-up innovators)

    Serikali kupitia mamlakaya mawasiliano nchini TCRA inahimiza wabunifu kubuni huduma mbalimbali za kiteknolojia ili kuchochea kasi ya maendeleo na kuboresha huduma ili kurahisisha maisha Lakini kikwazo kikubwa ni ughali wa leseni za usajili wa huduma hizo za kibunifu kwa wabunifu wanaoanza yaani...
  16. JamiiForums Tanzania Serikali yaiagiza TCRA kufatilia wanaouza vocha tofauti na bei elekezi

    Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Maryprisca Mahundi amesema Serikali imetoa maelekezo kwa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kufuatilia Wafanyabiashara wanaouza vocha za kukwangua kinyume na bei elekezi. Amesema hayo wakati akijibu swali la...
  17. JamiiForums Tanzania Tatizo la bei za vocha latua TCRA

    Baada ya jambo hili kuliweka hapa jukwani, TCRA limewafikia sasa wabapokea taarifa kutoka maeneo tofauti nchini kuhusu bei za vocha za simu. Pia soma > Vocha za mitandao tofauti Kagera zauzwa bei ya juu
  18. M

    JamiiForums Tanzania Bando sasa ziwe bila ukomo wa muda wa matumizi

    Salam kwenu. Kufuatia changamoto ya internet tunayoendelea kuipata niiombe TCRA kuyaagiza makampuni yote yanayotoa huduma za internet. 1. Kufidia wateja wote kwa kurejesha bando zilizolika ama ku expire kipindi hiki cha tufani la internet. 2. Vifurushi vyote vya internet sasa visiwe na ukomo...
  19. JamiiForums Tanzania Kwa hii Shida ya Mitandao ya simu iliyotokea leo, turuhusu Starlink iingie Tanzania

    Leo kuna shida kubwa sana ya mitandao yote ya simu tangu saa nne. Nimejikuta nayakumbuka madishi ya Elon Musk ya Starlink. NDUGU ZANGU TOA USHAURI USITUKANE ==== Pia soma: Mitandao ya simu ipige faida ya internet kwa mara ya mwisho. Elon Musk kuleta internet ya Starlink Tanzania
  20. JamiiForums Tanzania TCRA: Kuna tatizo la Mfumo wa Mawasiliano ya Intaneti kwenye Mkongo wa Baharini

    Kama umekosa huduma ya intaneti kwa saa kadhaa leo, tambua shida sio kifaa unachotumia bali ni tatizo la kiufundi lililotokea kwenye miundombinu ya intaneti iliyopitishwa baharini. Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dk Jabir Bakari amelithibitisha hilo alipotafutwa na...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…