JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Covid-19 ni janga ambalo lilitikisa ulimwengu kuanzia mwaka 2019. Virusi vya korona ni jamii kubwa ya virusi vinavyojulikana kusababisha magonjwa yanayoanzia homa ya kawaida hadi homa kali kama vile Homa Kali ya Upumuaji ya Mashariki ya Kati (MERS) na Homa Kali ya Mfumo wa Upumuaji (SARS). Virusi hivyo kwa mara ya kwanza viligunduliwa 2019 huko Wuhan, China. Uzi huu utapitia baadhi ya nadharia zilizoibuka wakati huo pamoja na fafanuzi za kitalamu za nadharia hizo.
Salaam Ndugu zangu, katik pitapita zangu mitandaoni hasahasa kwenye mjadala unaomuhusu Dkt Slaa nimekuwa nikikutana na clip fupi ya Sekunde zipatazo 15 ikimuonesha anatamka kuhusu kupindua Serikali. Kwa namna Clip hiyo ilivyokatwa nashindwa kuelewa muktadha wa kauli hiyo. Naombeni mtusaidie kutafuta ukweli wa tukio hilo au Interview hiyo kwa kirefu zaidi. Clip niliyokutana nayo na inayosambaa ni hii hapa chini: Picha: Dkt Slaa Video 1: Kipande (clip) inachosambaa kwenye mitandao ya kijamii Video 2: Sehemu ya kipande cha Dkt. Slaa kwa urefu zaidi Chanzo: Star TV
Kwa taarifa za uhakika ni kuwa tangu January hadi sasa sio chini ya askari 20 walikwisha uwawa ila serkali Inafanya siri hata sisi hatukuruhusiwa kufika KIBITI kwa kuambiwa kuwa mkuu wa wilaya na kamati yake ya ulinzi na usalama hawaruhu Kwa kuwa eneo ni hatari sana. Kwa taarifa za uhakika ni kuwa wale magaidi wa kipindi cha magufuli wamerudi Kwa kasi wana silaha nzito za moto huku idadi ya askari ikiwa ndogo baada ya eneo kuonekana shwali baada ya operation ya kipindi cha magufuli Nitoe wito kwa serikali iweke wazi ili raia wajue nini kiaendelea rufiji kwa umma isifanye Siri huku hali ikizidi kuwa mbaya. USSR
Nianze kwa ku-declare interest kuwa mimi ni mzaliwa wa Mkoa wa Kagera Wilaya ya Missenyi. Katika makuzi yangu hasa baada ya kutoka nje ya mipaka ya mkoa wa Kagera, nimekuwa nikishambuliwa na kutaniwa sana kuhusu UKIMWI kuanzia mkoa wa Kagera. Hayati Rais Magufuli kwa nyakati tofauti amewahi kunukuliwa akiusema mkoa huko kwamba kila janga baya huanzia mkoa huo. Rais Magufuli awashangaa Kagera kila jambo baya kuanzia mkoa huo Pia watu mbalimbali katika mitandao ya kijamii wamekuwa wakiuponda mkoa huo kuhusu kuwa chanzo cha kuleta UKIMWI Tanzania. Je, ukweli ni upi kuhusu historia ya UKIMWI nchini?
Wakuu mko vyede? Kuna kipindi fulani hili suala lilizuka sana kuwa wanaoishi na HIV hasa matajiri walikuwa wanaenda South Afrika kubadilisha damu ili kupunguza makali ya ugonjwa huo. Hii ilikuwa kweli? Maana mpaka leo naamini walikuwa wanafanya hivyo, ila swali likaja wanabadilishaje? Wanamtoa damu nusu halafu wanamuongezea nyingine ambayo haina virusi ama? Msaada wenu kung'amua hili wajuvi.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limetangaza anuai mpya ya COVID-19 iitwayo EG.5 - iliyopewa jina lisilo rasmi "Eris" huku likishauri kila nchi kuchukua hatua mahsusi za kufuatilia uwepo wake. Lakini shirika hilo linasema inaleta hatari ndogo kwa afya ya umma, bila ushahidi kwamba husababisha ugonjwa mbaya zaidi kuliko lahaja zingine zinazozunguka kwa sasa.
Kizza Besigye na Yoweri Museveni walikuwa marafiki walioshibana wakati wa Vita ya Msituni Uganda kumuondoa Milton Obote miaka ya 1980, na Dkt. Besigye aliwahi kuwa daktari binafsi wa Museveni na wanajeshi wengine waliokuwa msituni pamoja na Museveni Rais Museveni na Winnie Byanyima walikuwa wachumba kati ya 1981 na 1986, Bi Byanyima alikuwa pamoja na Museveni alipoingia Kampala akiwa mkuu wa jeshi la waasi mwaka 1986. Lakini Museveni hakuwa tayari kumuacha mkewe, Janet, na Bi Byanyima akafukuzwa. Hatimaye aliolewa na Dkt. Besigye 1998. Inadaiwa kitendo kile kilimuuma sana Rais Museveni, kwanza akataifisha ranchi ya babake Winnie Byanyima, Mzee Boniface Byanyima. Pia matukio hayo ya ngono na usaliti yalijenga uadui mkubwa kati ya...
Back
Top Bottom