Mnamo mwaka 2020 kuelekea mpaka 2021, ziwa Basotu, wilaya ya Hanang, mkoani Manyara lilikuwa linaleta madhara makubwa kwa wananchi kwa maji yake kujaa, kusambaa kwenye makazi ya watu na kusababisha mafuriko.
Nakumbuka vyombo vya habari vilitoa takwimu mwaka 2021 kuwa watu zaidi ya 90 walikosa...
Mahakama ya mkoa Manyara imemhukumu John Emmanuel (18) mkazi wa kijiji cha Malangi wilayani Babati kuchapwa viboko sita (6) baada ya kukutwa na kosa la ubakaji.
Hukumu hiyo ya kesi namba 73 ya mwaka 2021 imetolewa leo Septemba 26,2022 na Hakimu mkazi mkoa wa Manyara Mariam Rusewa.Hakimu Rusewa...
Mkoa wa Manyara uliundwa mwaka 2002 baada ya kuugawa uliokuwa mkoa wa Arusha. Bahati mbaya Baada ya Magufuli kupata urais wa Tanzania alitangaza wazi kuwa mikoa ya Kaskazini itabidi isubiri wakati mikoa mingine wakipelekewa maendeleo. Mwanzoni sikuamini, lakini sahivi ndio nimeamini ile kauli...
Waziri wa Tamisemi fika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara. Wakuu wote wa idara ni makaimu na Wizi wa fedha ni mkubwa sana.
Ni nini kinasababisha wakuu wa idara kukaimu Nafasi hizo kwa miaka na miaka?
Jeshi la Polisi Mkoani Manyara linamshikilia Petro Basco (38) mkazi wa Gabadaw Wilayani Babati Mkoani Manyara kwa kosa la kumpiga mkewe Maria Sakware (49) kwa fimbo na kumsababisha kifo huku chanzo kikielezwa kuwa mtuhumiwa kumtuhumu mkewe amechukua pesa yake kiasi cha shilingi elfu 10.
Tukio...
Kwema ndugu zangu.
Naomba kutoa yangu ya moyoni naona kama Serikali inatuchanganya kwenye masuala ya chanjo ya Corona maaana kwenye vyombo vya habari wanasema n hiari lakini huku Kiteto mkoani Manyara imekuwa tofauti wakina mama wanazuiwa kupima watoto clinic mpaka upate chanjo ya Corona na...
Taasisi Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Manyara imetoa ripoti yake kwa muda wa miezi mitatu, Januari hadi Machi 2022.
TAKUKURU imetoa elimuya rushwa na athari zake katika jamii, kwa askari wa Jeshi la Polisi eneo la Tengefu la Mirerani.
Pia imefanya semina 31, mikutano ya...
Salaam Wakuu,
UKEKETAJI NI NINI?
Ukeketaji ni ukataji wa sehemu za siri za mwanamke. Ukataji huo unahusisha maeneo nyeti. Au ni kitendo chochote kinachojeruhi uke kutokana na sababu ambazo sio za kimatibabu.
Ukeketaji unaumiza wanawake na wasichana kimaungo na kiakili na hakuna faida yoyote...
Katibu Tawala Mkoa wa Manyara, Caroline Mtapula amewataka mangariba katika Wilaya ya Simanjiro kuacha kukeketa watoto wa kike na kuwaozesha wakiwa katika umri mdogo kwani wanahaki ya kupata elimu, ni haki ya kila mtoto kike kupata elimu.
Mtapula amesema kuwa mtoto wa kike anayestahili kwenda...
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mwada wilayani Babati. Picha Mussa Juma
Babati. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali itajenga uwanja wa ndege wa Mkoa wa Manyara ambao utasaidia kukuza sekta ya utalii.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara katika...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara linawashikila Viongozi watatu wa CHADEMA kwa kosa la kufanya mkutano bila kibali katika eneo la Stendi ya Katesh wilayani Hanang.
Viongozi wanaoshikiliwa ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake (BAWACHA) mkoa wa Manyara Regula Mtei (45), Valentina Shayo (37) Mhasibu...
Jeshi la polisi mkoa wa Manyara katika operesheni zao, wamegundua kiwanda bubu kilichopo Mtaa wa Ngarenaro mjini Babati, kinachozalisha pombe kali feki zinazofungashwa kwenye vifungashio vya kampuni ya Konyagi.
Jeshi hilo limekamata shehena ya pombe hizo feki huku wakiwaweka wafanyakazi wa...
Mifugo 62,593 imekufa wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwa kukosa maji na malisho kutokana na ukame. Kati ya mifugo hiyo;
Ng'ombe - 35,746
Kondoo - 15,136
Mbuzi - 10,033
Punda - 1,670
======
Hali ya ukame inayoendelea wilayani Simanjiro mkoani Manyara imesababisha mifugo mbalimbali ikiwemo...
Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara limesema linamtafuta mkazi wa Kata ya Magugu wilayani Babati, Frednand Yohana ambaye anatuhumiwa kumbaka mtoto wake wa kumzaa mwenye umri wa miaka 11.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa huo, Benjamin Kuzaga ameyasema hayo leo Jumatatu Desemba 13, 2021 mjini Babati wakati...
MKUU wa Mkoa wa Manyara, Makongoro Nyerere, ameahidi kutumia gharama yoyote ya fedha kupeleka nyama kwa wawindaji, waokota matunda na warina asali wa jamii ya Wahadzabe, ili kuwashawishi wajitokeze kushiriki sensa ya watu na makazi ya mwaka 2022.
Wahadzabe hao ni wale wanaoishi katika Kitongoji...
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Madini ya Tanzanite yanapouzwa ovyo yanashusha thamani yake, akisema yanatakiwa kuuzwa kwa mpangilio maalum
Ameeleza hayo leo akizungumza na Wananchi Manyara na kuongeza, "Endapo yatauzwa kwa mpangilio na kuachiwa kidogo kidogo duniani thamani yake itapanda"...
Mkurugenzi wa Mashitaka ya jinai nchini l (DPP)amemfutia Mashtaka ya uhujumu uchumi yaliyokuwa yakimkabili Mahakamani mhadhiri wa Chuo kikuu cha SAUT tawi la Arusha, Subilaga Masebo na wenzake wanne.
Akiwasilisha maombi ya kuondoa shtaka hilo, mwendesha mashtaka wa serikali Lusiana Shaban...
Babati. Mkazi wa mtaa wa Kiongozi Mjini Babati mkoani Manyara, Lucas Mangu (46) amefariki dunia kwa kujinyonga mara baada ya kumuua mke wake Anna Kisino (41) kwa kumpiga kutokana na wivu wa kimapenzi.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Marrison Mwakyoma akizungumza na Mwananchi Digital leo...
Mkazi wa Kijii cha Ng’wandakw, Kata ya Haydom Wilayani Mbulu Mkoani Manyara, Philemon Tandu (50) amefariki dunia kwa kujinyonga baada ya kuachwa na mke wake akiwa na watoto watano.
Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, kamishna msaidizi (ACP) Marrison Mwakyoma akizungumza jana alisema tukio...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.