Siku ya msiba wangu
Haoni navyoumia, sichoki kubembeleza
Kila siku ninalia, huku nikimueleza
Karibu nitajifia, Moyo ushajimaliza
Siku ya msiba wangu, kwake iwe ni sherehe
Aalike na vigoma, na wapiga vuvuzela
Kwake nimetia koma, ila anipa madhila
Aniona ja ukoma, haoni zangu fadhila
Siku ya...