Ni kweli "wanampenda" JPM na "kumchukia" JK?

Elli

Platinum Member
Mar 17, 2008
55,520
86,081
Kuna baadhi ya nyakati katika maisha binadamu mtu hupaswa kusimamia kile anachokiamini, akakiheshimu na kukiishi hicho! Binafsi nimechukizwa na nimefadhaishwa sana na kelele za baadhi ya wafuasi wa CCM wakimlaumu JK kuwa amefilisi nchi, nchi imefika pabaya kwa "uzembe" wa JK. si hao tu hata baadhi ya Viongozi wa kisiasa nikimaanisha DC na RCs na wengine wenye dhamana hizo wamesikika si mara moja wala mara mbili wakimkebehi JK aidha kwa maneno na matamshi yao au hata kwa vitendo vyao, mifano iko wazi kwa hili; kuzuia watu kwenda likizo, kufungia wafanyakazi nje ya geti, kufunga watu bila mpangilio eti tu kwa kushindwa kutekeleza jambo Fulani, na mara zote wakijibu kwa kujiamini kuwa hii ni AWAMU MPYA na kwamba sasa "wanafanya kazi" Rubbish!!!!

Lakini watu hawa hawa, miaka kumi iliyopita yaani karibia siku 700 nzima wamekua wakimsifu JK, hata pale tulipolalamika, watu hawa hawa waliandaa Press Conference na maandamano ya kumsifu JK, magazeti yakajazwa maneno mazuri ya sifa dhidi ya JK. Tulilia weeeee kuwaomba watu waone kuwa nchi inakoelekea siko kwenyewe lakini kamwe hatukusikilizwa. Cha ajabu leo hii watu hawa ndio wako mstari wa mbele kumkosoa JK kwa mgongo wa JPM..... kweli watu hawa wana akili timamu? Huu ni unafiki uliopitiliza.

Labda la mwisho kwa leo, kwa dhambi yenu hii hii ya unafiki, Magufuli nae mtamfanyia haya haya ya JK kwakua wengi wenu ni wachumia tumbo na mnaolinda maskahi yenu na watoto wenu, mimi nasema hivi, serikali ya CCM labda atokee malaika ndio itakua safi, nje ya hapo sitakaa nitegemee lolote toka kwa mtu aliye ndani ya CCM.

Hakuna dhambi mbaya kama unafiki.
 
Jk anachukiwa na chadema kwa juhudi zake kulizuia fisadi lisiingie ikulu, na kuzuia kulinda kura mita 200
 
Jk anachukiwa na chadema kwa juhudi zake kulizuia fisadi lisiingie ikulu, na kuzuia kulinda kura mita 200
Fisadi JK anachapwa za uso tu fisadi mwenzake Maguufuli muuza nyumba na mnunua feri mitumba hana ajizi naye yamrejea huko aliko Tanzania hapakaliki Mzee wa msoga maisha yake Ethiopia na Washington achana na Lowassa bwana mdogo kina kirefu huyo
 
Viongozi wengi wa ccm sio wakweli ni watu wa kujikombakomba tu kwa wakubwa wao
 
ASANTE!!!

Kikwete ni sawa na sijui nimlinganishe na nini aisee, maana kwa uzembe wa makusudi alioufanya akiwa madarakani yaani huwezi hata kumwelezea ni mtu wa aina gani!!! Kwa kipindi cha miaka kumi aliyokaa madarakani ni kama vile nchi haikuwa na kiongozi, nchi ilienda kwa kusukwasukwa huku na kule kama meli isiyo na nahodha. Nchi haikuwa na dira kabisa.
 
Ndugu yangu, viongozi wengi na watumishi wa serikali ni wanafiki wakubwa, ni bendera fuata upepo, ni wachumia tumbo, watakusifia na kukulamba miguu ukiwa madarakani ili mikono yao iende kinywani. Madaraka yakiisha wanakugeuzia mgongo na kuanza kumkumbatia mrithi wako na kukubeza wewe. Ukiwa juu siku zote ogopa watu walio royal sana kwako, hao ni wapambe tu. Angalia yanayomkuta J.K. mambo yake yote yaliyofichwa kwa kivuli cha urais sasa yanawekwa hadharani na walewale waliokuwa wakijipendekeza kwake. Chezea watanzania wewe.....!!!
 
Back
Top Bottom