chadema

CHADEMA (Chama cha Demokrasia na Maendeleo)
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ni chama cha kiasiasa nchini Tanzania ambacho kilianzishwa tarehe 28 Mei 1992 na mwanasiasa mkongwe Edwin Mtei, aliyewahi kuwa Waziri wa Fedha katika miaka 1997 hadi 1979.

Mwaka 2000 CHADEMA hakikuwa na mgombea wa Urais. Mwaka 2005 mgombea wa CHADEMA Freeman Mbowe alikuwa namba tatu kati ya wagombea kumi akapata asilimia 5.88 za kura.

Mwaka 2010 CHADEMA ilipata asilimia 27.1% na mgombea Urais wa chama Wilbroad Peter Slaa na kura 4,627,923 kwa 31.75%.

Hata hivyo CHADEMA imekataa matokeo mengi kutokana na mchakato mzima kuwa mikononi mwa Tume ya Uchaguzi isiyo huru.
  1. JamiiForums Tanzania SI KWELI PreGE2025 Maria Sarungi amesema CHADEMA imepoteza mvuto wa kitaifa

  2. Z

    JamiiForums Tanzania Ushauri kwa vyombo vyetu vya Ulinzi na usalama viwe makini sana na hawa wahuni wa Chadema kwani wana nia ovu ya kuchafua amani na utulivu wa Nchi yetu

    Ushauri kwa vyombo vyetu vya ulinzi na usalama waendelee kuwafuatilia hadi chooni hawa wahuni, genge la kihalifu ambao wamejificha kwa mwamvuli wa kisiasa Chini ya Chama Cha Chadema. Genge hili kila kukicha lina panga na kuratibu mipango miovu ya kuchafua amani ya nchi, kufanya matukio ya...
  3. JamiiForums Tanzania CHADEMA: Tunasikitishwa na Jeshi La Polisi kuwakamata wanachama 10 bila ya kuwapatia haki ya kuonana na mawakili wao

    CHADEMA imelaani kitendo cha Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani kuwashikilia wanachama wake 10 waliokamatwa Kibaha bila dhamana na bila kupewa nafasi ya kuonana na ndugu zao. Chama kimesema kitendo hicho ni kinyume cha sheria na Katiba, kikitoa wito kwa Polisi kuwapatia wanachama hao haki za msingi...
  4. JamiiForums Tanzania Huyu James Mbowe anatakiwa ajue Mbowe alisajili vipaji vya siasa CHADEMA na sio kwamba aliwatengeneza yeye

    Huyu dogo James anakosea sana kusema kuwa Mbowe aliwasaidia kina Lissu, Lema, Msigwa kuwa wanasiasa wakubwa. Mbowe alichofanya ni kama Madrid inavyosajili mastaa wa soka toka timu mbalimbali. CHADEMA iliwahitaji kina Lissu na wenzake kuliko wao walivyoihitaji CHADEMA. Kwa mfano Lema hata...
  5. JamiiForums Tanzania GE2025 Mwenyekiti CHADEMA Arusha: Mbowe atoke hadharani na aseme 'No reforms No election'

    Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Arusha, Elisa Mungure, ametoa wito kwa Mwenyekiti Mstaafu wa chama hicho ngazi ya taifa, Freeman Mbowe, kujitokeza hadharani na kuunga mkono kaulimbiu ya chama ya “No Reforms, No Election”, kwa kuwa ndiye mwanzilishi wa msimamo...
  6. JamiiForums Tanzania GE2025 Mwenyekiti wa BAZECHA Mbeya: Kama kweli CCM imefanya kazi nzuri kwanini waogope kushindana na CHADEMA

    Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimetajwa kuiogopa CHADEMA kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutokana na mazingira ya kukibana chama hicho kikuu cha upinzani huku vyama vingine vya upinzani vikionekana kuimarika, kikiwemo ACT Wazalendo na CHAUMMA. Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Baraza la...
  7. JamiiForums Tanzania CHADEMA sio waumini wa demokrasia kweli, wakipata dola watatunyanyasa kwa udikteta

    Nimesema hivyo kwa sababu, CHADEMA pamoja na wanachama wao, hawaamini, hawakubali na wala hawaridhiki mtu mwingine kuwa na mawazo na maamuzi tofauti na wao. Wanalazimisha yule watakayemfanya adui, LAZIMA kila mtu amfanye adui. Ukiamua binafsi kwa maslahi na faida yako mwenyewe Ukamfanya rafiki...
  8. JamiiForums Tanzania GE2025 Huyu ndie Paul L Fulano. Kada wa CHADEMA ambaye kama hakuna wizi wa kura lazima awe mbunge wa Sengerema

    Huyu ndie Mwamba wa Chadema Sengerema.
  9. K

    JamiiForums Tanzania Umashuhuru wa Mama 2021-2022 uliletwa na Chadema kumbe!! angalieni sasa

    Ukweli unauma kumbe Mama ni kama punda aliyembeba yesu alifikiria ni yeye mashuhuri sasa ukweli unajulikana kwa kushuka sana kwa umashuhuri wake. Wakati ule maongezi ya Haki na demokrasia ndiyo yalimpa umashuhuri sasa yupo na wana mitandao wakina Kikwete na Rostam tunaona tofauti.
  10. K

    JamiiForums Tanzania Tatizo lijalo la CCM hawana vijana mahiri kama wa Chadema

    Hivi ukiangalia CCM chama kimajaa wazee wakina Kikwete, Samia. Vijana wengi hawana uwezo Chadema angalia viongozi wao ni vijana
  11. JamiiForums Tanzania John Mnyika aelezea hisia zake baada ya maamuzi ya Mahakama kuhusu mgawanyo wa mali

    Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imetupilia mbali maombi ya viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliotaka kuruhusiwa kuendelea na shughuli za kisiasa, baada ya zuio lililowekwa kutokana na kesi ya mgawanyo wa mali za chama hicho. Akizungumza baada ya uamuzi huo Agosti 18...
  12. JamiiForums Tanzania Ushauri :- CHADEMA , kwakuwa wanakubalika sana na Watanzania naomba wawekeze nguvu kubwa kufanya siasa za mitandaoni hiyo pekee inatosha sana

    Kwakuwa Kwa sasa Chadema inafanyiwa hujuma mbalimbali. Naomba wawekeze Katika majukwaa ya mitandaoni , Hizi Hujuma wanazofanyiwa Chadema zisiwe sababu za wao kurudi Nyuma. Tone Tone iendelee kama kawaida iwe online na hela inayokusanywa iwe inatolewa taarifa ili kuanagalia Speed na kuboresha...
  13. JamiiForums Tanzania CHADEMA: Jeshi la Polisi Pwani limetoa taarifa ya uongo kuhusu kukamatwa kwa wanachama wetu Kibaha

  14. JamiiForums Tanzania Kesi ya mgawanyo wa mali uongozi wa CDM wakwaa kisiki tena

    Ombi la uongozi wa Chadema kutaka kuendelea kutumia mali za chama zenye mgogoro limegonga mwamba na kutupiliwa mbali.
  15. JamiiForums Tanzania Nashauri: CHADEMA, wafuasi wa Lissu, Ndugu, Rafiki na jamaa Wasiende Mahakama kuanzia siku ya Leo

    Hamjambo! Sijui nini kinaendelea, na sitaki kujua. Kumaanisha siwezi kueleza na sitaki kuelezewa kuhusu kile kiitwacho Kesi ya Lisu. Ila nitashauri mambo madogo ambayo yanamashiko tunapoenda katika ukingo wa zoezi hili; 1. Kuanzia leo, Wale wanaojiona wana ukaribu na Lisu, wanachama wenzake...
  16. JamiiForums Tanzania Orodha ya Maadui wa CDM

    Mbowe KIGAILA MWALIMU CHAUMMA ZITTO SPIKA JAJI MKUU MAHAKAMA YANGA ENG HERSI ALI KAMWE Kwa ufupi kila mtu ni mbaya kwao.hii ni dalili ya kuchanganyikiwa kitaalamu inaitwa paranoia yaani ukichaa unaoogopa hadi ndugu au mwenza wako. Ongeza orodha
  17. S

    JamiiForums Tanzania Nalaani vikali eneo takatifu la Mahakama kugeuzwa na Chadema kuwa ulingo wa siasa, dini na vurugu

    Kila inapofika kesi ya Lissu au ya Chadema lazima kutokee tafrani ya wafugaji na Polisi, huu ni mchezo wa kifala sana unaochezwa na Kitengo cha propaganda cha chama hicho ili watanzania tuamini kuwa chama hicho kinaonewa na kinapambania haki, kamanda Muliro usikubali uhuni wa namna hiyo, upande...
  18. JamiiForums Tanzania CHADEMA Mmeishiwa mbinu? Serikali haina dini na haitaongozwa kwa misingi ya dini

    Naona aibu sana kuona chama ambacho kilikuwa kwenye ubora wa kipekee miaka kadhaa nyuma sasa kimeporomoka na kufanya vitu visivyoeleweka. Serikali haina dini japo watu wake ni waamini wa dini mbalimbali.
  19. M

    JamiiForums Tanzania CHADEMA wanahitaji kuwa na Malcom X na Steven Biko wao ili kusaidia siasa za ki Mandela na ki Martin Luther

    Siasa za CHADEMA kwa miaka ya karibuni zimekuwa siasa za ki Mandela Mandela na Ki Martin Luther King(Ukipigwa shavu la kulia geuza na la kushoto). Hakuna Steven Biko na Malcom X tena (Jino kwa Jino) huko katikati ndio maana uonevu unazidi kila siku. Miaka ya nyuma akina Lema walijitahidi kuwa...
  20. JamiiForums Tanzania GE2025 CHADEMA imeaminisha watu kuwa Act-Wazalendo ni CCM 'B'

    Akizungumza na kituo cha redio cha East Afrika leo Agosti 18, 2025, Isihaka Mchinjita, Makamu Mwenyekiti wa ACT-Wazalendo Bara, amesema kuwa CHADEMA imefanya kazi kubwa sana katika kujaribu kuuaminisha umma kuwa ACT ni CCM ‘B’ jambo analosema si la kweli bali ni propaganda ya kisiasa. Chanzo...
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…