Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa (UN), Dkt. Abdallah Possi, katika Kikao cha 61 cha Baraza la Haki za Binadamu, amejibu kauli za Jumuiya ya Ulaya, Uingereza, Uswisi, Sweden, Ireland, Ubelgiji na Norway pamoja na Human Rights Watch na Amnesty International kuhusu matukio ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania.
Akizungumza mjini Geneva Machi 2, 2026, Possi alisema Serikali imesikitishwa na kauli hizo alizodai zimechagua matukio bila kuzingatia muktadha.