Ulaya na Marekani rasmi sasa hoi bin taabani WATANZANIA TUANZE KUJIANDAA KUFUNGA MIKANDA KWA MIEZI ISHIRINI NA NNE na pengine zaidi na kama tusipokuwa watundu na wabunifu na kuachana na mazoea basi mamb o yanaweza yakawa magumu zaidi. Mkakati mmoja ni kuacha kukumbatia nchi za Magharibi na k uanza kuzikumbatia nchi za BRICs.
KATIKA miezi hii iliyobakia kufikia Juni 2009 Watanzania tunatakiwa kurudia somo la Ujamaa na Kujitegemea kwa makini sana.
Maana imetangazwa rasmi kwamba nchi za Ulaya Magharibi na awali Marekani yenyewe zimeingia katika hali ya uchumi inayoitwa 'depression' au 'recession' au 'deflation'
ambayo ni hali inayoendana na watu, makampuni na nchi kukosa fedha za kutosha kuwekeza na kuzalisha kwa kiwango cha juu zaidi kuliko ongezeko la watu, kupanda gharama za maisha na vitu kama hivyo.
Hii ina maana kwamba nchi kama Uingereza zitapunguza matumizi yake mbalimbali katika nchi ambazo wanaona wanatumia zaidi kuliko ya kile wanachopata, mathalani, Tanganyika na Zanzibar na kuzijali zaidi nchi wanazopata kuliko wanavyotumia kama vile Kenya na Rwanda.
Kwa mantiki hii, utegemezi wa Tanzania kwa Uingereza na Marekani kutokana na maono na mtazamo dhaifu wa uongozi wetu umetufanya tule chuya.
Hivi sasa, ili tusipate hasara zaidi, inatakiwa pia tushirikiane kwa kila namna na nchi nyingine kama vile zile za China, Russia, Uarabuni, Marekani Kusini na kadhalika ili kutoweka mayai yetu yote kwenye kiota kimoja. Yanaweza yasianguliwe yote na yakaishia kuwa viza na kuyatupa.
Kwa mtazamo wangu binafsi ninadhani huu ni wakati muhimu wa kujenga mkakati na mbinu za kushirikiana kikweli kweli na Uchina ili waweze:
. kututengenezea matrekata ya bei nafuu,
. mitambo mbalimbali inayotumia nishati tofauti na mafuta na umeme na hasa ile inayotumia gesi, upepo na nishati ya jua,
. kuunda vifaa mbalimbali vya mahospitali, mashule na maofisi kwa gharama nafuu,
. kutengeneza vyombo mbalimbali vya usafiri wa anga, majini na nchi kavu vinavyotumia nishati mbadala badala ya peteroli na dizeli,
. kutuundia mitambo ya kupampu na kusambaza kwa maji inayotumia upepo, nguvu za maji au gesi,
. na vitu vingine mbalimbali ambavyo itawezekana kwa kuwa mashine zilizokuwa zikinguruma kutengeneza vitu vya kuuza Ulaya na Marekani sasa imenyamaza na inataka shughuli mpya kufufuliwa.
Hebu tuliangalie hili kwa makini maana kwangu huu ni mwanzo wa nchi kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kutumia rasilimali mali asili na rasilimali watu na ushirikiano na nchi za BRICs, yaani, Brazili, India, China na kama hizo kupunguza gepu kubwa kati ya nchi tajiri na sisi.
KATIKA miezi hii iliyobakia kufikia Juni 2009 Watanzania tunatakiwa kurudia somo la Ujamaa na Kujitegemea kwa makini sana.
Maana imetangazwa rasmi kwamba nchi za Ulaya Magharibi na awali Marekani yenyewe zimeingia katika hali ya uchumi inayoitwa 'depression' au 'recession' au 'deflation'
ambayo ni hali inayoendana na watu, makampuni na nchi kukosa fedha za kutosha kuwekeza na kuzalisha kwa kiwango cha juu zaidi kuliko ongezeko la watu, kupanda gharama za maisha na vitu kama hivyo.
Hii ina maana kwamba nchi kama Uingereza zitapunguza matumizi yake mbalimbali katika nchi ambazo wanaona wanatumia zaidi kuliko ya kile wanachopata, mathalani, Tanganyika na Zanzibar na kuzijali zaidi nchi wanazopata kuliko wanavyotumia kama vile Kenya na Rwanda.
Kwa mantiki hii, utegemezi wa Tanzania kwa Uingereza na Marekani kutokana na maono na mtazamo dhaifu wa uongozi wetu umetufanya tule chuya.
Hivi sasa, ili tusipate hasara zaidi, inatakiwa pia tushirikiane kwa kila namna na nchi nyingine kama vile zile za China, Russia, Uarabuni, Marekani Kusini na kadhalika ili kutoweka mayai yetu yote kwenye kiota kimoja. Yanaweza yasianguliwe yote na yakaishia kuwa viza na kuyatupa.
Kwa mtazamo wangu binafsi ninadhani huu ni wakati muhimu wa kujenga mkakati na mbinu za kushirikiana kikweli kweli na Uchina ili waweze:
. kututengenezea matrekata ya bei nafuu,
. mitambo mbalimbali inayotumia nishati tofauti na mafuta na umeme na hasa ile inayotumia gesi, upepo na nishati ya jua,
. kuunda vifaa mbalimbali vya mahospitali, mashule na maofisi kwa gharama nafuu,
. kutengeneza vyombo mbalimbali vya usafiri wa anga, majini na nchi kavu vinavyotumia nishati mbadala badala ya peteroli na dizeli,
. kutuundia mitambo ya kupampu na kusambaza kwa maji inayotumia upepo, nguvu za maji au gesi,
. na vitu vingine mbalimbali ambavyo itawezekana kwa kuwa mashine zilizokuwa zikinguruma kutengeneza vitu vya kuuza Ulaya na Marekani sasa imenyamaza na inataka shughuli mpya kufufuliwa.
Hebu tuliangalie hili kwa makini maana kwangu huu ni mwanzo wa nchi kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kutumia rasilimali mali asili na rasilimali watu na ushirikiano na nchi za BRICs, yaani, Brazili, India, China na kama hizo kupunguza gepu kubwa kati ya nchi tajiri na sisi.