WildCard,
Asante kwa maneno yako ya kutia moyo. Kadiri siku zinavyosonga mbele ndivyo na uelewa wa watu unavyoimarika juu ya jinsi CCM inavyowafukarisha kishenzi. Ni wazi hata wale mbumbumbu wa vijijini wanaoendelea kuwapa kura hao mafisadi wa CCM kwa kugawiwa t-shirt, khanga na visenti kidogo...
Awamu ya pili ya Mzee Ruksa tulishuhudia sakata la Loliondo kutaka kuuziwa Mwanamfalme wa hukohuko Uarabuni.
Awamu ya tatu ya Mkapa tulishuhudia mashirika ya umma na rasilimali za nchi kama madini vikiuzwa kwa wageni kwa bei ya kutupwa.
Awamu hii ya nne ya JK inaanza kuonyesha dalili za kuuza...
Naomba mnisaidie: Hivi hii ASB haiwezi kuwa inashabihiana na ile ABSA ya Sauzi iliyopewa NBC na huyo huyo Che Nkapa licha ya kuwa aliyeshinda tender ya kununua NBC alikuwa mwingine? Duh! kumbe Che Nkapa aliamua kuiacha nchi kapa kwa kuuza kila kitu kwa wageni na nyumba za serikali kwa maswaiba...
Kama ni ajali, basi bahati mbaya. Ajali haina kinga. Sidhani kama ataweza kumgonga mtu kwa makusudi pamoja na jeuri aliyo nayo!! Tuwape pole wafiwa na kuwaombea furaha ya milele waliofariki. Hata Vijisenti tumpe pole kwa yaliyompata. Huo ndiyo uungwana.
Mzee (Jumanne) John Malecela, aliwahi kuwaambia watanzania waliokuwa wakilalamikia huduma mbovu za Shirika la Reli wakati yeye akiwa Waziri wa Mawasilano na Uchukuzi kwamba waende kuzimu "they go to hell". Sasa wakati umefika wa kumwambia "Mzee hovyo Malecela, go to hell" Sasa hivi hana la maana...
Sasa, nimeelewa, nchi hii haina mwenyewe. Nchi ya wanamtandao hiyo. Hata la kuendelea kusema sina. Tishio la Dr. Idris wa Tanesco liko bayana. Si muda mrefu Boss wa Maji naye akasema vivyo hivyo. Si umeme ndiyo nguvu ya kusukuma maji. Wana-JF, haya!!!
Dr. Shein alikuwa Makamu wa Rais wa Mkapa ambaye wakati wa utawala wake ufisadi ulijengwa na kuimarishwa kikamilifu. Sasa ni Makamu wa Rais wa Kikwete anayeendeleza ufisadi huo uliojengwa na Mkapa akisaidiwa na Shein. Hadi leo sijamsikia akikemea ufisadi kwa nguvu zake zote. Shein siyo...
Magufuli yupi? Yule aliyeshupalia kuuza nyumba za serikali akiwagawia hata ndugu na "washikaji" (wa kike) wake ambao si wafanyakazi wa umma? Aah!! tena siyo "kuuza" bali kugawiana, nyumba yenye thamani ya Shs. 150m/= inauzwa kwa bei ya kutupa ya Shs. 10m/= hadi 30m/=?! Wizi mtupu!!!!
Dr...
Naona Kijana Kipanya amejitahidi kufanya ubunifu. Kwa kweli kukusanya vijana wenye mfumo tofauti wa maisha (differing life styles) na kuwaweka pamoja katika maisha ya kijijini si jambo dogo. Naamini wale vijana watajifunza mengi kutokana na kuishi katika kijiji kile. Watakaporudi makwao watakuwa...
Umesema kweli Mr. Zero. Nami huwa nashangaa kwa nini Sherehe za Kidini kama vile Baraza la IDD, MAULID n.k. wanaalikwa viongozi wa siasa kuwa wageni rasmi? Hivi kweli hakuna viongozi wa Dini wanaoweza kualikwa na kushiriki kutoa mawaidha yenye manufaa kwa Dini tukufu ya Ki-Islamu? Hao viongozi...
Tatizo lao, ndugu KGM, ni kwamba Wabunge wa Kigoma hawana ushirikiano katika masuala yanayohusu maendeleo ya kwao Kigoma. Kama ulivyosema Serukamba ni mtetezi mkuu wa Mafisadi na alishiriki kwa nguvu zote kumsimamisha Zito bungeni wakati ule wa suala la Buzwagi. Ndugu yetu Msambya ni mwanasiasa...
Wananchi kukataa kuwachagua wasomi sana kunasababishwa na pande zote mbili, wananchi wenyewe na wasomi. Enzi za Mwalimu, wananchi wengi hawakuwa na elimu na/au uelewa wa uwakilishi Bungeni. Na wasomi wachache waliokuwapo walikuwa na tabia ya kujiona kuwa watu wa daraja la juu katika jamii na...
Jamani wacheni hawa CCM wajikaange na mafuta yao. Kwani 2010 iko mbali? Hata mtoto mdogo anajua kuwa CCM ni chama cha mafisadi. Mzee Kitine kasema ukweli na haupingiki. Uteuzi wa viongozi unategemea mtandao, uswahiba na siyo uwezo kama ilivyokuwa enzi za Mwalimu. TANU bwana kilikuwa chama cha...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.