Habari wakuu,
Wakati najipanga hapa nikaona niombe mchango wa mawazo na uzoefu wenu.
Bila shaka wapo ambao mnafahamu gharama ya kumtumia mkandarasi kujenga, walau kwa kukisia tu.
Nashukuru sana kwa mchango wenu.
Hivi kwa mil. 5 naweza kujenga nyumba ndogo ya chumba 1, sebule, jiko na choo mpaka kiwango gani?
NB: Kiwanja kipo Dodoma Kisasa Au niongeze mpaka ngapi wakuu?