mshairi.mtangan
New Member
- Nov 12, 2008
- 1
- 0
Zichungeni shilingi,bajeti inazotoa,
Matapeli wako wengi, wanazifuatilia,
Msibumbwawe kwa wingi,tumboni zitaishia,
Na kitakachobakia, uchaguzi wanukia!
Twabeba nizigo mingi, hakuna wa kutuhurumia,
Anzia na mashangingi,mitaani yakizagaa,
Hayaingizi shilingi, bali zinaangamia,
Na kitakachobakia, uchaguzi wanukia!
Chungeni kila shilingi, sasa itakayoingia,
Na wekeni na vigingi, kila watakayoitoa,
Udhbiti ni msingi, fedha vema kutumia,
Na kitakachobakia, uchaguzi wanukia!
Kwa sasa walaji wengi,waletaji wapungua,
Mezani msongemangi, wanajua kutumia,
Bongo zao hazigongi, vipi nasi tutajaa,
Na kinachobakia, uchaguzi wanukia !
mshairi
Matapeli wako wengi, wanazifuatilia,
Msibumbwawe kwa wingi,tumboni zitaishia,
Na kitakachobakia, uchaguzi wanukia!
Twabeba nizigo mingi, hakuna wa kutuhurumia,
Anzia na mashangingi,mitaani yakizagaa,
Hayaingizi shilingi, bali zinaangamia,
Na kitakachobakia, uchaguzi wanukia!
Chungeni kila shilingi, sasa itakayoingia,
Na wekeni na vigingi, kila watakayoitoa,
Udhbiti ni msingi, fedha vema kutumia,
Na kitakachobakia, uchaguzi wanukia!
Kwa sasa walaji wengi,waletaji wapungua,
Mezani msongemangi, wanajua kutumia,
Bongo zao hazigongi, vipi nasi tutajaa,
Na kinachobakia, uchaguzi wanukia !
mshairi