katiba

  1. M

    Rais Samia usikubali. CCM walikataa Katiba leo wanataka Katiba Mpya, walidhani Katiba ni ya CHADEMA tu

    Leo maji yamewafika shingoni wanakosa jinsi ya kukutoa madarakani wanaanza kujipitisha huku wakisema katiba mpya inahitajika, walidhani mfumo dume utadumu milele hawakujua mungu ndiye apangae. Sasa hivi wa CCM wanaumizwa na katiba kuliko wana Chadema.
  2. Lord OSAGYEFO

    Rais Samia, Katiba Mpya ndio suluhu ya matatizo ya Watanzania

    Rais Samia Suluhu Hassan kwanza nakupongeza sana kwa hatua mbalimbali unazochukua baada ya kuondokewa na Magufuli Mhe. Rais kama lilivyo jina lako wewe ndio Suluhu ya suala la Katiba mpya. Haya yote unayohangaika nayo kuyaweka sawa ni kutokana na Mwendazake kuona mapungufu yaliyopo kwenye...
  3. T

    Suala la Tume Huru au Katiba hatma yake ni Madaraka na si maslahi ya wananchi. Tuweni macho

    Habarini wakuu, Tangu mjadala wa wapinzani wengine kudai tume huru ya uchaguzi na wengine katiba mpya kuingia katika taswira mpya baadhi yetu tumeingiwa na mashaka. Je, kwa nini wasimamie kitu kimoja? Je, wanaofanya hivyo ni kwa maslahi ya nchi au wananchi? Nimejipa muda wa kusikiliza pande...
  4. J

    Kama kwa Katiba iliyopo Rais ana kila kitu, hiyo Tume Huru ya Uchaguzi utaipataje? Bunge na Mahakama ziko huru?

    Ni mtu aliyevimbiwa tu anayeweza kuanza kudai Tume Huru ya Uchaguzi kabla ya Katiba Mpya. Katiba tuliyonayo hata irekebishwe vipi haitaweza kutoa mwanya wa kupata Tume Huru ya Uchaguzi kutokana na msingi wake. Liangalie bunge kisha iangalie mahakama ndio utaelewa. Tusisahau ilianza Katiba ya...
  5. B

    Hongera Maria Sarungi, mmeanza vyema kupata wajumbe wa Kamati ya Katiba lakini nadhani mmekosea fanyeni maboresho

    Awali nilipokuwa naangalia ujio wa SPACE kama njia ya kufanya bunge la wananchi sikuona Kwa upana ukubwa wa forum Hii. Nikiri Kwamba Maria Sarungi ni Moja ya mtu aliyenufaika kiubunifu na utawala wa awamu ya Tano. Alipofungiwa online TV yake hakukata tamaa alifanya research ni namna gani...
  6. sajo

    Uspika wa Bunge 2022: Sababu za Kisheria na Kikatiba Dkt. Tulia kukosa sifa za kugombea

    Mjadala umeibuka nchini baada ya Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Spika wa Bunge la JMT iliyoachwa wazi baada ya Ndugai kujiuzulu. Hoja bishaniwa imekuwa ni iwapo Dk. Tulia ana sifa au la za kugombea nafasi hiyo. Kwa mujibu wa Sheria ya Kinga, Haki na Madaraka...
  7. S

    Ni suala la muda tu kabla Ndugai hajakiri au kutamka hadharani kuwa Katiba ya nchi ni mbovu

    Bnafsi naamini kilichomfanya Ndugai ajiuzulu si mashambulizi(shinikizo) kutoka ndani na nje ya chama chake, bali ni baada ya kugundua Rais hana imani nae huku mhimili anaouongoza Rais ukiwa umejichimbia zaidi. Hivyo, bwana Ndugai akaona hana ubavu wa kupingana nae akaamu kujiuzulu. Kwahiyo...
  8. Sijali

    Kwa wale wasiojua umuhimu wa Katiba nzuri

    Bado nashikilia nadharia kuwa ni bora zaidi, hasa kwa nchi isiyo na uwezo mkubwa, kuvifanyia marekebisho vipee vibovu vya Katika (Constitutional ammendment) badala ya kuandika upya Katiba nzima. Nilitoa sababu tano za na hoja za kupendelea zaidi (Constitutional Ammendment). Leo nataka tu...
  9. F

    Mabadiliko ya Katiba natamani hili lingezingatiwa pia

    Wakati Katiba Mpya inaandikwa kama ningelikuwepo kwenye mazingira hayo, ningependekeza kuwepo na Mihimili minne katika Tz kwa jinsi mambo yanavyoenda tangu baada ya awamu ya kwanza ya uongozi wa nchi, yaani mitifuano ya kisiasa ambayo haina afya kwa ustawi wa taifa. Mhimili wa nne ungekuwa ni...
  10. Nyankurungu2020

    Chonde chonde wabunge wa CCM msichague Tulia Ackson kuwa Spika, tayari ameshaonesha udhaifu wa kutosimamia katiba ya JMT. Hafai kabisa kuwa spika

    Tunajua mpo wengi ndani ya mjengo wa National Assembly. Maana ni karibu ya 98 % ya wabunge wote. Japokuwa wengi mpo bungeni kimazabe mazabe baada ya uchaguzi mkuu wa 2020 kuwa na maluelue lakini hili la spika kuweni na Uzalendo. Bunge haliwezi kuwa na spika ambae ataona staha kuisimamia na...
  11. Idugunde

    Huu ni wakati wa Watanzania kudai katiba mpya, wasipodai taifa lao litaibiwa kama shamba la bibi.

    Katiba mpya itazuia mapungufu ya kila aina ambayo yanasabisha hili taifa kuibiwa na kuporwa kama shamba la bibi. Katiba mpya itawapa wananchi nguvu ya kuzuia, kurekekebisha na kukataa uovu wa kila namna ndani ya taifa lao. Mfano kukaataa na kupinga utawala unaokumbatia ufisadi kwa kuzuia au...
  12. farryandy

    Randama ya Rasimu ya Katiba Mpya: Hivi ndivyo inavyosema kuhusu Serikali tatu

    SURA YA SITA MUUNDO WA JAMHURI YA MUUNGANO Ibara ya 60 Muundo wa Muungano a. Maudhui ya Ibara Ibara ya Rasimu ya Katiba inaainisha muundo wa Muungano wa Shirikisho la Serikali tatu, ambazo ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Mapinduzi ya...
  13. Peter Madukwa

    Ndugai amefuata utaratibu wa kujiuzulu Uspika kwa mujibu wa Katiba. Mbatia hayupo sahihi na kesi yake haina mashiko

    Kumekuwa na mjadala kutoka baadhi ya watu mbalimbali mtandaoni juu ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Spika Mh Job Ndugai. Ulianza mjadala kwamba kwanini ktk barua yake ameandika herufi kubwa pekee? KIMSINGI kilichosambaa mtandaoni siyo barua bali ni TAARIFA KATIKA VYOMBO VYA HABARI ambayo ni sawasawa...
  14. Richard

    CCM imetudhihirishia kuwa ni chama Dola. Rais na Spika ni watu tofauti na Taaisisi ya Urais na Bunge ni vitu vingine

    Kitendo cha Spika wa Bunge la JMT kuandika barua yenye utata ya kujiuzulu na kisha kujitokeza hadharani kutamka kumwomba radhi raisi Samia Hassan, kina maana kubwa. Job Ndugai ametojitokeza ameomba radhi na kisha amejiuzulu na kuondoka. Huyu Spika si yule marehemu Adam Sapi Mkwawa na wala si...
  15. E

    Kayiba Mpya ni mwarobaini wa mihimili kuheshimiana bila kijali vyama

    Ndugu wanajukwaa nawasalimu kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Taifa la Tanzania kwa sasa tunahitaji katiba mpya. Uhitaji huu ni wa lazima kwasababu wote tumeshuhudia jinsi ambavyo mihili miwili haiko huru. Haiwezekani spika unazungumza kama muhimili halafu muhimili mwingine...
  16. K

    Mwanasheria: Barua ya Job Ndugai kujiuzulu Uspika ni batili kwa mujibu wa Katiba

    Leo nimesikiliza Mwanasheria mmoja kupitia UTV ameeleza kuwa kwa mujibu wa Katiba Spika akitaka kuachia madaraka anapaswa kulitaarifu Bunge na si Chama kama alivyofanya. Je Bunge litakuwa na uhalali wa kufanyia kazi barua yake kama asipoandika barua kwa Katibu wa bunge?
  17. C

    Katiba na Siasa za Tanzania - Tuwekane sawa

    Kiwango kilichofikiwa kinafikirisha. 1. Kufanya siasa kwenye ubora wa elimu ilikuwa mkakati wa muda mrefu uliobuniwa na utawala wa awamu ya pili ili kuwa na taifa la watu wasiojielewa kusudi waburuzwe, AU ilitokea coincidently tu kulingana na uelewa wa kiongozi wa nchi juu ya maana na umuhim wa...
  18. Nguruvi3

    Anguko la Ndugai: Somo la Katiba, viongozi na nchi

    Hatimaye Spika aliyeongoza kwa 'mkono wa chuma'' anguko lake limetimia. Mh. anaondoka akiacha historia ya Spika wa kwanza kujiuzulu tangu uhai wa Taifa hili Spika asingeweza kutekeleza majukumu yake kwa fyongo yake na dhalili aliyopata Fyongo si alichosema ni kile alichofanya baada ya kusema...
  19. I

    Kinachoiponza CCM ni katiba yao kuwa Rais wa nchi ndiyo mwenyekiti wao wa Taifa

    Kama CCM ingekuwa na Mwenyekiti wa Taifa tofauti na Rais wa nchi hali isingekuwa kama ilivyo sasa ya msuguano ndani ya chama. Ndugai kama Mkuu wa muhimili wa Bunge angekuwa na uhuru wa kumkosoa Rais na Rais angeweza kujibu hoja bila jazba. Aidha Rais angeweza kukosoa udhaifu wa Bunge na Spika...
  20. The Dictator

    Chalamila akanusha uvumi ulioenea asema sitaki katiba mpya wala marekebisho ya katiba

    Albert Chalamila amesema hataki katiba mpya wala marekebisho yake. Ameeleza hayo akikanusha habari zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kwamba anaunga mkono mabadiliko ya katiba. "Wala sihitaji hiyo katiba mpya, wala sihitaji hayo marekebisho,"- amesema Chalamila. Pia soma > Chalamila...
Back
Top Bottom