Siyo siri hicho chama ni kero na wao wana mtazamo wa ajabu mno,kwamba ukiwa upinzani kila kitu kinachofanywa na serikali ya chama tawala wao watakipinga tu kisa eti hao ni ccm,ipo mifano hai Musoma ikiwa chini ya Chadema miradi mikubwa kama ule wa Maji Bukanga serikali ilitafuta fedha kwa Wafadhili ili kusambaza maji ktk Manispaa pamoja na Musoma Vijijini,siku ya Uzinduzi Chadema waliwakataza watu wao kushiriki sherehe hizo eti hiyo itawapa point CCM,upuuzi Mtupu,haya Sherehe ya Siku ya Wakunga Duniani ilifanyika Kitaifa Musoma Mara,kilichotokea watu waliambiwa hiyo ni Sherehe ya CCM,pamoja na kwamba alikuja rais wa chama hicho duniani,waliojitokeza ni Wakunga peke yao na watoto wa shule,aibu.Wkt wa kampeni za juzi kiongozi wa Baraza la Vijana Chadema aliwajeruhi baadhi ya wafuasi wa CCM akakamatwa na kuwekwa ndani huku majeruhi wakiwa wamelazwa hospitali,Mgombea wa Chadema akakusanya Wafuasi na Wapambe huku akiwaita Makamanda kuwa waende kituoni kumtoa kwa Nguvu kiongozi mwenzao kwa kauli kuwa Polisi wamemuonea,watu zaidi ya elfu wamekwenda kuzingira kituo,mgombea anaulizwa iwapo huyo aliyekamatwa ana Kinga yoyote ya Kisheria ya kutokamatwa,polisi wakachukua nafasi na kukamata wavamizi na pikipiki zaidi ya 30 zilizotelekezwa na hao wahuni,Jee ktk hili watu wangekufa nani angelaumiwa?mgombea kakamatwa na kuswekwa ndani kesho mahakamani,Mgombea bila aibu baada ya kupewa dhamana anaitisha Press Conference ooh polisi wanaonea,polisi wanatumiwa,polisi wametumia nguvu kubwa kuwakamata na kuwabambikizia kesi,kibaya zaidi Waandishi nao hawahoji maswali mazito ili ku-ballance taarifa yao nao wanaingia ktk mkumbo.Hakuna aliye juu ya sheria ndani ya JMT.