Ndugu yangu, viongozi wengi na watumishi wa serikali ni wanafiki wakubwa, ni bendera fuata upepo, ni wachumia tumbo, watakusifia na kukulamba miguu ukiwa madarakani ili mikono yao iende kinywani. Madaraka yakiisha wanakugeuzia mgongo na kuanza kumkumbatia mrithi wako na kukubeza wewe. Ukiwa juu...
Huko nyuma nilimuona Dr Shein kama kiongozi mwenye busara kiasi, lakini nimegundua na yeye ni boya tu. Hata hiyo kamati ya kina Mwinyi, Dr Salmin na wengineo sioni hasa wanajadili kitu gani wakati ukweli unaonekana waziwazi. Ingekuwa heshima kubwa kwa viongozi hawa wastaafu kumshauri Shein...
Mimi nadhani hawa viongozi wetu wa Afrika wamechoka kufikiri. Azimio hilo kiukweli ni la kulinda serikali kandamizi zifanyazo mauaji kwa raia wake na kuwatesa pasipo chembe ya huruma kwa kujua kuwa wakijitoa ICC hakuna chombo kitakachowashughulikia kuhakikisha sheria inachukua mkondo wake. Na...
Kikwete ni sawa na sijui nimlinganishe na nini aisee, maana kwa uzembe wa makusudi alioufanya akiwa madarakani yaani huwezi hata kumwelezea ni mtu wa aina gani!!! Kwa kipindi cha miaka kumi aliyokaa madarakani ni kama vile nchi haikuwa na kiongozi, nchi ilienda kwa kusukwasukwa huku na kule kama...
Huo uhuni wa serikali ya CCM usifumbiwe macho, ni ishara tosha ya ubakwaji wa demokrasia nchini. Kama nchi hii inayopigiwa mfano wa amani tunafanya hivi, tuna tofautu gani na mtu kama Kurunzinza?
Naungana na wewe asilimia mia. Wakati wa JK nchi ilikuwa imesimama kana kwamba haina kiongozi. Kibaya zaidi ni pale zilipoibuka kashfa kubwa kubwa na akashindwa kuwachukulia hatua wahusika. kingine kikubwa kuliko vyote, kuna kashfa alizibeba mabegani mwake yeye mwenyewe kwa vile alikuwa nazo...
Profesa Muhongo ni mmoja wa viongozi waliochotewa fedha nyingi kwa mabilioni kwenye lumbesa kutoka benki ya Stanbic ambayo kutokana na kuwa na ubia na viongozi wa chama tawala(CCM) benki hiyo imekataa kutoa orodha ya wanufaikaji wa pesa hizo. Na kutokana na kashfa hiyo ya kutakatisha fedha...
Ninakubaliana na wahenga waliosema kweli kwenye miti hakuna wajenzi. Watanzania tulipaswa kuishi maisha bora zaidi duniani kuliko hata raha ile ya maisha ambayo Rais Gadaffi wa Libya aliwapa wananchi wake. Hebu jaribu kuvuta fikra kama nchi mfano ndio ingekuwa Japan leo ingekuwaje?
Tanzania inasifiwa kwa viongozi kuachiana madaraka kila baada ya vipindi viwili bila kigugumizi kutokana na uwepo wa sheria hii kandamizi ya kutomshitaki Rais,kwa vile anajua hata akifanya maovu kiasi gani akiondoka madarakani sheria itamlinda. Tumeona haya kwa Mwinyi, Mkapa muasisi wa ufisadi...
Inasikitisha sana watanzania tunavyodanganywa kama watoto kuhusiana na suala hili la umeme, ni kwa nini serikali nyakati zote haisemi ukweli kuhusu tatizo la umeme nchini? Kabla ya uchaguzi Waziri George Simbachawene alituhakikishia uwepo wa huduma wakati wote na giza kuwa historia kufuatia...
Tangu kuanza kwa bomoabomoa jijini DSM nimekuwa nikijiuliza swali moja,"Namna zoezi linavyoendeshwa ni sahihi?" Nafahamu kabisa wananchi kuishi maeneo ya mabondeni ni kuhatarisha maisha yao na mali zao, nafahamu pia kuwa maafa kadhaa yamewahi kutokea na kusababisha madhara mengi ikiwamo vifo...
Serikali iliyopita ya JK ilikuwa ya wapiga dili tu, nani alijali udhibiti wa raslimali za taifa, zilimhusu nini? Kama twiga anaweza kusafirishwa kwenye ndege pasipo kujulikana ni vingapi vilipita kabla? Huyu aliyekamata fuvu leo kwa maana ya taasisi alishindwaje kukamata wanyama zaidi ya 100...
Kikwete kalihujumu taifa kwa kiwango cha kutisha kabisa, hatuwezi kukaa kimya eti sababu kastaafu, ni jukumu letu kupiga kelele na kuhahakikisha kuwa sheria zinabadilishwa ili na wao wapambane na mkono wa sheria.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.