Neno mtemi asili yake ni kiongozi wa ufyekaji.
Zamani kwenye jamii ya Wasukuma na Wanyamwezi, vijana wakifika umri wa kujitegemea walikuwa wanachagua kiongozi na kwenda porini kufyeka eneo la kuanzisha makazi.
Kiongozi aliyekuwa anaratibu shughuli hiyo alikuwa anaitwa Mtemi.