Weka ushahidi mezani tuanzie hapo, kubomoa huwa ni rahisi sana kuliko kujenga.
Afu nikwambie si kila mtu ni wa kumchafua ama kumdhulumu haki yake, wenye tabia kama yako(wachawi) huwa wanapima kwanza.
Jifunze usije ukaishi maisha ya laana.
Unaishi kwa mikopo unategemea uishi kwa furaha?
Unaishi kutegemea kubet unategemea uwe na furaha?
Tozo na kodi zisizoeleweka.
Taifa limejaa waongo na matapeli unategemea upate furaha?
Mambo ni mengi.
Ni kweli kabisaa, ila hapo inabidi uchague risk unayoimudu.
Ni heri kukosa pesa ila ukalala usingizi mzuri kuliko kuwa na pesa ukakosa usingizi kwa moyo kupanuka kwa presha.
Itoshe kusema hujawahi kufanya biashara na hujui unachokisema, hiyo attitude ya kiburi uliyonayo si sahihi kama kweli umedhamiria kuwa mfanyabiashara mwenye mafanikio. Ukiwa na mtazamo huo utamdharau hata mteja wako.
Kwenye biashara kuna kupanda na kushuka, haijalishi unaijua biashara kiasi...
Mkuu amini kila unachokipanda utakivuna tu, nikushauri usipende kuhukumu bila kuwa na uhakika maana kwa kipimo hicho hicho nawe utavuna. Kinachonitofautisha mimi na wewe ni uwezo wa mind kuchanganua mambo mimi niliona mlango ila wewe umeona ukuta, uko sawa.
Thread iko wazi, weka ushahidi hapa...
Wakuu kwema, kwa kiasi fulani nilifanikiwa. Na nitaleta mrejesho kwa siku za mbeleni, lengo ni kumtia moyo kila mpambanaji anayepitia magumu, ajiamini na aamini uwezo alio nao ni mkubwa kuliko matokeo yanayoonekana na watu. Ukiwa na focus, determination na discipline lazima utafanikiwa tu...
Mkuu biashara ni zaidi ya mtaji wa pesa, pesa ingekuwa kila kitu basi wafanyabiashara wote tungekuwa matajiri sana. Pesa pekee haitoshi kufanikisha biashara, hujui ni gharama gani nimetumia hadi kuwapata hao wateja, hujui ni kwa namna gani nimeweza kuaminika na hao wateja. Hujui ni kwa namna...
😁😁 mkuu hao ni wa uhakika sababu tu hakuna mshindani ndo maana SP anakuwa na kiburi. Huduma mbovu lakini utaenda tu maana huna cha kufanya.
Lakini mimi ninayo izungumzia ni ile ambayo mteja atamleta mteja kulingana na huduma yako kwake, pia demand yake inakuwa ipo juu kuliko upatikanaji wake.
Ni swala la kukaa mezani na kukubaliana 40/60 inawezekana.
Pia kwenye swala la pesa ujanja ujanja huwa ni mwingi sana hasa kwa sisi wabongo hivyo swala la kuzungukana huko mbele linawezekana kwa pande zote mbili. Kufika mbali itategemea na uaminifu wa sote ila hatupaswi kuaminiana kabisa, cha...
Kwasasa nina oda za kuuza korosho nyeupe, wateja ni wa uhakika.
Usalama wa pesa zako ni kuwa wewe ndo utahusika kwanzia kununua hadi kuuza ila tutakuwa pamoja kwenye kila hatua.
Faida kwangu nitapata gawio la asilimia hamsini ya faida itayokuwa imepatikana baada ya kutoa matumizi yote, pia...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.