Uchaguzi wanukia
Haya, haya nyie wenye njaa,
Uchaguzi unanukia,
Kaa mkao wa kufaa,
Wamwagaji waingia!
Matajiri wenye njaa,
Kofia mbili kuvaa,
Wasioishiwa tamaa,
Hadi mauti kuingia!
Wanakuja kuzinunua,
Shahada mtazopewa,
Hesabu wajipangia,
Kila mtu kumnunua.
Haya, haya wenye...