Nimesikia sehemu kuwa binadamu anaweza kupata usugu wa vimelea kutokana na kutumia mazao yatokanayo na wanyama mbalimbali, mfano wa mazao hayo ni nyama nk.
Hofu yangu ni kuwa wafugaji wengi siku hizi wamekuwa si waaminifu kabisa, wamekuwa wakitumia madawa hatari kwa ajili ya kukuzia haraka wanyama ili waingize sokoni, au wakati mwingine wamekuwa wakitumia madawa kwa ajili ya kuhifadhi mazao hayo ili yakae muda mrefu bila kuharibika.
Kumekuwepo cases nyingi za nguruwe na kuku kuchanganyiwa dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI.
JamiiCheck.com naomba mniondoe wasiwasi huu maana tunakoelekea huko mbeleni ni hatari.