Manyara: Amuua mkewe kisa Tsh. elfu kumi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Jeshi la Polisi Mkoani Manyara linamshikilia Petro Basco (38) mkazi wa Gabadaw Wilayani Babati Mkoani Manyara kwa kosa la kumpiga mkewe Maria Sakware (49) kwa fimbo na kumsababisha kifo huku chanzo kikielezwa kuwa mtuhumiwa kumtuhumu mkewe amechukua pesa yake kiasi cha shilingi elfu 10.

Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara, ACP Benjamin Kuzaga.

Kamanda Kuzaga amesema kiini cha tukio hilo ni ulevi wa mume wa marehemu ambapo alichukua hatua mkononi kwa kumchapa na fimbo na kumsababishia majeraha mwili mwake ikiwemo maumivu katika mguu wake wa Kushoto pamoja na kumvunja mkono wa kushoto.

Marehemu alifikishwa katika kituo cha Afya cha Bashnet kwa ajali ya kupata matibabu na ndipo umauti ulipomkuta.

Hata hivyo Jeshi la Polisi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo kwa kusababisha kifo cha mkewe na upelelezi utakapokamilika atafikishwa katika vyombo vya sheria.
 
Watu wengi watakimbilia kusema ni umasikini ila nyuma ya pazia hatujui ukute ni mizozo na mifarakano ya kila siku pamoja na kiburi cha huyo marehemu.
 
Afya za watu zimekua na migogoro sana siku hizi,mtu anapigwa na umauti unamkuta kisha unajikuta kwenye Kesi ya mauaji!

Tuache kujichukulia sheria mkononi,kila mtu siku hizi ana matatizo yake ya kiafya.
 
Hawa lazima walikuwa na mgogoro,kutoelewana kwenye mahusiano yao

Hiyo la ten ndiyo kama sababu

Ova
 
Jeshi la Polisi Mkoani Manyara linamshikilia Petro Basco (38) mkazi wa Gabadaw Wilayani Babati Mkoani Manyara kwa kosa la kumpiga mkewe Maria Sakware (49) kwa fimbo na kumsababisha kifo huku chanzo kikielezwa kuwa mtuhumiwa kumtuhumu mkewe amechukua pesa yake kiasi cha shilingi elfu 10.

Tukio hilo limethibitishwa na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Manyara, ACP Benjamin Kuzaga.

Kamanda Kuzaga amesema kiini cha tukio hilo ni ulevi wa mume wa marehemu ambapo alichukua hatua mkononi kwa kumchapa na fimbo na kumsababishia majeraha mwili mwake ikiwemo maumivu katika mguu wake wa Kushoto pamoja na kumvunja mkono wa kushoto.

Marehemu alifikishwa katika kituo cha Afya cha Bashnet kwa ajali ya kupata matibabu na ndipo umauti ulipomkuta.

Hata hivyo Jeshi la Polisi limefanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo kwa kusababisha kifo cha mkewe na upelelezi utakapokamilika atafikishwa katika vyombo vya sheria.
Maisha ya tozo af mtu apite na "luteni" 1Ok bila maagizo lazma kiwake 😂😂😂
 
Back
Top Bottom