Wacha azungumze hii nchi ilishaharibika viongozi waliachia watendaji wakwapue kwa wanavyotaka hivyo inahitaji ukichaa kidogo kufanya maamuzi Magumu kama haya. Wanaomkandia nahisi ni masalia ya walionufaika na ukwapuaji wa utawala wa awamu ya 4. Magufuli aluta continua
Jana tu Balozi wa Norway kutembelea ofisi za CUF ndio imekuwa noma!? kama alienda kuwashawishi wakubali kurudia uchaguzi si jema hilo? CCM mbona mnaweweseka na kivuli?
Wabunge watamkumbuka Mussa Hassan Zungu. Zungu alikuwa ana balance CCM na UKAWA lakini Tulia hajatulia alimnyima kabisa Mbunge wa Kilombero Mh. Lijualikali achangie taarifa ya kuzama kivuko kwenye jimbo lake!?
Waingie hata breweries TBL wapange bei elekezi Bia ziwe buku buku, na masokoni mchele kilo iwe buku buku nk. Wazazi hawana shida na Ada shule za Academy maana kuna standard and quality (monies worth) na ukifanya utafiti shule za Serikali ambayo ada ni 70,000 gharama ya mwanafunzi mmoja kwa mwaka...
CCM ni ile ile haitabadilika hata Malaika akitua hapo. Magufuli kama Kikwete tu yaani kuna shida ya ajira wasomi wenye madigrii (degree) wanauza Mpesa na vocha za simu. Watu wamefanya Kazi miaka 30+ amefikia muda wa kustaafu (miaka 60) unampa kazi nyingine yenye cheo Katibu wa mkoa (RAS) hi si...
Mwandishi Mosses Mathew ni Kibaraka wa CCM hata hoja zake asimamii ukweli bali ukada wake. Juzi pia hapo hapo StarTV alitetea sana Serikali ya CCM kuzima matangazo Bungeni ya moja kwa moja (Live) bila kuwa na hoja ya msingi. Sababu alizosema Waziri Nape ni 3 ambazo ni gharama kubwa, watu wafanye...
TBC wanapata ruzuku, hawalipi kodi, hawalipi pango, wanapata mishahara kutoka serikali kuu wanasema ni gharama kuonyesha live Bunge. StarTV na ITV kupitia EATV hawapati ruzuku, wanalipa kodi na wanajigharamia kila kitu wanaonyesha Bunge Live. Kuna kitu wanaficha na ni uchaguzi Zanzibar. Nipe TBC...
Penda usipende Bila kujua English fluently utaachwa nyuma kimataifa, nashangaa watanzania tunapiga vita lugha ya kiingereza na hata juzi kwenye mdahalo wa ITV walimu wanadai lugha ya kufundisha kutoka shule ya awali hadi Chuo Kikuu iwe kiswahili!? Kiingereza ndio Kiswahili cha Dunia, hapa nchini...
Benki kubwa kama CRDB itakosa changamoto!? Mbona Benki kuu BOT na maswala ya Escrow husemi Governor ajiuzulu!? Hata Ikulu utawala wa JK na makashfaa yote mbona hakupigania Rais awajibike!? Aidha una wivu wa kike au umetumwa
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.