Ziwa Nyasa ni milki halali ya Malawi

Sote tunajua kuwa Malawi wamesema ziwa Nyasa, ambalo kwa Malawi linaitwa Ziwa Malawi, ni mali yao na Tanzania haina hata tone moja la maji. Mazungumzo yanayoratibiwa na Tanzania yameshindwa kubadili msimamo wa Malawi. Malawi imejiandaa kwenda mahakamani ya kimataifa, ICJ, kutafuta suluhu ya kile wakisemacho. Uwezekano wa kushinda kesi ni mkubwa, tena mkubwa sana.

Malawi ina ushahidi wa kutosha kuhusu wasemalo: mkataba wa Heligoland 1890 kati ya Mjerumani na Mwingireza uliipa Uingereza (Malawi kwa sasa) ziwa lote. Mjerumani (Tanganyika/Tanzania) iliachiwa Heligoland na makoloni mengine Afrika ya Magharibi.

Kuna ushahidi wa kutosha pia kuwa waziri mkuu wa Tanzania, kwa wakati huo, Kawawa, aliwahi kutoa matamko Bungeni, mara nyingi tu, kuwa Tanganyika/Tanzania haina hata tone moja la maji katika ziwa Nyasa/Malawi. Kwa maneno mengine ziwa Nyasa au Ziwa Malawi ni mali ya Malawi.

Ni mhimu kujua kuwa maneno/matamko yanayotolewa na viongozi wa serikali ya nchi husika, kwa sheria za kimataifa, yanahesabiwa kuwa ni sera ya nchi na hivyo huibana nchi anakotoka kiongozi aliyetoa maneno/matamko hayo. Kwa wafuatiliaji wa mambo, angalia kesi zilizoamuliwa na mahakama ya mbalimbali za kimataifa hasa ICJ. Kuna kesi tatu mhimu kwenye hili: Tamko la Ihleni (Ihlen Declaration), kesi ya Peninsula ya Bakassi na Matamshi ya mwakilishi wa Marekani katika WTO. Kesi mbili za mwanzo ziliamuliwa na mahakama ya kimataifa ya ICJ.
(Pakua na Soma zaidi....liliandikwa siku nyingi)
Umeamkia kutoka kilabu gani leo hii ndugu yangu wakati swala hili bado linashughulikiwa na timu ya kimataifa ya arbitration na wala hawajatoa uamuzi wao? Kumbuka kuwa kuna sheria ya kimataifa iliyo wazi kabisa kuhusu definition ya mpaka unaohusu maji yalioko mipakani kuwa siku zote maji hayo yatagawanywa baina ya nchi mbili husika. Mipaka ya nchi haiwekwi kwa kingo za maziwa au mito; ama ziwa/mto wote pamoja na ardhi inayolizunguka iko chini ya nchi moja au nchi mbili zinagawana maji ya ziwa au mto huo. Angalia miaka ya nchi hizi ambazo ama iko kwenye maziwa au mitoni.

Canada- USA
Uruguay-Brazil
Uruguay-Argentina
Argentina-paraguay
Paraguay-Brazil
Bolivia-Peru
Estonia-urusi
Turkmenistan-Uzbekistani
Switzerland- Ufaransa


Iwapo wasipogawana maji hayo basi yanakuwa ni international waters kama ambavyo ilivyo Black sea. Mojawapo kati ya mifano michache ambapo maji yote karibua na mpaka huchukukiliwa na nchi yote ni pale maji hayo yanakuwa yamenzungwa na nchi hiyo kama ilivyo Ziwa Nicaragua mpakani mwa Nicaragua na Costa Rica, ziwa lote limezungukwa na Nicaragua ingawa liko mpakani.
 
Hivi wakisema ziwa ni la kwao mipaka imeishia wapi? Wakisema mwisho wa maji yalimoishia. Na maji ya ziwa au bahari yanatabia ya kupwa na kujaa. Je maji yakipwa mpaka utaishia wapi? na pia yakijaa watasema maji yanaishia wapi? Kwaiyo walioweka mipaka katikati ya maziwa hawakuwa wajinga hawa labda wanatafuta kiki au ugomvi na Tanzania yetu.
 
Hawa majirani zetu Malawi naona wanaombea Vita, Ushauri wangu kwa Viongozi wetu wasipuuzie hizi Choko Choko, tujiandae na kujipanga, Akuanzae ....
Malawi waambiwe kabisa sasa hivi Tanzania tupo Busy kujenga Tanzania Mpya, hatuna mpango wa wazo la Vita.
Hatuna haja ya kujua Mkoloni Mweupe alisema nini wala Viongozi wetu wa zamani walisema nini.
Sheria za Kimataifa zinazohusu Mipaka ya Nchi na Nchi zinasemaje.
Hivi lini mliwatangazia watanzania kua imezeeka sasa mbahitaji hiyo Tanzania mpya..mmeshindwa kusimamia maslahi ya wananchi kama Demokrasia, ajira kwa vijana na haki za binadamu ndio mnaweza ili la Ziwa Malawi
 
Mi naona wachukue ziwa lao tu hamna namna,hatuwezi g'ag'ania ziwa huku tuna ardhi ya kijani,kumbuka serikali ya Tanzania haina shamba sasa hayo maji ya nini?
 
Hivi lini mliwatangazia watanzania kua imezeeka sasa mbahitaji hiyo Tanzania mpya..mmeshindwa kusimamia maslahi ya wananchi kama Demokrasia, ajira kwa vijana na haki za binadamu ndio mnaweza ili la Ziwa Malawi

Boss, Kwanza naomba ni declare kuwa sina Upande wala Chama. Ukweli usiopingika, Tanzania na Wananchi tulikuwa tumefika mahali pabaya sana, iwapo Mambo yalikuwa yanaenda kwa kujuana na 10%. Sifurahishwi kabisa na baadhi ya Kauli na Matamko na Maagizo ya Ngosha.
 
Hivi wakisema ziwa ni la kwao mipaka imeishia wapi? Wakisema mwisho wa maji yalimoishia. Na maji ya ziwa au bahari yanatabia ya kupwa na kujaa. Je maji yakipwa mpaka utaishia wapi? na pia yakijaa watasema maji yanaishia wapi? Kwaiyo walioweka mipaka katikati ya maziwa hawakuwa wajinga hawa labda wanatafuta kiki au ugomvi na Tanzania yetu.
Wakisema hvyo ujue mbeya songwe songea na njombe ni sehemu za malawi.....iwapo wakishinda kesi
 
Lema tu anawatoa kamasi anawachukulia karibu sasa miaka miwiri kushinda kesi mahakamani munakimbilia ma court injunctions lCC mutasimama
Tuna discuss issue muhimu kwa maslahi ya nchi huu upuuzi wa nini tena?
 
JK alisha sema waende hata mbinguni mpaka upo katikati ya maji kwisha, na mimi nasema hivyo wakileta ubishi twachukua mpaka ardhi yetu tageuza mkoa.
 
Ningekuwa Mimi ndo rais, ningeshamuita balozi wetu kutoka Malawi kisha namfukuza wa kwao mapema. Then, nakaa kimya bila kunena chochote... Halafu naanzisha mradi mkubwa wa maji kutoka ziwa Nyasa kwa ajili ya watu wa songea na wilaya zake. Halafu tena naweka boat za kisasa za uvuvi huko ziwani na wanajeshi ndo wanafanya uvuvi. OVA
 
Kitendo cha Mjerumani kupigwa katika vita kuu ya kwanza ya dunia na kunyang'anywa makoloni yake ni Ushahidi kuwa Heligoland treaty ilifia hapohapo.
Laiti mkataba huo ungekuwa bado unaheshimiwa hata baada ya vita kuu ya kwanza basi, Mjerumani angerudishiwa makoloni yake yote yaliyoko katika mkataba huo.
Kitendo cha Muingereza kuichukua Tanganyika, Rwanda na Burundi kwenda kwa Mbelgiji Automatically kunaivunja hiyo Helligoland treaty na Mwingereza alikuwa hayuko bounded kufuata chochote katika mkataba huo baada ya hapo!.
Treaty ya kufuatwa hivi sasa ni International law juu ya maji ya mpakani!
Nataka kujuzwa jambo Moja:

1.Kabla ya Hao wakoloni kuja, ziwa lilikuwa Mali ya nani?

2. Hiyo mikataba sijui Heligoland na uchafu mwingine, inaheshimiwa kwa sababu zipi? Je, ni kusema kwamba uvamizi wao ulipata vibali mahali Fulani kiasi cha wao kutupangia matumizi ya rasimali zetu na kuamua mipaka yake?
 
Boss, Kwanza naomba ni declare kuwa sina Upande wala Chama. Ukweli usiopingika, Tanzania na Wananchi tulikuwa tumefika mahali pabaya sana, iwapo Mambo yalikuwa yanaenda kwa kujuana na 10%. Sifurahishwi kabisa na baadhi ya Kauli na Matamko na Maagizo ya Ngosha.
Safi sanaa wa brash wote wavicha vya panya ....Shigogo analia2 wamemufilisi nakumtupa.
 
Mito yote inayoingia Ziwani inatoka Tanzania. Tuweza kuikausha kiana. Ni kuanzisha irrigation schemes za kufa mtu kutoa maji mto Songwe, Lufilyo na Mbaka.
Malawi waangalie upande wa pili
Tatizo sio malawi ni wakoloni waliohalalisha ziwa liwe lao na OAU ikabariki.
 
Stop that rubbish. Uganda ilishindwa kwa sababu every Ugandan was against Amin kwa udikiteita wake na mauaji ya waganda- kila mmoja aliguswa na ukatili wa Amin. Watanzania walisaidiwa sana na waganda kumsaliti Idd amin otherwise the story could have been different!
Kumbe hata wewe ni mfua gagulo za wazungu!
 
Ni kweli nyie wamalawi hamuwezi kushinda, ziwa ni nusu kwa nusu kama mlivyo gawa katikati na Mozambique, pia mbali na international law pia ziwa lina tabia ya kuhama hama kwahiyo mpaka nao utakuwa unahama? ?
Nani aliegawa?
 
Kama tatizo ni wakoloni, Malawi wanapata wapi jeuri ya kusema watalitumia peke yao?
Tz itamwaga meli tuone kama watazuia.
Malawi wanafuata ramani waliyorithi kutoka kwa wakoloni ambayo imebarikiwa na OAU ndio maana nimeandika tatizo sio la malawi sab waliochora ramani ni wakoloni na nchi zote za afrika zikakubalia kwa kutia saini makubaliano kwamba wakubali mipaka ya kikoloni sasa wamalawi kosa lao liko wapi?
 
Malawi wanafuata ramani waliyorithi kutoka kwa wakoloni ambayo imebarikiwa na OAU ndio maana nimeandika tatizo sio la malawi sab waliochora ramani ni wakoloni na nchi zote za afrika zikakubalia kwa kutia saini makubaliano kwamba wakubali mipaka ya kikoloni sasa wamalawi kosa lao liko wapi?

Siku zote mpaka umekuwa nusu kwa nusu.

Kamuzu Banda na jeuri yake yote akisaidiwa na makaburu alikubali ukweli huo. Matumizi "de facto" ya ziwa siku zote yamekuwa hivyo.

Sasa limezuka la upatikanaji wa mafuta ziwani na ghafla Malawi wameona mwanga. Huo mkataba naujua fika lakini ukweli utabaki pale pale kwamba tutalitumia wote. Wasuluhishi wa SADC walijaribu kuwaambia Malawi wakubali hali halisi lakini hawataki

Liwalo litakuwa lakini Tz itaendelea kulitumia kama zamani
 
Back
Top Bottom