Msaada ndugu nina mgogoro wa ardhi mahali ambapo bibi yangu alikuwa analima kuanzia miaka ya 80 na sidhani kama aliwahi kuwa na hati ya hilo eneo ila ndio mahali tumekuwa tukipata mazao ya kula kama familia.
Sasa kuna mtu amevamia eneo baada ya bibi kufariki, sasa je nitaweza vipi kuthibitisha...
Wananchi wa Kijiji cha Ndaleta Wilayani Kiteto Mkoani Manyara wameilalamikia Halmashauri ya Wilaya hiyo wakidai imehusika kuhujumu Wananchi kwa kiwango kikubwa katika masuala ya mgogoro wa ardhi yanayoendelea.
Wameeleza kuwa wamefikisha malalamiko yao mara nyingi kuhusu mgogoro wa ardhi lakini...
Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) kimetoa wito kwa Serikali kufuatia maandamano yaliyofanywa na mamia ya wananchi wa Ngorongoro tarehe 18 Agosti, 2024, wakidai kuheshimiwa kwa haki zao za kimsingi. Maandamano haya yalionyesha hisia kali kutoka kwa wananchi wanaopinga kuondolewa kwenye ardhi...
Mwaka 2018 mzee wangu alilitoa shamba la familia lenye ukubwa wa heka 4 likiwa pamoja na miti ya mbao.
Maamuzi ya kutoa sadaka shamba la familia aliyafanya mwenyewe bila kumshirikisha mtu yeyote ndani ya familia, ni jambo lililosababisha migogoro ambayo mpaka leo imeathiri familia yetu...
SERIKALI YAAHIDI KUTATUA MGOGORO WA ARDHI KATI YA WANANCHI NA JESHI LA MAGEREZA WILAYANI NGARA MKOANI KAGERA
Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imepokea malalamiko ya mgogoro wa Ardhi kati ya Wananchi na Jeshi la Magereza katika Kijiji cha Rusumo Wilayani Ngara Mkoani Kagera.
Kauli hiyo...
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Jerry Silaa ameingilia kati mgogoro wa ardhi wa muda mrefu kati ya Wananchi wapatao 246 na muwekezaji wa Kampuni ya Tanzania Road Haulage katika eneo la Kurasini wilayani Temeke jijini Dar Es Salaam ambapo wananchi hao wanadai kutolipwa malipo...
Shalom,
Naomba kuutarifu uma na Serikali kwa ujumla kwamba mimi na wenzangu kadhaa miaka ya 2010, 2011 kulikuwa na taarifa za wazi juu ya mgogoro wa eneo hilo na ukiachana na wale ambao tayari walikuwa wamenunua wengine wote waliambiwa kuhusu eneo kuwa na mgogoro na kulikuwa na kesi...
Siku za hivi karibuni kumekuwepo na mgogoro wa ardhi baina wakazi wa Tungutungu Kata ya Mapinga Wilaya ya Bagamoyo pamoja na “kigogo”, nimefika mara kadhaa eneo hilo ni vilio vilio.
Mgogoro huo ulikuwa ukifukuta kimyakimya lakini kwa sasa umepamba moto kutokana na nyumba za wakazi wa eneo hilo...
Uongozi wa Dodoma Jiji unadai eneo hilo tunaloishi wakazi wa Kata ya Ipala Jijini Dodoma ni mali ya Serikali, wanataka kutuhamisha kwa njia ambayo tunaona siyo sahihi.
Wakati wakitaka kutuhamisha tuliomba zuio na vielelezo vinavyoonesha kwamba ni eneo la Serikali lakini hawatupi, zaidi wamekuwa...
1.0 Waheshimiwa Wabunge, tarehe 14 Februari, 2024 nilipokea barua kutoka Kanisa la EFATHA, ikiwasilisha utetezi wake kuhusu mchango alioutoa Mhe. Deus Clement Sangu, (Mb) dhidi ya EFATHA, Mchango huo ulihusu mgogoro wa Ardhi kati ya Wawekezaji kwenye Shamba la Malonje na Vijiji vinavyolizunguka...
Alihudumu kama Waziri kwa vipindi vyote viwili vya Jakaya Kikwete kama Waziri wa Ujenzi kisha Elimu. Dkt. Shukuru Kawambwa ambaye baada ya kuwa Lecturer UDSM akagombea ubunge wa Bagamoyo.
Kwenye clip anaonekana akiburuzwa na vijana kwenye changamoto ya viwanja eneo la Bagamoyo. Mafao ya ubunge...
MGOGORO WA ARIDHI TONDORONI
Kesi ya ardhi namba 85 ya mwaka 2016, iliyowahusisha wanakijiji zaidi ya 700 wa Tondoroni dhidi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Leo(03.04.24)mahakama kuu chini ya Jaji Luvanda imetupiliwa mbali kwa kufunguliwa nje ya muda (Time barred'). Mgogoro huu wa ardhi...
Siku chache baada ya baadhi ya Wakulima wa Vijiji vya Mwitikira, Ndaleta, Katikati na Ngabolo Wilayani Kiteto Mkoani Manyara wanaodai kuporwa maeneo yao ya mashamba kuamua kurejea katika mashamba hayo, baadhi yao wamekamatwa na kushikiliwa na Jeshi la Polisi wakidaiwa kuvamia sehemu ya Hifadhi...
Kutokana na mgogoro wa ardhi unaoendelea Wilayani Kiteto Mkoani Manyara, baadhi ya Wakulima wa Vijiji vya Mwitikira, Ndaleta, Katikati na Ngabolo inadaiwa wamekamatwa na Polisi na wamewekwa ndani.
Hakuna taarifa yoyote inayoendelea, Jeshi la Polisi mbona mnafanya maamuzi ambayo ni ya kidikteta...
Wakulima wa Vijiji vya Mwitikira, Ndaleta, Katikati, Ngabolo na Olboloti Wilayani Kiteto Mkoani Manyara waliodai kuporwa maeneo yao ya mashamba wamemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuingilia kati changamoto yao inayowakabili kuhusu kuporwa ardhi ya Wafugaji wakidai kuwa wanapewa nguvu na baadhi...
UPDATE: Aliyefariki ni Isore Mtegetu Marwa (28) Mkazi wa Mekomariro Wilaya ya #Bunda alijeruhiwa wakati wa vurugu zilizohusisha baadhi ya Wakazi wa Mekomariro dhidi ya Wananchi wa Kijiji cha Ryaming’orori Wilayani Serengeti ambapo pia watu wengine kadhaa wakijeruhiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa...
Mimi ni Mkazi wa Kijiji cha Mekomariro Wilaya ya Bunda, naomba jamii ijue kuwa kuna ugomvi wa ardhi kati Wananchi wa Kijiji chetu na Wananchi wa Kijiji cha Wilaya ya Serengeti, mpaka sasa kuna ugomvi mkubwa, watu wamechomana mishale.
Huu mgogoro hauwezi kumalizika kwa kuwa kuna viongozi au...
Habarini za asubuhi wakuu!
Ule mgogoro wa ardhi katikati ya Jiji la Mwanza mtaa wa Rwagasore kati ya Wananchi watano na mfanyabiashara nakumbuka walienda TAKUKURU baaae maafisa ardhi walihojiwa na DED Jiji aliondolewa kazini na mama lakini baadae Waziri Mkuu aliingilia kati na kumkabidhi...
Binafsi nichukue nafasi hii kuwashukuru Halima Mdee na Jafari Chege kwa kuwasemea Wananchi wa maeneo haya kuhusu manyanyaso ya Serikali dhidi yao.
Nianza na Kata ya Nyatwali. Kata hii ina vijiji vitatu Tamau, Nyatwali na Serengeti. Vijiji vyote viko kisheria na vilianzishwa tangu mwaka 1972...
Habarini zenu wakuu, nina suala linanisumbua kati yangu na jirani angu kuhusu mipaka.
Ni hivi jirani yangu kapanda mti wa mparachichi hii ya kisasa jirani kabisa na mpaka takribani nusu mita toka mpaka ulipo, sasa umekua na matawi mengi yamekuwa shambani kwangu ambapo nimepanda migomba...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.