PENZI LA MWANA WA BOSI
1
Nipomaliza la saba, litorokea mjini,
Mguuni nina raba, na kibegi mgongoni,
Nauli ninayo haba, nimeweka mfukoni,
Penzi la mwana wa bosi, menitia matatani.
2
Gari zuri tukapanda, kuelekea mjini,
Shauku ilinipanda, kuondoka kijijini,
Nauli nikailinda, nisiibiwe mjini...