Wewe unabahati umepoteza mil 5, miaka kama mitano au sita nilipoteza $25,000/- kwa mambo hayo ya online business za Forex, ndipo nikaamini hakuna short cut kwenye mafanikio, kila kitu kina mchakato wake.
Msitu unaweza kuteketea kwa cheche chache za moto kwenye nyasi kavu, hapa naona kuna dalili za kuteketeza nchi yetu pendwa kwa hizi ajenda za kibaguzi za wale waislamu na hawa wakristo, wale Wazanzibari na hawa Watanganyika, tuombe hili jambo lisipewe nafasi katika fikra zetu kwani majuto yake...
Ajenda za kufukuza watu kwenye nchi zao Trump ndiye champion wao halafu ikafuatiwa na South Afrika, hizi ajenda zipo za kuwapoteza watu kutoka kwenye mambo yao ya msingi, ulimwengu wa sasa watu wanatakiwa wawe kitu kimoja siyo kufukuzana.
Njia aliyoichagua Lissu katika siasa za upinzani ni ngumu na nzito na zina gharama kubwa katika uhai wake, afya yake, uchumi wake na maisha yake na familia yake kwa ujumla hasa kwa nchi zetu za kiafrika. Na nina uhakika yeye mwenyewe analijua hilo.
Maendeleo ya kiuchumi hayana dini, kutoboa kimaisha ni mchakato, sisi watu tunaopenda starehe kuliko kazi vipi tutatoboa? Ndiyo maana wasanii wanatengeneza mkwanja mrefu kuliko hata walimu, wanasiasa wanatengeneza sheria za kujinufaisha zaidi wao kuliko watu wao waliyowachagua. Tunapenda njia za...
Katika mjadala wa masuala ya umma, hususan yale yanayohusu migogoro ya kisiasa na kijamii, ni muhimu kutenganisha hisia binafsi na taarifa rasmi zilizothibitishwa kupitia taratibu za kisheria na kiuchunguzi. Kauli zilizotolewa na Paskali zinapaswa kutazamwa katika muktadha huo.
Maudhui...
Kuna wakati magari yaliyotoka Japan miaka hiyo yalikamatwa na kurundikwa uwanja wa taifa, sijui yaliagizwa kinyume na taratibu, baadaye yakaachiliwa.
Enzi za Nyerere mambo yalikuwa moto.
Huo ni mtazamo wako, lakini sisi wengine tunaona dini ndizo zimeweza kuleta maarifa zaidi ya sisi wanadamu kujuana, kuheshimiana na kupendana, misingi ya utengamano kwa sisi wanadamu tunaipata kwenye mafundisho ya dini, lakini kuna watu si wa dini wanatumia dini kama njia ya kujinufaisha wenyewe...
Ikiwa kucheza fainali wamepata viwanja basi wakishinda watajengewa na nyumba kabisa na huenda wakapata na hata na usafiri ila umri wa kundesha utakuwa bado.
Zamani ndoa ilikuwa ni jambo la kifamili, yaani linajumuisha familia zote za muoaji na muolewaji. Ni mchakato wenye kuunganisha familia nne (1-familia ya baba wa mume, 2-familia ya mama wa mume, 3- familia ya baba wa mmke na 4-familia ya mama wa mke), na vijana walikuwa wakifundwa kama mambo ya...
Hapo kwanza tuna advantage ya mashabiki, kwa kuwa wamoroko walizinguana na wasenegali kwenye fainali ya AFCON (ya wakubwa) hivyo hapo kuna ile kauli ya kuwa "adui wa adui yangu ni rafiki yangu", na vijana itabidi wajitoe kwa asilimia zote kwani hawana cha kupoteza ila hapo ndipo wanajitengenezea...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.