Zombe Aishitaki serikali, adai 5.2 Billion!!

abdallah zombe amerudi tena.mara hii adai serka fidia ya bil5 na mil200 kama fidia ya ile kesi ya kuua wafanya biashara.
 
Watanzania tutaendelea kulipa fidia hizi zinazotokana nauzembe wa watendaji na viongozi wa serikali mpaka lini? ukichukua hili suala la Zombe, huyu bwana alipona mkono wa sheria kutokana na sababu za kiufundi; hivi sasa serikali italazimika kumlipa mabilioni ya fedha za walipa kodi. Zipo fidia nyingi zinazulipwa kwa makondrasi wa barabara kwa uzembe kama huo. Leo serikali inadaiwa fidia nyingi zinazotokana na mikataba mibovu. La kushangaza ni kwamba wakati watanzania masikini wanalazimika kukosa matibabu na elimu kutokana na matumizi hayo mabaya ya raslimali ya taifa, wale wanaosababisha hasara hiyo wanaendelea kupeta.
 
Hatutakubali kufanyika kwa malipo hayo. Tutaandamana watanzania wanajua aliyokuwa anayafanya Zombe na genge lake. Tunasubiri maamuzi ya mahakama. Hatutakubali ngo!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Abdallah Zombe afungua kesi ya madai akidai fidia ya shs bilioni 5.2. Wakati huo huo Jerry Muro na washtakiwa wenzake wamekutwa na kesi ya kujibu. RADIO1 STERE
 
Si mnataka haki za binadamu na demokrasia? mtu kakamatwa na madawa ya kulevya airport tena kayahifadhi kwenye rectum anapewa juice ya kuharisha anamwaga pipi kadhaa lakini utasikia tunafanya upelelezi ukikamilika atapelekwa mahakamani, huku nyuma mtu anaandaa namna ya kujitetea. wanasheria wanatuambia "somebody is not guilty until proved guilty and shall proved guilty in the court of justice" mimi si mwanasheria ila naamini nimeeleweka. Sasa kwa mtu aliyekamatwa na dope, bunduki na risasi bila kibali, pesa za moto nk kwanini wasinyongwe kama ilivyo Iran, Saudi Arabia, Syria na China? au akapelekwa jela moja kwa moja kuna haja gani ya kuanza kusikiliza kesi?

Kwa zombe askari wenzie walikiri kura jamaa alikua na mtandao wa majambazi na ndiye aliyeamuru wale mabwana wauawe na madini alichua yeye badala ya kifungo bila kesi au kungongwa ndiyo hayo sasa yanakuja na lazima alipwe kama akishinda kesi dhidi ya serikali. Cha msingi ni kuandamana kutaka sheria ya kumnyonga mtu pale anapopatikana na kosa la wizi, mauaji, rushwa na madawa ya kulevya. palepale amekutwa na pesa za moto au unga asomewe hukumu ya kunyonwa bila kujali ni ndugu yangu au ni nani itakua fundisho kwa wengine. Ukiandamana kupinga mtu kulipwa wakati mahakama yako imeshahukumu hivyo katika rufani zote itakua ngumu hata iwe ni chama gani kiko madarakani, njia ya kupinga hukumu ni kukata rufaa pekee na siyo tofauti ama la Zombe anyamazishwe kwa kuondolewa katika sura ya dunia.
 
Suala la madai ya fidia kwa Zombe haliwezekani sasa hivi de facto (as a matter of fact) wala de jure (as a matter of law) na kama ameanza taratibu hizo sasa basi mibangi anayovuta imekikoroga vibaya kichwa chake! Suala la kuachiwa huru kwake na wenzake liko kwenye hatua ya rufani Mahakama ya Rufani ya Tanzania ambayo haijaisikiliza rufani hiyo na haijatoa uamuzi. Sasa yeye anaomba fidia ya nini? Anajuaje kama Mahakama ya Rufani haitamtia hatiani kwa kushiriki mauaji ya wauza madini wa Mahenge Morogoro ambayo in fact he played a central role in commission of the same to the extent of fabricating evidence as to where the deceased were killed!
 
Watanzania tutaendelea kulipa fidia hizi zinazotokana nauzembe wa watendaji na viongozi wa serikali mpaka lini? ukichukua hili suala la Zombe, huyu bwana alipona mkono wa sheria kutokana na sababu za kiufundi; hivi sasa serikali italazimika kumlipa mabilioni ya fedha za walipa kodi. Zipo fidia nyingi zinazulipwa kwa makondrasi wa barabara kwa uzembe kama huo. Leo serikali inadaiwa fidia nyingi zinazotokana na mikataba mibovu. La kushangaza ni kwamba wakati watanzania masikini wanalazimika kukosa matibabu na elimu kutokana na matumizi hayo mabaya ya raslimali ya taifa, wale wanaosababisha hasara hiyo wanaendelea kupeta.

Colleague!

Unfortunately many Tanzanian voters are ignorant of their rights. People on power have been taking that adv to enrich themselves. I remember one day our Pres JK reported through TV that the qvt would refile/appeal for rejudgement of Zomba's case. How far has that gone? Hivi tunafanyaje kama mfumo mzima wa kutoa haki kwa wananchi waliowengi umekufa?
 
Kama ana haki alipwe. Pia serikali nayo iwadai wale wote waliokopeshwa na serikali mfano wanafunzi wote waliokwisha maliza chuo na walipewa mikopo na bodi.
 
Si mnataka haki za binadamu na demokrasia? mtu kakamatwa na madawa ya kulevya airport tena kayahifadhi kwenye rectum anapewa juice ya kuharisha anamwaga pipi kadhaa lakini utasikia tunafanya upelelezi ukikamilika atapelekwa mahakamani, huku nyuma mtu anaandaa namna ya kujitetea. wanasheria wanatuambia "somebody is not guilty until proved guilty and shall proved guilty in the court of justice" mimi si mwanasheria ila naamini nimeeleweka. Sasa kwa mtu aliyekamatwa na dope, bunduki na risasi bila kibali, pesa za moto nk kwanini wasinyongwe kama ilivyo Iran, Saudi Arabia, Syria na China? au akapelekwa jela moja kwa moja kuna haja gani ya kuanza kusikiliza kesi?

Kwa zombe askari wenzie walikiri kura jamaa alikua na mtandao wa majambazi na ndiye aliyeamuru wale mabwana wauawe na madini alichua yeye badala ya kifungo bila kesi au kungongwa ndiyo hayo sasa yanakuja na lazima alipwe kama akishinda kesi dhidi ya serikali. Cha msingi ni kuandamana kutaka sheria ya kumnyonga mtu pale anapopatikana na kosa la wizi, mauaji, rushwa na madawa ya kulevya. palepale amekutwa na pesa za moto au unga asomewe hukumu ya kunyonwa bila kujali ni ndugu yangu au ni nani itakua fundisho kwa wengine. Ukiandamana kupinga mtu kulipwa wakati mahakama yako imeshahukumu hivyo katika rufani zote itakua ngumu hata iwe ni chama gani kiko madarakani, njia ya kupinga hukumu ni kukata rufaa pekee na siyo tofauti ama la Zombe anyamazishwe kwa kuondolewa katika sura ya dunia.

Mzee maneno magumu haya hasa hapo kwenye red,je askari wakikubambikia kama wanavyofanya sasa hivi unakuwaje hapo?
 
lakini serikali ilikata rufaa kwenye kesi ya zombe baada ya kubwagwa. sasa atafunguaje kesi wakati rufaa haijaamuriwa?
 
lakini serikali ilikata rufaa kwenye kesi ya zombe baada ya kubwagwa. sasa atafunguaje kesi wakati rufaa haijaamuriwa?
Mkuu, sina uhakika kama walikata rufaa, ninachokumbuka mimi JK alisema wahajaridhika na hukumu ya mahakama kipindi ANAONGEA na wananchi kupitia runinga ya TBC1.
 
Huyu Zombe naye ajatulia: nani atakubali kumlipa hayo madai: kama alishindwa kuwekeza huko nyuma imekula kwake. Watanzania tuwe makini katika hili, tusikubari upuuzi wa Kifisadi.
 
Serikali haikuwa serious kabisa wakati wa hii kesi na ndio maana akashinda...yale yale ya kesi ya DOWANS
Sasa hivi anafungua kesi ya madai dhidi ya serikali hii hii na kwa uozo uliomo lazima atashinda tu!
Hii lazima ni dili na hiyo hela atakayoshinda hali peke yake....

Ama kweli bongo shamba la bibi!!!
 
Zombe ni jambazi na muuwaji,anatakiwa awe jela hivi sasa,anajua udhaifu wa serikali na sasa anaendeleza mchezo wa kutaka kuchezea kodi ya wananchi,anastahili kuwa lupango kwa mauwaji ya raia wasiokuwa na hatia.
 
Back
Top Bottom