bendaki
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 952
- 346
Itapelekea mtu mwenye uelewa mkubwa kukubaliana na porojo hizo hapo juu:
2. Mageuzi utokana na kujitathmini:
Katika tahmini ninayo iona hapa ni kuwa chama kilijaa Mafisadi na wala Rushwa ndicho kigingi kikubwa cha
maendeleo ya Watanzania. Ufisadi na rushwa ni mizizi ya tatizo au ni matawi ya tatizo kwa matatizo ya Watanzania?
Vipi uwezo mdogo wa chama na ubnafsi wa wenye chama?
a) UWEZO: Chama kilipewa nchi kwa zaidi ya miaka 50 sasa, mfano unavyo mpatia mtu kandarasi ya kukujengea nyumba yako, ukiamini kuwa ni fundi stadi kwa anavyo jinasibu ndani ya zabuni nk. Baada ya nyumba kukamilika unagundua imejengwa ikiwa ina kasoro kibao, sakafu inakatika, rangi haing'ai, mabomba yanavuja, umeme ni shoti kila siku, nk nk. Unafuatilia unakuta kuwa japo kandarasi alikuwa simati, kwa maneno kumbe simati yake ilikuwa feki, mafundi aliokuwa akiwatumia wengi hawakujifunzia kazi walizokuwa wakizifanya. Kuna wafanya kazi hewa kibao katika orodha yake ya wafanya kazi usimamizi hajui.
CCM ilikuwa kila baada ya miaka mitano inapewa dola la tanzania. Inaajili watu wakuiwezesha kufikia Ilani zake ilizo zinadi. Baada ya miaka 50 nchi inaonekana haisogei mahali pamoja na raslimali nyimgi ilizo nazo inafahamika kuwa imekuwa ikitumia maelufu ya wafanyakazi hewa. imekuwa na wengi wa watumishi ilio kuwa ikiwatumia wakiwa na elimu feki. (Imedhihirishwa na ccm wenyewe kupitia kwa Mwenyekiti wao)
CCM inadhihirisha kuwa tatizo lake kubwa ni uwezo, capacity, capacity ya kufanya vitu kitaasisi, kidola kwa skills za utawala zilizo tukuka. CCm haikuwa nazo na bado hainyeshi kuwa inakwenda kuwa nazo.
Ingekuwa nazo bunge leo hii lingekuwa limeisha toka kwenye ndioooooo, ndiooooo na kujikita katika constructive mission ya kujenga hoja kuiongoza serikali nk nk na kufanya hivyo kunatakiwa uwepowa collective vision. Iko hivyo????
Kufuta sheria zote zilizowekwa kihewa na kivyeti feki pia kuwepo kwa katiba safi.
b) UBINAFSI:
CCM imejiianisha kuondoa tofauti kati ya CCM "Wenyewe na CCM "Vibao"?
Wenyewe ni wale katika mfumo mfu walijilimbikizia mali na mali (Majumba, Magari, Mahoteli, Ardhi, nk). Wengine walichota pesa wakanunua au walichukua vilivyokuwa ni mali ya serikali. Hata chama kilifanya hivyo, mfano viwanja vya michezo. Anzia Ikulu, Upanga, Osterbay, Msasani, mikoceni, na kila pazuri DAR na kwingineko ukifika hutaamini wanaishi kama Watanzania wa watoto wa wakulima maskini ambao ndio "CCM VIBAO".
Je katika mageuzi kuna mpango wa kuvirudisha hivyo walivyojilimbizia wenyewe kwa vibao (80% ya watanzania)?
Au kuwa walioisha vipata waishi kama mbinguni na wanaotafuta maisha sasa katikati ya mageuzi waishi kama mashetani?
kama sivyo, rationally ya Watu wote ni sawa, kila mtu anastahili heshima, kila mtu atapata urithi sawa nk nk viko wapi?
TUTAFAKARI>
- Hizo projo hazitabainishii ni katika forum ipi hicho chama kimeamua kufanya mageuzi. Mfano watu wachache au mtu mmoja alipowazia kuleta wazo la "Ujamaa na Kujitegemea" wakati chama kilikuwa TANU, kuliitishwa kongamano la Halmashauri Kuu ya chama. Halmashauri hiyo ilikaa Arusha na ikatoka na maazimio baada ya mjadala mrefu. Likazailiwa likiwa Azimio la Arusha. yapo mageuzi mengi yaliyoisha anzishwa na aidha TANU au CCM kwa nyakai mbali mbali kama, Uhuru ni Kazi, Siasa ni Kilimo, Azimio la Arusha, Kilimo Kwanza nk nk. Sasa haya mageuzi unayoyazungumzia ni Mageuzi ya chama au ni Mageuzi ya mtu?
2. Mageuzi utokana na kujitathmini:
Katika tahmini ninayo iona hapa ni kuwa chama kilijaa Mafisadi na wala Rushwa ndicho kigingi kikubwa cha
maendeleo ya Watanzania. Ufisadi na rushwa ni mizizi ya tatizo au ni matawi ya tatizo kwa matatizo ya Watanzania?
Vipi uwezo mdogo wa chama na ubnafsi wa wenye chama?
a) UWEZO: Chama kilipewa nchi kwa zaidi ya miaka 50 sasa, mfano unavyo mpatia mtu kandarasi ya kukujengea nyumba yako, ukiamini kuwa ni fundi stadi kwa anavyo jinasibu ndani ya zabuni nk. Baada ya nyumba kukamilika unagundua imejengwa ikiwa ina kasoro kibao, sakafu inakatika, rangi haing'ai, mabomba yanavuja, umeme ni shoti kila siku, nk nk. Unafuatilia unakuta kuwa japo kandarasi alikuwa simati, kwa maneno kumbe simati yake ilikuwa feki, mafundi aliokuwa akiwatumia wengi hawakujifunzia kazi walizokuwa wakizifanya. Kuna wafanya kazi hewa kibao katika orodha yake ya wafanya kazi usimamizi hajui.
CCM ilikuwa kila baada ya miaka mitano inapewa dola la tanzania. Inaajili watu wakuiwezesha kufikia Ilani zake ilizo zinadi. Baada ya miaka 50 nchi inaonekana haisogei mahali pamoja na raslimali nyimgi ilizo nazo inafahamika kuwa imekuwa ikitumia maelufu ya wafanyakazi hewa. imekuwa na wengi wa watumishi ilio kuwa ikiwatumia wakiwa na elimu feki. (Imedhihirishwa na ccm wenyewe kupitia kwa Mwenyekiti wao)
CCM inadhihirisha kuwa tatizo lake kubwa ni uwezo, capacity, capacity ya kufanya vitu kitaasisi, kidola kwa skills za utawala zilizo tukuka. CCm haikuwa nazo na bado hainyeshi kuwa inakwenda kuwa nazo.
Ingekuwa nazo bunge leo hii lingekuwa limeisha toka kwenye ndioooooo, ndiooooo na kujikita katika constructive mission ya kujenga hoja kuiongoza serikali nk nk na kufanya hivyo kunatakiwa uwepowa collective vision. Iko hivyo????
Kufuta sheria zote zilizowekwa kihewa na kivyeti feki pia kuwepo kwa katiba safi.
b) UBINAFSI:
CCM imejiianisha kuondoa tofauti kati ya CCM "Wenyewe na CCM "Vibao"?
Wenyewe ni wale katika mfumo mfu walijilimbikizia mali na mali (Majumba, Magari, Mahoteli, Ardhi, nk). Wengine walichota pesa wakanunua au walichukua vilivyokuwa ni mali ya serikali. Hata chama kilifanya hivyo, mfano viwanja vya michezo. Anzia Ikulu, Upanga, Osterbay, Msasani, mikoceni, na kila pazuri DAR na kwingineko ukifika hutaamini wanaishi kama Watanzania wa watoto wa wakulima maskini ambao ndio "CCM VIBAO".
Je katika mageuzi kuna mpango wa kuvirudisha hivyo walivyojilimbizia wenyewe kwa vibao (80% ya watanzania)?
Au kuwa walioisha vipata waishi kama mbinguni na wanaotafuta maisha sasa katikati ya mageuzi waishi kama mashetani?
kama sivyo, rationally ya Watu wote ni sawa, kila mtu anastahili heshima, kila mtu atapata urithi sawa nk nk viko wapi?
TUTAFAKARI>