'Ujinga' wa Ikulu unarudi kwa kasi

'Ujinga' wa Ikulu unarudi kwa kasi

Bei elekezi kwenye nauli za mabus na daladala, mafuta ya magari, maji na umeme uliona powa tu. Sasa imekuja sehemu yako unayonyonyea wananchi umeona nongwa eeh? Subiri uisome namba. Na bado zinakuja bei elekezi kwenye kodi ya nyumba za kupangisha, guest house na gharama za hospitali. Mtanyooka tu

😀😀😀
 
Uzi mtamu huu....Ila kiukweli mm naona bora ada elekezi itolewe hali ilizidi kuwa mbaya sana kwani bei zilizidi kupanda...hivyo hivi sasa mzazi mwenyewe ashindwe tuuu kumsomesha mwanae
 
Cha msingi kinachotakiwa kufanywa ni kuboresha shule za serikali kuanzia msingi hadi sekondari.Zamanishuleza serikali zilikuwa bora zaidi kulikoza binafsi kwasababu walimu walikuwa wanaheshimika na umuhimu wao kuonekana.Leo walimu wanadharaulika kiasi kwamba mtoto akifeli shule wanasemasi uende ualimutu.Mjinga anafundisha sijui huyu mwanafunzi anayefundishwa na Failure wa shule anakuaje.

Serikali isikimbie kivuli chake ianze kuboresha shule zake.Hata kama ikianza na kila mkoa shule moja tunajua zote haziwezekani kwamara moja lakini kila mkoa shule moja ya primary na moja ya sekondari,walimu waboreshewa stahiki zao.Hizi nyingine zote hazitakuwepo.
 
Kwanza mleta mada jiulize, hao wenye shule waliomba kutoa Huduma au kufanya biashara?

kabla ya kuanza kutukana Ikulu jitukane mwenyewe kwanza mpumbavu wewe...
 
Waingie hata breweries TBL wapange bei elekezi Bia ziwe buku buku, na masokoni mchele kilo iwe buku buku nk. Wazazi hawana shida na Ada shule za Academy maana kuna standard and quality (monies worth) na ukifanya utafiti shule za Serikali ambayo ada ni 70,000 gharama ya mwanafunzi mmoja kwa mwaka ni zaidi ya 3,000,000 sema tu ni kodi zetu hatujui na haiumi. Waboreshe shule zao watoto wasibebe fagio na dum na wasivae yeboyebo.
 
Kwanza mleta mada jiulize, hao wenye shule waliomba kutoa Huduma au kufanya biashara?

kabla ya kuanza kutukana Ikulu jitukane mwenyewe kwanza mpumbavu wewe...
HUDUMA YOYOTE INAUZWA! KWA HIYO KILA HUDUMA NI BIASHARA! KUMBUKA: DUNIANI KOTE NA SIKU ZOTE NI VITU VIWILI TU YINAVYOUZWA: 1. BIDHAA. 2. HUDUMA
 
BORA UMESEMA, SIO KILA MTU AJIPANGIE BEI TU, FIKIRIA KUNA SHULE YA TANGU MWAKA 1990 KILA MWANAFUNZI MPYA ANALIPIA MAJENGO!! MPAKA SASA INGETAKIWA ITAIFISHWE MAANA HAYO MAJENGO SIO YAKE TENA YAMESHALIPIWA!! LAKINI BADO WANATOZA TU, DAWATI LINAKAA MIAKA ILA KILA MWANFUNZI MPYA ANALIPIA, UKAGUZI NI WA SERIKALI ILA UNALIPIWA!!
nisaidie ni kwa nini watu mmeambiwa na serikali yenu kuwa inatoa elimu bure lakini hamtaki kuwapeleka kwenye hizo shule za bure?!
 
Serikali basi ichukue jukumu la kulipa walimu wa shule hizi pamoja gharama nyingine, mie binafsi nafanya private, salary pekee kwa mwezi mmoja kwa staff wote ni million 26 fanya sasa kwa mwaka mzima, natumai jibu mtalipata
 
Hapo bado sijafanya hesabu ya msosi wa wanafunzi na ghasia nyingine kibao, wamiliki wa hizi shule zitawashinda kwa mwendo huu
 
Hii tabia ya serikali kuanza kuirudisha nchi kwenye mfumo wa ujamaa, ambao ulithibitika kwa vitendo kuwa mfumo wa kijinga, usiotekelezeka, unaogandisha mawazo na unaowafanya viongozi kuwa watawala pekee na siyo viongozi kweli; ni upotofu na udikteta wa hali ya juu. Serikali yoyote inayopanga bei ni serikali ya wajinga, wenye mawazo mgando na madikteta!

Hivi karibuni serikali ya ccm na magufuli wametangaza kuzuia shule binafsi kupandisha ada eti wangoje kile ambacho ikulu walikiita "ada elekezi".

Nasema huu ni ujinga kwa sababu kinachopaswa kuihusu serikali katika shule binafsi ni kuhakikisha wanafuata mtaala wa nchi tu. Tofauti na hapo hakuna kingine. Kumbukeni hakuna kodi yoyote ya mtu iliyotumika kujenga ama kugharamia chochote kwenye hizi shule!

Sasa kwa nini waingiliwe?! Hivi serikali haitupi ujumbe kwamba kwenye shule binafsi ndiko kuliko na elimu bora na kwa hiyo haki ya kupata elimu bora maana yake ni haki ya kusoma kwa bei ndogo kwenye shule binasi?!

Boresheni shule za walipa kodi. Porojo hatutaki!
Mimi binafsi sioni kama Ikulu inaleta ujinga wa kiujamaa hapana kwa mtizamo wangu Ikulu ina lengo lakusaidia jamii yenye kipato cha chini na kati kuweza kumudu gharama za shule zinazotozwa na shule binafsi na hakuna pahala ambapo mzazi analazimishwa na serikali kumpeleka mwanae shule hizo bali kuweka utaratibu wa ada ni wazo zuri lenye masilahi mapana kwa watu ili kuondoa ugumu wakulipia gharama zingine,, ukiangalia ada tunazolipa shule za serikali ni ndogo sana pamoja na malazi, chakula ni muhimu kuangalia umuhimu wakuisaidia jamii ifurahie matunda ya uhuru kwa kila mtanzania na si kubagua makundi ya wenye nacho na wasionacho.
 
Hakuna kokote duniani uhuru wa Soko husio na mipaka, Hata kama kuna free market lazima Serikali makini kuwepo na government intervention na pia kumbuka kuna hali ya mtaji ( the consumer rights) ni serikali Ndo msimamizi wa yote haya.
 
DAH, MKUU WANGU SIJUI KAMA UNAJUA ULISHOKIANDIKA, AU UNAMASLAI NA ULISHOKIANDIKA. MUNGU AKUSAIDIE NDUGU MAANA HUJUI UTENDALO. HIVI UNAJUA NCHI ILIPOKUWA INAENDA? UNAJUA PENGO LA WASIO NACHO LILIKUWA NI BOMU AMBALO LINGELIPUKA WAKATI WOWOTE? JE! UNGEWEZA KUINJOY MAALA AMBAPO WENYE NACHO TUNGE UWAWA KWA KUVAMIWA NA WASIO NACHO? HEMBU TUACHE UBINAFSI TUUNGE MKONO PALE SERIKALI INAPOFANYA VIZURI KWA MASLAI YA MASKINI WENGI WA NCHI HII. TUSIANGALIE MATUMBO YETU, TUFIKIRIE NA WENGINE.
 
Mleta mada ni mbumbumbu wa maana, ana viwango vya kimataifa huyu vya umbumbumbu, kama vipi tumpeleke tu olyimpiki atuletee medali ya dhahabu
 
Naiunga serikali mkono, na wamiliki wa shule ambao watazingua wanyang'anye leseni ya biashara.
 
Hii tabia ya serikali kuanza kuirudisha nchi kwenye mfumo wa ujamaa, ambao ulithibitika kwa vitendo kuwa mfumo wa kijinga, usiotekelezeka, unaogandisha mawazo na unaowafanya viongozi kuwa watawala pekee na siyo viongozi kweli; ni upotofu na udikteta wa hali ya juu. Serikali yoyote inayopanga bei ni serikali ya wajinga, wenye mawazo mgando na madikteta!

Hivi karibuni serikali ya ccm na magufuli wametangaza kuzuia shule binafsi kupandisha ada eti wangoje kile ambacho ikulu walikiita "ada elekezi".

Nasema huu ni ujinga kwa sababu kinachopaswa kuihusu serikali katika shule binafsi ni kuhakikisha wanafuata mtaala wa nchi tu. Tofauti na hapo hakuna kingine. Kumbukeni hakuna kodi yoyote ya mtu iliyotumika kujenga ama kugharamia chochote kwenye hizi shule!

Sasa kwa nini waingiliwe?! Hivi serikali haitupi ujumbe kwamba kwenye shule binafsi ndiko kuliko na elimu bora na kwa hiyo haki ya kupata elimu bora maana yake ni haki ya kusoma kwa bei ndogo kwenye shule binasi?!

Boresheni shule za walipa kodi. Porojo hatutaki!

Nimesoma maelezo ya Serikali na inavyoonekana kuna utaratibu wa shule binafsi kuomba kibali cha kuongeza ada. So mwanajukwaa hapa umeteleza maana Serikali inatimiza wajibu wake kwa utaratibu uliopo.
 
Mtoa mada umejichanganya! Kama ulitegemea kuwaibia wananchi eti kwa kigezo tu kwamba hakuna mtu aliyechangia gharama za ujenzi washule umepotea! Lazima monitorig system toka serikalini ili kuwepo usawa gulan.
 
Back
Top Bottom