CHADEMA na Mnyika waongo katika suala la Gesi

CHADEMA na Mnyika waongo katika suala la Gesi

Mleta mada labda ungeweka na hiyo kauli yao (cdm) rasmi kuhusu mtwara gas, ili tuweze kudadavua vizuri uongo, ugeugeu na udandaaji hoja wao. Vinginevyo kwa quote hiyo ya hansard huwezi kuwabana hata chembe.

Soma hotuba ya Mnyika hapa http://mnyika.blogspot.com/2012/07/hotuba-ya-kambi-rasmi-ya-upinzani.html

Tamko la chadema utalipata kwenye blog hiyo hiyo ya Mnyika na website ya Chadema.....total contradiction. Wanathibitisha wasivyo chama makini. Bora CUF wamekuwa na msimamo consistent toka mwanzo na sio kufuata upepo
 
Ubongo wa mleta post hii ungekuwa na ukubwa wa peanut size ungetosha kumpa akili ya kujua hoja katika bomba la gesi ni nini!Wana Mtwara is kwamb hawatak bomba lijengwe bali wahakikishiwe wanafaidikaje na hasa kwa ujenzi wa mtambo wa kutengeneza gesi hapo hapo Mtwara.Pia kuimarishwa kwa bandari yao.Halafu bomba ndipo lijengwe.Wasikilize vizuri watu wa Mtwara usitafute ubaya wa CDM dada.

Wewe nawe ni great thinker? Naona badala ya kujibu hoja, unatoa matusi. Kuhusu watu wa Mtwara una uhakika na unachosema......hakuna kitu kama watu wa mtwara.......HAPA NI wajanja wachache wenye maslahi yao binafsi wanawatumia wenzao kucheza ngoma wasioijua in the pretext ya kudai bomba halijengwi, sababu hawanufaiki. Watu wa Mtwara halisi wanaotumia akili zao na sio kufuata upepo,...wanachotaka kujua ni serikali inawaandaaje vijana wetu wa Mtwara kuweza kushiriki katika uchumi wa gesi utakaokuja muda si mrefu. Maana hatari hapa ni kwamba hata viwanda na mitambo ya kuzalisha umeme ikijengwa Mtwara, kama watu wake hawajaandaliwa kielimu na ujuzi, kazi hizo zitafanywa na watu kutoka nje ya Mtwara.

As a matter of fact, baadhi ya watu wa Mtwara hao hao, wameshaanza kuuza ardhi yao kwa kasi kubwa kwa watu wanaotoka mikoa mingine hususan dar es salaam.....wakidhania wanafaidika......matokeo yake......neema ya gesi itawakuta wakazi wapya waliouziwa ardhi na wanamtwara kwa hiari. Laiti maandamano yanayoendelea yangekuwa na agenda ya dhati ya kupigania haki ya wanamtwara, issues zingekuwa hizo....capacity building ya wanamtwara, ardhi yao isichukuliwe kama njugu etc....lakini hapa ajenda ni nyingine kabisaa.....SABABU KUNA WANAONUFAIKA NA VURUGU HIZI, ndani yake wamo wanasiasa, wafanyabiashara, makuwadi, mashirika ya kijasusi n.k..... Tunacheza ngoma tusiyoijua, tutakuja kujuta huko mbeleni. Ni aibu kuona cha makini kama Chadema wanakwenda na upepo pasipo kufanya tathminii ya kina ya yanayoendelea. Akina Mnyika, Zitto, Mrema , Prof Bregu wekeni vichwa chini muone bigger picture....msiwe simplistic kwenye masuala ya msingi ya kitaifa kama haya.
Mnyika ulikosea kudandia hoja ya nauri ya feli....tuka ignore...lakini hii ya gesi.....unachemsha.

Hivi wajua wanaotsfuta gesi hivi sasa, wanataka kujenga mtambo wa kuchakata gesi ( LNG Plant) baharini? Serikali haitaki. Kwanini? Kwasababu wakijenga baharini itakuwa vigumu kudhibiti na kuhakiki kiasi cha gesi wanachochukua na kusafirisha nje ya nchi. Serikali inataka kinu hicho kijengwe Mtwara, ili pamoja na kuwezesha ufuatiliaji mzuri na wa karibu, pia kitoe ajira kwa watanzania. Lakini sasa kwa vurugu zinazoendelea hivi sasa Mtwara, wawekezaji hao mmeaongezea nguvu ya hoja ya kutojenga kinu hicho Mtwara na badala yake watadai kijengwe baharini maana Mtwara hakuna usalama......maandamano na vurugu kibao! Who is the looser there? N pi Watanzania wote hasa wanamtwara

Tusikubali ku compromise national interest kwa vijsenti vichache vinavyotolewa na hao wenye maslahi yao ya kuvuruga nchi yetu kwa tamaa zao.
 
Hata kama msimamo wao kabla ilikuwa ni kuwa bomba lijengwe toka mtwara kuja dar,kwa hali ilivyo sasa ni mwendawazimu tu (serikali ya magamba) asingebadili msimamo kuhusu suala hili. Kama watu wamekataa lazma uwasikilize

Wamekataa watu gani? Wale innocent people waliorubuniwa na visenti wakaandamane? Hivi nikuulize Mtwara ina wananchi wangapi? Walioandamana ni wangapi?

Chama kilicho tayari kushika dola hakibadili msimamo kiholela tu simply because watu wamekataa...... Kwa style hiyo, mkishika Serikali, lazima nchi itayumba tu. wakiandamana watu leo hawataki kulima kahawa, unabadili msimamo! Chadema isnt ready to rule this country kwa style hii ya ukigeugeu
 
Hapo kwenye 'kuweka wazi mkataba husika' ndo maneno iko. Wanamtwara wanataka kujua hatima yao. Watanufaikaje? Sio bomba linaenda dar na mwisho wanajengewa madarasa matatu yasiyo na walimu, ama wodi moja isiyo na vitanda!

Umenena sawa sawa. i wish hoja ingekuwa ndio hii, kuna mantiki ndani yake. Lakini hoja ya halijengwi bomba tu.......haina mashiko.....sana sana ni kucheza ngoma ya SoNGAS na Panafrican Energy waajiri wa Zitto Kabwe ambao hawalitaki bomba kwasababu ya msingi....itawa run out of business
 
Mkataba wa mkopo wa ujenzi wa bomba haukuwekwa wazi kama ilivyotakiwa na kambi ya upinzani Bungeni, hivyo ni dhahiri kuna mchezo mchafu sana, mkopo ni mkubwa sana kulinganisha na gharama halisi, hivyo basi, ukijumlisha na riba, faida yote ya Gesi hiyo itaishia kulipa deni, ni sahihi kuwaunga mkono wananchi wa Mtwara wasifanywe kama wa Kahama na dhahabu yao. Sidhani kama CDM wanadandia hoja kwani wao ndio walioianzisha hoja hii ya 'kudai manufaa' kutokana na gesi hiyo mwaka jana wakati wa opereshen M4C kule Mtwara na Lindi.

Mkataba upi, wa mradi gani, wa ndhi gani uliwahi kuwekwa wazi? Hoja hiyo haizingatii kwamba sisi ni taifa lenye ushindani na mataifa mengine......kila kitu cha nyumbani kwako unaanika hadharani? Ndivyo Chadema itakavyokuwa inaendesha nchi kihivyo? Mbona mtatuuza mapema sana. Siamini afterall kama mtafanya hivyo, maana kama mmeshindwa kuuweka hadharani mkataba wa kumpa mkopo Dr Slaa....ndio mje kuuweka wazi mkataba wa gesi?
 
"Mheshimiwa Spika, kutokana na unyeti wa mradi huo kwa mustakabali wa nchi na maisha ya wananchi wa sasa na baadaye, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuwasilisha Bungeni na kuweka wazi kwa umma mkataba wa mradi husika ili Bunge liweze kuishauri na kuisimamia Serikali kuanzia katika hatua za awali kuhakikisha kwamba maslahi ya Taifa yanalindwa katika hatua zote na pia wananchi wananufaika kutokana na fursa za uwekezaji"

hapa uongo uko wapi?

Conveniently umeacha para zenye kuonyesha ukigeugeu....rudi upaste upya whole para, utauona ukigeugeu
 
Chadema wanasema wananchi wanufaike na mradi huu au haujaielewa sentesi ya mwisho, hata hivyo kubadilika kwa maslahi ya taifa sio dhambi na kuwasikliza wananchi kile wanachokitaka, toa post yako haina mashiko.
 
Haya Chadema waongo,achaneni nao,ila mke wenu CUF amewasaliti huko,yeye ndiyo mkweli,au hamjawapa ya mboga,na mwambieni Baba Ritz akawasikilize wampige hata jiwe moja tu,wamtoe jino aache kuchekacheka kama,,,,!
 
Chadema wamejitokeza kuhamasisha watu wa Mtwara tusikubali ujenzi wa bomba la gesi. Waziri kivuli wa Nishati na Madini wa Serikali hiyo Mhe Mnyika ametoa matamko ya kuunga mkono hoja za watu wa Mtwara kuhusu kukataa ujenzi wa bomba la gesi. Lakini ni wazi kwamba Chadema hawasemi ukweli,ni vigeugeu, na wadandia hoja kwa ajili ya kutafuta umaarufu wa chapchap.

Ushahidi wangu huu hapa........angalia hansard uone walichosema Bungeni katika taatifa ya kambi rasmi ya upinzani Bungeni....


http://polis.parliament.go.tz/PAMS/docs/HS-8-34-2012.pdf

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani ilitaka kiwango cha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuongezwa ili vipaumbele vifuatavyo viweze kuzingatiwa kwa uzito unaostahili: Kuwekeza fedha za kutosha kwenye sekta ya umeme na Gesi ili kumaliza kabisa tatizo la nishati ya Umeme na kupunguza gharama za maisha.

Mheshimiwa Spika, hatua hizo ziambatane na kuwekeza katika Bomba la Gesi, pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant) ili kuwezesha gesi kutumika kwenye magari, viwandani na majumbani; kuhakikisha tunazalisha 360MW za umeme kila mwaka ili kufikia malengo ya Mpango wa Maendeleo wa miaka Mitano na kumaliza tatizo la mgawo wa umeme na mwisho kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya usafirishaji na usambazaji wa umeme vijijini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi vijijini

Mheshimiwa Spika, mzigo huu usingekuwa mkubwa iwapo Serikali ingetekeleza katika mwaka wa fedha 2011/2012, maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani ya kuhakikisha nyongeza ya fedha kwenye bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa upande wa Sekta Ndogo ya Gesi kwa ajili ya mitambo ya umeme na kuharakisha kuwekeza katika Bomba la Gesi pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant). Mheshimiwa Spika, kutokana na hatimaye Serikali kuzindua ujenzi wa bomba la gesi katika mwaka wa fedha 2012/2013 na ahadi ya Wizara ya Nishati na Madini kuwa ujenzi huo utakamilika katika kipindi cha miezi kumi na nane ijayo, Kambi Rasmi ya Upinzani inataka Serikali kutoa kauli ya uhakika kwa Taifa.

Mheshimiwa Spika, mradi mkubwa wa maendeleo ambao umepangwa katika mwaka wa fedha ni ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es salaam.

ambapo kwenye kasma 3162 umetengewa kiasi cha shilingi 93,000,000,000 huku kiwango kingine cha fedha za mradi huo kikitarajiwa kupatikana kutokana na mkopo kutoka nje. Mheshimiwa Spika, kutokana na unyeti wa mradi huo kwa mustakabali wa nchi na maisha ya wananchi wa sasa na baadaye, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuwasilisha Bungeni na kuweka wazi kwa umma mkataba wa mradi husika ili Bunge liweze kuishauri na kuisimamia Serikali kuanzia katika hatua za awali kuhakikisha kwamba maslahi ya Taifa yanalindwa katika hatua zote na pia wananchi wananufaika kutokana na fursa za uwekezaji


Hivi watu wa wa aina hii wanaoadilisha misimamo kutokana na upepo, watafaa kweli kuongoza nchi?


Maslahi ya taifa yako hapo, sioni sababu ya watu kuleta siasa kwenye suala muhimu kama hilo.
 
Chadema wamejitokeza kuhamasisha watu wa Mtwara tusikubali ujenzi wa bomba la gesi. Waziri kivuli wa Nishati na Madini wa Serikali hiyo Mhe Mnyika ametoa matamko ya kuunga mkono hoja za watu wa Mtwara kuhusu kukataa ujenzi wa bomba la gesi. Lakini ni wazi kwamba Chadema hawasemi ukweli,ni vigeugeu, na wadandia hoja kwa ajili ya kutafuta umaarufu wa chapchap.

Ushahidi wangu huu hapa........angalia hansard uone walichosema Bungeni katika taatifa ya kambi rasmi ya upinzani Bungeni....


http://polis.parliament.go.tz/PAMS/docs/HS-8-34-2012.pdf

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani ilitaka kiwango cha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuongezwa ili vipaumbele vifuatavyo viweze kuzingatiwa kwa uzito unaostahili: Kuwekeza fedha za kutosha kwenye sekta ya umeme na Gesi ili kumaliza kabisa tatizo la nishati ya Umeme na kupunguza gharama za maisha.

Mheshimiwa Spika, hatua hizo ziambatane na kuwekeza katika Bomba la Gesi, pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant) ili kuwezesha gesi kutumika kwenye magari, viwandani na majumbani; kuhakikisha tunazalisha 360MW za umeme kila mwaka ili kufikia malengo ya Mpango wa Maendeleo wa miaka Mitano na kumaliza tatizo la mgawo wa umeme na mwisho kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya usafirishaji na usambazaji wa umeme vijijini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi vijijini

Mheshimiwa Spika, mzigo huu usingekuwa mkubwa iwapo Serikali ingetekeleza katika mwaka wa fedha 2011/2012, maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani ya kuhakikisha nyongeza ya fedha kwenye bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa upande wa Sekta Ndogo ya Gesi kwa ajili ya mitambo ya umeme na kuharakisha kuwekeza katika Bomba la Gesi pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant). Mheshimiwa Spika, kutokana na hatimaye Serikali kuzindua ujenzi wa bomba la gesi katika mwaka wa fedha 2012/2013 na ahadi ya Wizara ya Nishati na Madini kuwa ujenzi huo utakamilika katika kipindi cha miezi kumi na nane ijayo, Kambi Rasmi ya Upinzani inataka Serikali kutoa kauli ya uhakika kwa Taifa.

Mheshimiwa Spika, mradi mkubwa wa maendeleo ambao umepangwa katika mwaka wa fedha ni ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es salaam.

ambapo kwenye kasma 3162 umetengewa kiasi cha shilingi 93,000,000,000 huku kiwango kingine cha fedha za mradi huo kikitarajiwa kupatikana kutokana na mkopo kutoka nje. Mheshimiwa Spika, kutokana na unyeti wa mradi huo kwa mustakabali wa nchi na maisha ya wananchi wa sasa na baadaye, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuwasilisha Bungeni na kuweka wazi kwa umma mkataba wa mradi husika ili Bunge liweze kuishauri na kuisimamia Serikali kuanzia katika hatua za awali kuhakikisha kwamba maslahi ya Taifa yanalindwa katika hatua zote na pia wananchi wananufaika kutokana na fursa za uwekezaji


Hivi watu wa wa aina hii wanaoadilisha misimamo kutokana na upepo, watafaa kweli kuongoza nchi?

Mimi nadhani unataka kutukumbusha Kwamba Mnyika na Chadema -Kambi Rasmi ya Upinzani walijua nini kitafuata ndio maana wakatahadharisha Mkataba uwekwe wazi ili ijulikane utawanufaishaje wananchi na taifa kwa ujumla uzuri umeleta uthibitisho mwenyewe
 
huyu mleta mada naisi naye ni mmmoja wa mafisadi, kiufupi serekari ya majimbo ndio mpango mzima
 
Wakati CDM wanatoa kauli yao Bungeni kuhusu mradi wa serikali wa ujenzi wa bomba la gesi, msimamo wa wananchi wa mtwara kuhusu mradi huo ulikuwa bado kutangazwa. Hivyo kama CDM wangetamka bungeni kwa wakati huo kwamba wananchi wa mtwara hawaungi mkono mradi huo, huo ungekuwa uzushi na uchochezi kwa wananchi wa mtwara kwamba waukatae mradi huo; Na hivyo leo hii wangeweza kubebeshwa lawama kuhusu yote yanayotokea huko mtwara na masasi kwa sasa hivi, kwamba yanatokana na uzushi na uchochezi wa CDM. Kumbe CDM wanaona mbali, wana vision ya hali ya juu.
 
Ni kweli Chadena waongo tu ukisoma maneno ya Mnyika ni tofauti anachosema sasa hivi. Chadema acheni siasa za matukio.

Unazifahamu sera za chadema wewe?? Serikali za majimbo??? Mambo ya mtwara yasingetokea kama serikali za majimbo zingekuwapo
 
Mkataba upi, wa mradi gani, wa ndhi gani uliwahi kuwekwa wazi? Hoja hiyo haizingatii kwamba sisi ni taifa lenye ushindani na mataifa mengine......kila kitu cha nyumbani kwako unaanika hadharani? Ndivyo Chadema itakavyokuwa inaendesha nchi kihivyo? Mbona mtatuuza mapema sana. Siamini afterall kama mtafanya hivyo, maana kama mmeshindwa kuuweka hadharani mkataba wa kumpa mkopo Dr Slaa....ndio mje kuuweka wazi mkataba wa gesi?

Unajua process za public contract....wananchi ni haki yao kujua mkataba unasemaje.....sijui kama una akili hata za kushikiwa tu......yaani mkataba ukiwekwa wazi ndio kuwauza???
Kwa hiyo kutokuwekwa wazi kunawasaidia vipi wananchi??? hujui kama hapo ndio kuuzwa bila kujua terms za mkataba??
JIFUNZE KUELEWA KWA SABABU UNAIBISHA JUKWAA HILI.
 
Kazi ya chama cha upinzani sio kushauri mipango ya serikali, hata ile ambayo hawaiungi mkono. Chadema wameweza mara kadhaa wameipinga mipango ya serikali ambayo hawakubaliani nayo....walishawahi hata kutoka nje ya Bunge ku protest. Hivyo wewe usitudanganye hapa kwa wameshauri mipango.....wameunga mkono, tena wakashinikiza mradi ukamilishwe haraka. Uzuri hii kitu ipo kwenye hansard...sio umbea wala majungu
Wewe Mbunge wa Namtumbo endelea kusinzia tu huko bungeni!

Hansard imesema CDM waliomba mkataba uwekwe hadharani ili wananchi wajiridhishe kama una tija kwao lakini magamba mkaukalia. Unajuaje pengine kama ungewekwa hadharani haya ya Mtwara yangeonekana mapema na CDM (Wabunge kwa ujumla wao) wangeshauri vizuri na haya yasingetokea? CDM hawana kosa kulingana na uliyokariri kutoka kwenye Hansard!
 
Chadema wamejitokeza kuhamasisha watu wa Mtwara tusikubali ujenzi wa bomba la gesi. Waziri kivuli wa Nishati na Madini wa Serikali hiyo Mhe Mnyika ametoa matamko ya kuunga mkono hoja za watu wa Mtwara kuhusu kukataa ujenzi wa bomba la gesi. Lakini ni wazi kwamba Chadema hawasemi ukweli,ni vigeugeu, na wadandia hoja kwa ajili ya kutafuta umaarufu wa chapchap.

Ushahidi wangu huu hapa........angalia hansard uone walichosema Bungeni katika taatifa ya kambi rasmi ya upinzani Bungeni....


http://polis.parliament.go.tz/PAMS/docs/HS-8-34-2012.pdf

Mheshimiwa Spika, Kambi Rasmi ya Upinzani ilitaka kiwango cha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuongezwa ili vipaumbele vifuatavyo viweze kuzingatiwa kwa uzito unaostahili: Kuwekeza fedha za kutosha kwenye sekta ya umeme na Gesi ili kumaliza kabisa tatizo la nishati ya Umeme na kupunguza gharama za maisha.

Mheshimiwa Spika, hatua hizo ziambatane na kuwekeza katika Bomba la Gesi, pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant) ili kuwezesha gesi kutumika kwenye magari, viwandani na majumbani; kuhakikisha tunazalisha 360MW za umeme kila mwaka ili kufikia malengo ya Mpango wa Maendeleo wa miaka Mitano na kumaliza tatizo la mgawo wa umeme na mwisho kutenga fedha za kutosha kwa ajili ya usafirishaji na usambazaji wa umeme vijijini ili kuchangia katika ukuaji wa uchumi vijijini

Mheshimiwa Spika, mzigo huu usingekuwa mkubwa iwapo Serikali ingetekeleza katika mwaka wa fedha 2011/2012, maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani ya kuhakikisha nyongeza ya fedha kwenye bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kwa upande wa Sekta Ndogo ya Gesi kwa ajili ya mitambo ya umeme na kuharakisha kuwekeza katika Bomba la Gesi pamoja na ujenzi wa mtambo wa kutengeneza Gesi (LPG extraction Plant). Mheshimiwa Spika, kutokana na hatimaye Serikali kuzindua ujenzi wa bomba la gesi katika mwaka wa fedha 2012/2013 na ahadi ya Wizara ya Nishati na Madini kuwa ujenzi huo utakamilika katika kipindi cha miezi kumi na nane ijayo, Kambi Rasmi ya Upinzani inataka Serikali kutoa kauli ya uhakika kwa Taifa.

Mheshimiwa Spika, mradi mkubwa wa maendeleo ambao umepangwa katika mwaka wa fedha ni ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara mpaka Dar es salaam.

ambapo kwenye kasma 3162 umetengewa kiasi cha shilingi 93,000,000,000 huku kiwango kingine cha fedha za mradi huo kikitarajiwa kupatikana kutokana na mkopo kutoka nje. Mheshimiwa Spika, kutokana na unyeti wa mradi huo kwa mustakabali wa nchi na maisha ya wananchi wa sasa na baadaye, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuwasilisha Bungeni na kuweka wazi kwa umma mkataba wa mradi husika ili Bunge liweze kuishauri na kuisimamia Serikali kuanzia katika hatua za awali kuhakikisha kwamba maslahi ya Taifa yanalindwa katika hatua zote na pia wananchi wananufaika kutokana na fursa za uwekezaji


Hivi watu wa wa aina hii wanaoadilisha misimamo kutokana na upepo, watafaa kweli kuongoza nchi.

Anzisha topic kwa kusoma au kuwa makini na unayotaka kuyaandika. Unaandika mwenyewe na kujichanganya mwenyewe.


Mheshimiwa Spika, kutokana na unyeti wa mradi huo kwa mustakabali wa nchi na maisha ya wananchi wa sasa na baadaye, Kambi Rasmi ya Upinzani inaitaka Serikali kuwasilisha Bungeni na kuweka wazi kwa umma mkataba wa mradi husika ili Bunge liweze kuishauri na kuisimamia Serikali kuanzia katika hatua za awali kuhakikisha kwamba maslahi ya Taifa yanalindwa katika hatua zote na pia wananchi wananufaika kutokana na fursa za uwekezaji
 
Soma hotuba ya Mnyika hapa http://mnyika.blogspot.com/2012/07/hotuba-ya-kambi-rasmi-ya-upinzani.html

Tamko la chadema utalipata kwenye blog hiyo hiyo ya Mnyika na website ya Chadema.....total contradiction. Wanathibitisha wasivyo chama makini.

Bora CUF wamekuwa na msimamo consistent toka mwanzo na sio kufuata upepo

Tehe tehe tehe, huo mstari wa mwisho ndiyo lilikuwa lengo lako hasa la post. Sasa mbona umeanza kwa uoga, huwezi hata kusema moja kwa moja kile ambacho wewe unaamini ni ukweli, sasa kama huwezi kujiamini mwenyewe, utaaminikaje na wengine kwamba unaweza kuandika kitu genuine?

Hotuba ya Ndugu John bungeni kwa niaba ya KUB ilikuwa very clear na ndicho ambacho ameendelea kukisema consistently kupitia njia za kibunge, na huo ndiyo msimamo wa chama, serikali iweke wazi mkataba juu ya mkataba.

Bahati nzuri sana sana, wewe mwenyewe umeiweka katika bandiko lako wakati ukianzisha post.
 
Kazi ya chama cha upinzani sio kushauri mipango ya serikali, hata ile ambayo hawaiungi mkono. Chadema wameweza mara kadhaa wameipinga mipango ya serikali ambayo hawakubaliani nayo....walishawahi hata kutoka nje ya Bunge ku protest. Hivyo wewe usitudanganye hapa kwa wameshauri mipango.....wameunga mkono, tena wakashinikiza mradi ukamilishwe haraka. Uzuri hii kitu ipo kwenye hansard...sio umbea wala majungu
Mkuu soma vizuri aya ya mwisho ya ulicholeta, uzi umeleta mwenyewe lakini inaonekana hukuchukua mda wa kutosha kusoma.
 
Mleta mada labda ungeweka na hiyo kauli yao (cdm) rasmi kuhusu mtwara gas, ili tuweze kudadavua vizuri uongo, ugeugeu na udandaaji hoja wao. Vinginevyo kwa quote hiyo ya hansard huwezi kuwabana hata chembe.

Hakuna kubanwa hapo, hapo kuna kuonesha jinsi magwanda walivyo vigeu vigeu na mleta mada kaweka kila kitu kinagaubaga na ushahidi kamili, nini usichokielewa?
 
Back
Top Bottom