Umemjibu vizuri, mtoa mada amekuwa mbinafsi sana kwa kujiangalia yeye tu na kushindwa kuwa objective. Katika khali ya kawaida mpaka hao wanaume wote wamuache lazima nae ana mapungufu yake na possible nao walimvumilia.
Naomba tu kumkumbusha kwamba kupanga kuolewa siyo kinga ya kupata malipizi...
Hiyo ndio tabia yake khalisi na ndio maana kila anapoomba msamaha na kuahidi kutorudia lakini mwishowe anafanya yale yale. Hivyo wewe ndio unatakiwa kuamua kama unaweza kuvumilia kuishi nae pamoja na hayo mapungufu yake au la, uwezekano wa kubadilika ni mdogo sana na wengi hawabadiliki sana sana...
Kweli vyuma vimekaza, dawa tu ya mswaki mbona kitu kidogo sana kanunue tu nyingine! Kuondoka nayo anaweza kuwa amesahau bahati mbaya au akawa na yeye anahitaji dawa ya meno na hamjamnunulia!
Kama haitambuliki kisheria hapo unaweza unaweza kuacha kulipa riba iliyosalia maana ni taasisi za fedha tu ndio kisheria zinaruhusiwa kutoza riba. Jambo la msingi lazima ukusanye ushahidi vizuri kuonesha kuwa ulishalipa mkopo halisi plus riba nyingi tu lakini deni haliishi. Tafuta bush lawyer...
Kutokana na uzoefu wangu tabia ni kilema siyo rahisi kuibadilisha baada ya umri fulani. Kama ulivyosema mwenyewe umejaribu kumbadilisha kwa mambo mengine lakini kwa hilo imeshindikana.
Nadhani una option mbili, kwanza maadam umetambua mapungufu yake mapema then ujipime kama unaweza kuyavumilia...
Tatizo la maoni yako ni upeo mdogo wa kufikiri. Wewe unaamini kuwa kuna single intervention ambayo inaweza kutatua matatizo mengi ya kijamii uliyoorodhesha hapo juu, kuboresha mazingira ya kazi. Lakini uhalisia hauoneshi hivyo. Baadhi ya matatizo mengi ya nchi hii yanatokana na viongozi na...
Suala la Osama linagusa usalama wa taifa na hilo kweli ni public interest na siyo suala la Dr. Slaa. Suala la Slaa ni public interest kwa muonekano wa UKAWA, kwa wana CCM na vyama vingine siyo muhimu kabisa. Hata hivyo hata kama umemuona Osama unatakiwa kumtaharifu boss wako alafu yeye ndio...
Whistle blower wapo lakini lazima ukubaliane na matokeo, afterall kutoa taharifa za Dr. Slaa siyo public interest kwa baadhi ya watu, ni public interest tu kwa wana UKAWA, hili naomba ulione kwanza. Na mara nyingi whistle blower popote duniani wamekumbana na changamoto kama iliyomtokea huyo wa...
Wewe naona unasukumwa na hisia zaidi kuliko kuwa professional. Kwanza ni marufuku kusema siri za wateja wa hotel na pia kuna mipaka katika kuongelea mambo ya taasisi na hasa kama wewe siyo msemji. Kwa baadhi ya mambo unatakiwa upate kibali cha mkubwa wako hata kama yanagusa masilahi ya taifa...
Kwa hiyo kama viongozi wengine siyo malaika ndio excuse ya Gwajima kutoa matusi kwa Kadinali Pengo? Kama ulifurahi Gwajima kumtukana Pengo, kwa nini tena leo unafurahi Gwajima huyohuyo anaposema Dr. Slaa amewatukana maaskofu na yeye atawatetea? Hii inamaanisha wewe na Gwajima wote wanafiki...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.