Ziwa Nyasa ni milki halali ya Malawi

Ziwa Nyasa ni milki halali ya Malawi

Siku zote mpaka umekuwa nusu kwa nusu.

Kamuzu Banda na jeuri yake yote akisaidiwa na makaburu alikubali ukweli huo. Matumizi "de facto" ya ziwa siku zote yamekuwa hivyo.

Sasa limezuka la upatikanaji wa mafuta ziwani na ghafla Malawi wameona mwanga. Huo mkataba naujua fika lakini ukweli utabaki pale pale kwamba tutalitumia wote. Wasuluhishi wa SADC walijaribu kuwaambia Malawi wakubali hali halisi lakini hawataki

Liwalo litakuwa lakini Tz itaendelea kulitumia kama zamani
Hawataki kwa sab wanafuata mkataba unavyosema na kawaida ya migogoro kama ikishindikana kusuluishika hufikishwa kwenye mahakama za kimataifa ambako inawezekana wakashinda au tukashinda.
 
Barbarosa, nakuhakikishia-....hatushindi. Soma article yangu/research hii hapa!
MBONA UMEONGEA KAMA ULIYETUMWA VILE. NA UNAONEKANA NI KITU KITAKUFURAHISHA KAMA HILO ZIWA LISIPOKUWA LA TZ. WA TZ TUNA CHANGAMOTO YA KITU KINAITWA UZALENDO. SINA MAANA TUMUONEE MTU ILA HUWEZI KUFURAHIA MAMA YAKO AKIPIGWA MAKOFI NA POLISI ETI KISA KAIBA UNLESS UWE NA TATIZO KICHWANI.
 
Sio issue ya msingi tena hiyo.sheria za kimataifa zinasema zenyewe water bodies zikiwa zipo kati ya nchi ya mbili then wamilki ni wote wawili wakuna mjadala.
 
Boss, Kwanza naomba ni declare kuwa sina Upande wala Chama. Ukweli usiopingika, Tanzania na Wananchi tulikuwa tumefika mahali pabaya sana, iwapo Mambo yalikuwa yanaenda kwa kujuana na 10%. Sifurahishwi kabisa na baadhi ya Kauli na Matamko na Maagizo ya Ngosha.
Mkuu naona unapoteza kabisa sifa za kua kwenye jukwaa ili...
Nikuelimishe kidogo tu..Hakuna serikali au utawala wowote unaoweza kufanya kazi na watu ambao hawawajui kwahiyo kujuana katika nafasi za juu hakukwepeki ndio maana ata Pombe alimteua mtu aliyesimamia PhD yake ambayo mpaka leo inamashaka.
Pili hivi kuna RC,D.C.,RAS, DAS,MD etc ambao wameteuliwa bila kua maswahiba wa viongozi au CCM? Msitake kumpaka Kikwete uchafu leo wakati nyuma hamkuweza kukosoa bali mlikua mnashangilia na kumlinda kama mnavyofanya kwa huyu...huu ni unafiki wa hali ya juu...Hivi unataka kuniambia Kikwete alikua anatoa ajira za ualimu, madaktari etc kwa kujuana? Pole yako kwakua mnafiki maana ni sifa ya kuendelea kua mwanacccm
 
Chukueni muda mkajisomee kuhusu International Law of the Sea pamoja na international Law of the Internal Water zaidi article 8 nadhani tunaweza kujadiri vizuri alafu twende kwenye recognition of former treaties e.g. Bilateral Treaties tunaweza kupata mwanga kuhusu ili jipu
 
Barbarosa, nakuhakikishia-....hatushindi. Soma article yangu/research hii hapa!

nakumbuka hotuba ya jk wakati mgogoro huu unafukuta kipindi chake, alisema mipaka yoote ya maziwa na mito iliwekwa katikati yake baina ya nchi na nchi, kasolo ziwa nyasa tu ndio mpaka wake uliachwa pembeni mwa ziwa, na ziwa hilo likabaki kuwa ni mali ya malawi.
kwa mawazo yangu nimehisi kwamba, kama ziwa hili limeachwa lote kua ni mali ya malawi, basi hata huo mpaka wa kati ya tanzania na malawi haupo kaupo pembeni mwa ziwa kama tunavyofikikili, labda utakua ndani zaidi mwa nchi ya tanzania, na labda viongozi wa kipindi hicho wa tz walijua umuhimu wa ardhi na wamefosi kuteka pande la ardhi hadi kwenye pwani ya ziwa. haya ni mawazo tu, lakini nakumbuka kulitokea ugonvi kama huu kwenye nchi za africa.ni nchi ya chard kama sijakose. lakini mwisho wa siku walipoenda mbele zaidi,mpaka uliwekwa katikati.
wamalawi hapa watashikilia kile kipengele cha umoja wa Africa kua, KILA NCHI ITAENDELEA KUHESHIMU MIPAKA ILIO'ACHWA NA WAKOLON BAINA YA NCHI NA NCHI."
kwahiyo wakijidanganya na UN ziwa litakatwa katikati.
LA
 
Mwaka 1922 Waingereza kwa kuwa wao ndo walikuwa washindi wa vita ya kwanza ya dunia waliuhamisha mpaka kutoka ukingoni mwa Ziwa na kuurudisha katikati ya ziwa!. Kisheria Walikuwa na haki ya kufanya hivyo kwa sababu wao hawakuwa bound na mkataba wa Helligoland baina yao na Mjerumani, Mjerumani alinyang'anywa makoloni yake!

Kwa hiyo kuanzia hapo Tanganyika mpya ikawa na mpaka katikati ya Ziwa.

Miaka michache kabla ya Uhuru Muingereza yuleyule akahamisha mpaka tena kutoka katikati ya ziwa na kuurudisha Ukingoni. Hii sasa kisheria ni kosa kwa sababu Tanganyika ya baada ya vita kuu ya pili ya dunia ni tofauti kabisa na Tanganyika ya mwaka 1922, Tanganyika ya mwaka baada ya Uhuru ilikuwa Chini ya Uangalizi tu wa Muingereza kwa mujibu wa UN hivyo Muingereza hakuwa na powers za kubadiri mipaka yake!. Ila Tanganyika ya mwaka 1922 Muingereza alikuwa na powers za kubadiri mipaka kwa sababu hakukuwa na sheria ya kimataifa ya kumzuia!

Kwa hivyo basi mpaka unaohold na tunaoutambua sisi ni wa mwaka 1922, Siyo huo wa Helligoland treaty iliyokufa kifo cha Mende baada ya Mjerumani kuchakazwa na kunyanganywa makoloni yake yote aliyopewa kwenye hiyo Helligonda treaty!
 
Huyo mwingereza anayewalisha ujinga hatakuwepo tutakapowafanyia kitu mbaya, ngoja wajilengeshe waingie kwenye 18 zetu.
 
Hii kesi ni ngumu ingawa wakati mwingine tuamue tu kutumia maji yote ya mito ilishasho hilo ziwa. Tuna maeneo mengi tuya divert tutengeneze dam kubwa waendelee na korongo lao kubwaaa. Kwani lile ziwa kwa kiasi kikibwa sisi tunalilisha maji kwa mito tuitunzayo.
 
Safi sanaa wa brash wote wavicha vya panya ....Shigogo analia2 wamemufilisi nakumtupa.

Asante sana Boss,
Tatizo lao, wanafikiri Mtu uki support kitu upo Chama Cha Mapinduzi na ukikosoa na kutoa ushauri upo Chadema au Chama Chochote cha Upinzani kingine.
 
Hii kesi ni ngumu ingawa wakati mwingine tuamue tu kutumia maji yote ya mito ilishasho hilo ziwa. Tuna maeneo mengi tuya divert tutengeneze dam kubwa waendelee na korongo lao kubwaaa. Kwani lile ziwa kwa kiasi kikibwa sisi tunalilisha maji kwa mito tuitunzayo.
Kabla ya ilo kwanza tuanze kutumia mito kama Kagera,Ruaha na Ruvu kwenye kilimo cha umuagiliaji maana njaa itawaua watu asa Misenyi,Tabora na Geita
 
Tanzania bado sana, tuna Safari ndefu.
Kwanza kabisa sijamtaja Rais Mstaafu Kikwete popote, Usinilishe maneno. Tanzania sasa hivi tuna Rais wa Tano. Pili nilivyosema neno Kujuana sikumaanisha kama ulivyolielezea wewe. Kujuana niliousemea mimi, ni Urasimu kwenye kupata Haki za msingi za Raia kama Kazi, Huduma za Jamii na menginiyo. Hapa kuna mifano hai mingi tu, sina muda wa kuitolea.



Mkuu naona unapoteza kabisa sifa za kua kwenye jukwaa ili...
Nikuelimishe kidogo tu..Hakuna serikali au utawala wowote unaoweza kufanya kazi na watu ambao hawawajui kwahiyo kujuana katika nafasi za juu hakukwepeki ndio maana ata Pombe alimteua mtu aliyesimamia PhD yake ambayo mpaka leo inamashaka.
Pili hivi kuna RC,D.C.,RAS, DAS,MD etc ambao wameteuliwa bila kua maswahiba wa viongozi au CCM? Msitake kumpaka Kikwete uchafu leo wakati nyuma hamkuweza kukosoa bali mlikua mnashangilia na kumlinda kama mnavyofanya kwa huyu...huu ni unafiki wa hali ya juu...Hivi unataka kuniambia Kikwete alikua anatoa ajira za ualimu, madaktari etc kwa kujuana? Pole yako kwakua mnafiki maana ni sifa ya kuendelea kua mwanacccm
 
Article imekaa kiuoga uoga dah ... tena kwa kutoa mifano ya mikataba ya kikoloni na kizungu. Kwa taarifa yako, hakuna hata sentimita moja hao wa-nyasa wako tutawapa na kwa kusema hivyo naelewa unafahamu migogoro kama hiyo huishaje! Wasituletee janja ya nyani, watalalamika na kulia kote watakakoweza ... si yetu ni sheria tu ya kimataifa zaidi ya hapo wafanye wanachoweza waone.

Mi kwetu kwa asili ni Machame ila ikibidi sitaona shida kuhamishia makazi yangu Matema Beach kuilinda Tanganyika yetu.

Sitegemei article ya kinyonge namna hiyo kutoka kwa wanaume kama wa Israel, Palestine, Sudan, India, Pakistan n.k., tatizo la wanaume wengi wa bongo tumekuwa walegevu legevu sana. Hii nchi ni yetu na ukihitajika (kwa mujibu wa sheria), jiandae kwenda kuilinda chi yako kama wanaume wengine ....
 
Asante sana Boss,
Tatizo lao, wanafikiri Mtu uki support kitu upo Chama Cha Mapinduzi na ukikosoa na kutoa ushauri upo Chadema au Chama Chochote cha Upinzani kingine.
Ni mijinga2 wataki freedom of opinion wajiona wajuwaji kumbe vilaza2
 
Dawa ya mtukutu ni kumpiga tu. Kama anaweza kushitaki na kushinda sisi ni kumpiga tu
 
Hatuwezi kushindwa tukiwapeleka Lissu na Kibatala tunashindwaje?
 
Barbarosa, nakuhakikishia-....hatushindi. Soma article yangu/research hii hapa!
Sheria ya hizi mambo za mito,maziwa na bahari vinapokuwa ktk mpaka lazma wagawe nusu kwa nusu Jk alieleza vzur kwenye hotuba yake kuhusu mgogoro wa malawi na tz kuhusu ziwa nyasa .
 
Back
Top Bottom