JamiiCheck

A citizen-centered approach in countering misinformation and disinformation Online and Offline by JamiiForums

On JF:

Leo nimeona video ambao imewekewa sauti ya mtu akisema wametumiwa video hiyo kwenye group la shule ya Themihill, video hiyo inaonesha mtu akifungua kitu kinachoonekana kama pen (kalamu) ambacho ndani yake kina risasi na baadaye kufyatuliwa. Anayeelezea video hiyo anadai pen hizo zinagawiwa mashuleni na kuuzwa huku akionesha hofu ya watoto kuuana au wao wenyewe kujidhuru kwa peni hizo. Ningependa kufahamu ukweli kuhusu video hiyo.
TAARIFA KWA WANACHAMA, WANANCHI NA WAPENZI WA CHADEMA TANZANIA Ndugu wanachama, Wananchi na wapenzi wa CHADEMA, Tunapenda kuwajulisha kuwa tarehe ya uzinduzi wa Operation #NoReforms, NoElection – Kanda ya Nyasa (Mbeya) imebadilishwa kutoka 23 Machi 2025 hadi 1 Aprili 2025. Marekebisho haya yamefanywa kutokana na sababu za kifedha na maandalizi yanayohitaji muda wa ziada ili kuhakikisha uzinduzi unafanyika kwa mafanikio makubwa na kwa ufanisi wa hali ya juu. Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza na tunawashukuru kwa uvumilivu wenu. Tunaendelea kuwasihi muendelee kuwa na hamasa, mshikamano, na utayari kwa siku hiyo muhimu. Kamati ya Maandalizi: Operation No Reforms, NoElection Kanda ya Nyasa - Mbeya.
Wadau hamjamboni nyote? Taarifa kamili hapo chini kwa kimombo: “Eat whatever you want during Holy Week, the sacrifice is not in the stomach but in the heart. People abstain from eating meat, but they do not talk to their siblings and/or relatives, they do not visit their parents and do not take care of their children. They do not share their food with those who need it most, they distance their children from their father/mother and/or grandparents, they criticize the lives of others, mistreat their partner, etc. Meat does not make you a bad person, just as a fish fillet will not make you a saint. Better to seek a good relationship with God by doing good to others. Let us be less arrogant and more humble of heart.” Pope Francis
Wapo vijana wanaopita mitaani wanaodai wametumwa na serikali za mitaa, kwa lengo kuchukuwa namba za luku za kila mita na majina ya wamiliki, wakidai mapato hayo yanataka kuondolewa na kurudishwa katika halmashauri, je hili ni la kweli? Ushauri wangu kama ni la kweli, je kwanini mapato hayo ambayo yanakusanywa na TANESCO kila mwisho wa mwezi yasihamishiwe moja kwa moja katika halmashauri, badala ya kutaka kuvuruga mfumo safi uliopo?
Kumekuwepo na madai yanayosambaa mtandaoni kuwa makasha ya dawa za meno huwa na rangi (code) za aina mbalimbali zinazofafanua aina ya kemikali zilizotumika kutengenezea dawa hiyo. Aidha, madai hayo yanafafanua zaidi kuwa kemikali husika ni hatari kwa afya na husababisha saratani, na kwamba makampuni yanayozalisha dawa hizi hayawezi kukupa siri hii. Ukweli wake upoje?
Serikali ya Marekani na DRC wamekubaliana kwamba marekani itaruhusiwa kuchimba madini adimu maeneo ya mashariki ya DRC wakati huo Marekani itatoa vifaa vya ulinzi, tekinolojia ya kijeshi kwa jeshi la DRC . aidha pia kulinda maeneo ya kimkakati ndani ya DRC. Hayo yamejiri baada ya Rais wa DRC Felix Etiene Tshisekedi wa Mulumba kukutana na maafisa wa Marekani na kuwekeana mikataba kadhaa ya ushirikiano sambamba na kuwaondoa waasi wote ndani ya DRC.
Back
Top Bottom