BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
Date::3/18/2009
Dk Slaa ataka posho za wabunge zipigwe panga ziongezwe waalimu
Na Mussa Juma, Moshi
Mwananchi
Dk Slaa ataka posho za wabunge zipigwe panga ziongezwe waalimu
Na Mussa Juma, Moshi
Mwananchi
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Mendeleo (Chadema), Dk Wilbroad Slaa amesema posho wanazolipwa wabunge wakati wa vikao bungeni ni kubwa , hivyo kupendekeza kuwa kuna haja ya kupunguzwa, ili fedha hizo zisaidie kuongeza mishahara ya watumishi na hasa walimu.
Akizungumza wakati wa mkutano wa Operesheni Sangara katika kata za Rundugai na Bomangombe, Dk Slaa alisema wabunge wanalipwa fedha nyingi kwa siku wanapokuwa kwenye vikao vya bunge ambazo alisema zinazidi mishahara ya walimu wengi hapa nchini.
Takwimu zinaonyesha kuwa walimu wa shule za msingi hupata mshahara wa kuanzia jumla ya Sh166,199 na baada ya makato Sh141,000 wakati walimu wa sekondari ngazi ya diploma huanzia jumla ya Sh203,000 na baada ya makato Sh178,000, wakati walimu wa shahada hupata kuanzia Sh360,000 na baada ya makato Sh270,000.
Posho za wabunge kila siku wanapokuwa katika vikao vya Bunge kila mmoja anapata Sh135,000 na kwa wiki tatu wanazokaa mjini Dodoma wakati wa vikao vya kawaida hupata jumla ya Sh2,835,000
Dk Slaa alisema suala hilo amekuwa akilipigia kelele kila wakati, lakini kutokana na kuwepo na wabunge wengi wenye ubinafsi, suala hilo limekuwa likipingwa na hivyo kuwataka wananchi kubadilika na kuchagua wabunge wengi wa upinzani, ili kuongeza nguvu bungeni na kusaidia kulinda malislahi ya nchi.
Alisema njia pekee ya kuondoa hali hii ni wananchi kuamka na kuchagua viongozi na wabunge wengi wa upinzani ambao watasaidia kutetea maslahi ya wananchi kwa kulinda fedha nyingi zinazopotea na kuwanufaisha watu wachache.
Akizungumzia kuhusu fedha mbalimbali zinazotolewa na serikali kuu na mifuko mbalimbali ya maendeleo ya jamii, Dk Slaa aliwataka wananchi kujenga tabia ya kuhoji mapato na matumizi ya fedha hizo zinazoletwa katika halmashauri za wilaya na manispaa kwa lengo la kuanzishia miradi ya maendeleo.
"Mimi kama mwenyekiti kamati ya hesabu za serikali za mitaa, nimebaini kuwa fedha nyingi za serikali haziwafikii walengwa lakini wananchi hamjui na wachache mnaojua hawahoji lolote," alisema Dk Slaa.