Yaani aende huko ambako Mzee Kingunge kawaacha anasema vijana ambao hawajitambui wapinga mabadiliko....itakuwa kichekesho japo ana haki ya kwenda anapotaka...pumzi kule imeshakata sijui atapumua vipi
Ukisoma huo uchambuzi kwa mtizamo wa kimrengo lazima uone ni porojo ila mtoa mada ameeleza uhalisia wa demokrasia ya mdomoni tu ambayo tunayo hapa nchini kwetu
Yeye kasema anasubiri kwa hamu kuona uchaguzi wa mwaka huu kujua kama mkuu wetu wa nchi anahubiri tu demokrasia au anaizingatia na kumaanisha!!
Tafsiri yake ni kuwa uchaguzi utakuwa huru na wa haki..??
Maana yeye na wa Burundi wanalaumiwa hawana utawala wa demokrasia....Je anayewalaumu yeye...
Vijana wanaojua kuwa rasilimali za nchi hii zimekuwa zinahujumiwa na sasa wanataka mabadiliko ya mfumo ili kuwa na utawala unaowajali na kuwasikiliza...Lugha za viroba ni lugha za mtaani zisizo na mashiko...Hapa tunajadili uhalisia
Yeye mwenyewe alisema vijana wote wanaojitambua wanadai mabadiliko ila tu wale vijana wake aliokuwa anawaongoza ndo wapinga mabadiliko...ndo mlobaki sasa mnamwita hayo majina...badilikeni...haya ni majira huwezi kuyapinga...
Umenena vema...kiongozi huwa anasililiza zaidi na kuongea kidogo.Ndo maana tumepewa masikio mawili ili tusikilize sana na mdomo mmoja kwamba tuongee kidogo
Kura zipo za kutosha na watu hawalali maana wameshajua mabadiliko hayakwepeki.Hakuna utawala unaovuka miaka 40 ukiwa madarakani.Ni nyakati hata maandiko yanasema anayelijua hili wala hapingi.
Hakuna adui wa kudumu kwenye siasa ndugu.Mwaka 2002 Kenya waliunganisha nguvu na wengine wakajitoa iliyokuwa KANU wakaunda muungano wa upinde na kuchukua nchi.Marekani Rais wa sasa alikuwa hapatani kabisa na makamu wake wa rais alokuja mteua bwana Joe Biden.Sasa wewe unashangaa hayo Leo?Au ndo...
Wewe ni CUF IPI uliyopo ilihali Maalim Seif kasimama Zenji kuwakilisha ukawa na dar wabunge kama mtatiro wapo na kwingineko na wana nguvu kubwa sana.Labda utakuwa mamluki uungane na prof
Mpango wa mabadiliko Chadema umeanza kitambo kumbuka mwanzo wa kauli mbiu na nembo ya M4C....Lowasa kajakuongezea kasi...atasimamia matakwa ya wananchi kupitia muungano wa ukawa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.