Na hapo ndipo ninapowaogopa Wa-TZ kwa usanii! Uchunguzi pia ufanyike ijulikane hata hicho cheti cha kuzaliliwa kilitolewaje? Na kama tunataka kushinda undanganyifu ktk taifa letu huyu kiongozi na awe mfano wa kukukiri hadharani kwamba alifanya udanganyifu.
Ndugu ningependa ufahamu jeshi la polisi Tanzania limepoteza ile heshima yake ya kuwa chombo cha kulinda raia na mali zao!.Baada ya polisi kuwa ni chombo cha kisiasa ndio maana unaleta uzi wa kuuliza ni kwa nini CHADEMA wanalaumu polisi.Ukweli ni kwamba polosi sasa ni chombo cha kusimamia...
Ni jambo la ajabu sana kwa mtu mzima na akili zake kuandika thread kama hii.Hata ktk nchi za vita hospitali na hotelini sio pahala pa kupiga boma kwa namna yoyote ile.
Kama huyo askari alikuwa pale kwa utaratibu ule pengine wa kufanyia uchunguzi mwili wa marehemu, nina uhakika hakuna kijana...
mleta mada inaonekana wewe ni mbumbumbu mkubwa na hatari kwa maendeleo ya taifa letu.Tabia ya kuanza kutoa utabiri ni ishara tosha ya umasikini wa kifikra ulionao na baadhi ya watu wengine.
Kwani wewe unayetoa taarifa ni kama nani? maana taarifa kama hii ilitakiwa kutolewa na mamlaka husika na si mwanachama tu wa mtandao wa jamiiforum.Ni vizuri tuaachia mamlaka husika wakatoa majibu kwani ni haki ya raia kupata maelezo juu ya maliasili za nchi yake.
Ndugu yangu!
Suala la kumsamehe Zitto sioni kama ni mjadala! Hii ni kwa sababu yeye mwenyewe Zitto alipaswa kuliona hilo mapema na kuomba msamaha! sioni kama chama kinapaswa kwenda kumuomba yeye Zitto bali yeye akiri makosa yake na kuomba msamaha! hapo tutamwona muungwana!.Kama akifanya hivyo...
Ni kweli hali ya polisi hawa imezidi! imetokea hata siku ya ibada J2! trafic yuko pale eneo la kanisani [Kristu Mfalme-Moshi] anatakiwa kuongoza watoto wametoka ibada ili waruke barabara.Mimi nilishuhudia askari wa kike akihangaika na kukagua magari na kudai rushwa huku watoto wakihangaika...
Chakunishangaza sio hizo kauli za Mhe. JK! kwani tumekwishamzoea! yeye anatumikia historia yake na wala sio Watanzania!.Cha ajabu hiyo inayoitwa taarifa kutoka ikulu! Jamani Tuache utani! watu wawajibike kwa wananchi nasio kutumia rasilimali za umma kuandika madudu!
Cha msingi hapa ni kutambua ya kuwa tekinolojia imekuwa! na hivyo watu wakome kutuma sms za matusi au vitisho kwa watu wengine hata kama ni kwa kutumia simu za wadogo zao! .Mkono wa sheria utakufikia tu!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.