Katika hali ya kawaida haiwezekani asilimia 60% ya watahiniwa wa form 4 wakafeli mtihani. Sote tunajua kwamba wanafunzi hawakufundishwa vizuri kwa sababu mbalimbali lakini kubwa ni mgomo wa kitaifa wa walimu mnamo mwezi wa saba japokuwa pilkapilka zake zilianza mapema kimya kimya bila...
Wakati CDM wanatoa kauli yao Bungeni kuhusu mradi wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi, msimamo wa wananchi wa mtwara kuhusu mradi huo ulikuwa bado kutangazwa. Hivyo kama CDM wangetamka bungeni kwa wakati huo kwamba wananchi wa mtwara hawaungi mkono mradi huo, huo ungekuwa uzushi na uchochezi...
Huyu mtu alimkashifu sana Kamanda wetu mpendwa LISSU, Bungeni wakati wa mjadala wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba wakati CDM walipotoka nje ya Bunge kwamba ni LISSU ni Mwanasheria Bandia na kwamba asikanyage Zanzibar. Jamani, mmeshasahau?
Tanzania ni nchi ya kusikitikia sana. Ni nchi yenye,
- Rais asiye Rais. Hajui yanayotendeka nchini mwake.
- Waziri mkuu asiye waziri mkuu. Hana mamlaka ya kuwasimamia mawaziri,
- CAG asiye CAG. Taarifa zake hazina maana kwa Kikwete,
- Pia tuna MAKAMU WA RAIS asiye MAKAMU WA RAIS. Kazi yake ni...
Ule usemi kwamba kelele za chura hazimzuii tembo kunywa maji umetimia leo hii bungeni. Pamoja na hoja kali za wabunge na watanzania wote kwa ujumla kuhusu ubadhirifu wa mawaziri, leo hii wakati wa kuahirisha bunge Pinda hakueleza lolote kuhusu msimamo wa serikali kuhusu hoja hizo.
Kwa maana...
Hivi Mkapa hakuulizwa kwamba ni muwekezaji gani aliyeuziwa Kiwira? Kwamba je, Kiwira ilikuwa na thamani ya kiasi gani wakati inauzwa, na huyo muwekezaji aliinunua kwa bei gani, na aliiendeleza vipi? Hapo ndipo tungefahamu kama kweli na yeye Mkapa ni fisadi au la.
Kama Kikwete anaona kwamba kilio cha wabunge kwamba kuna ufisadi mkubwa sana Serikalini ni upepo wa kupita maana yake ni kwamba hata taarifa ya CAG ni upepo wa kupita. Yaani taarifa hiyo ni uzushi tu, kwamba watu wanawaonea wivu mawaziri wake pamoja na wakurugenzi wake Wilayani. Yaani ule usemi...
Kama Kikwete anaonana kwamba kilio cha wabunge kwamba kuna ufisadi mkubwa sana Serikalini ni upepo wa kupita maana yake ni kwamba hata taarifa ya CAG ni upepo wa kupita. Yaani taarifa hiyo ni uzushi tu, kwamba watu wanawaonea wivu mawaziri wake pamoja na wakurugenzi wake Wilayani. Yaani ule...
Utaratibu wa kisheria ni kwamba kwa vile Lema ameappeal, anatakiwa kuweka injunction ya kutosimamishwa ubunge mpaka hapo appeal yake itakaposikilizwa na kuamuliwa upya na Court of Appeal. Hivyo Lema anatakiwa kuwa Bungeni haraka asiendelee kupoteza muda.
Nina imani kubwa sana na mzee Warioba. Uzalendo wake kwa nchi hii unajulikana. Nina imani kubwa sana pia na wajumbe wote watume hii kwa upande wa Tz bara. Kwa upande wa Zanzibar bahati mbaya wengi wao siwafahamu vizuri, ukiondoa Dr. Ahmed Salim. Kwa tume hii kweli Katiba nzuri inaweza...
Tamko la Mukama ni msimamo wa CCM. Hivyo CCM imeshaamua, ila Nape siku hiyo hakuwepo. Tena amesahau kumalizia kwamba sambamba na uamuzi huo wa safari hii ni zamu ya mwanamke. Hivyo wanaume waache kujisumbua kwa sababu majina yao hayatarudishwa. Nasikia mama Rwakatale ameanza kujiandaa.
Kumnyanganya Genereta ni sawa kabisa ili aone adha yas kukosa umeme. Unaelewa ni kwa nini Pilot wa ndege za kiraia haruhusiwi kuwa na mwavuli ya kuokoa maisha (Parachute?). Ili atambue kwamba asipokuwa makini yeye pamoja na abiria wake wote kwa pamoja wataangamia.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.