Ziwa Nyasa ni milki halali ya Malawi

Ziwa Nyasa ni milki halali ya Malawi

We Mnyasa upuuzi huu kausemee ukiwa upande wa pili wa Ziwa Nyasa kule kwenu sio huku
 
Mimi sumo kwanza akuna kinachonisaidia katika ilo ziwa. Kwanza hata samakiwenyewe ninakula wa kichina
 
Hii ni mpaka kiama. Hakuna cha ICJ wala nini. Ni kama South China Sea. Uzuri Tanzania sio member wa ICJ. Asante Nyerere kwa kuotea hilo
 
Naona mnamjaribu homeboy, tutalihamisha ziwa lote tulipeleke Chatle.....acha wajipendekeze kwa homeboy. Tutawamiliki wao na ziwa Nyasa [HASHTAG]#BringbackZiwaNyasaFully[/HASHTAG]
 
hapo naona hata wilaya ya nyasa iko mbion kuhamia huko malawi kwan weng wao wanaongea wanaongea kimalaw na wanapenda maisha ya malaw kuliko huku kwa sizonje! banda komaa 2we wananch wa malawi.
 
Hapa wazungu washatamani mafuta na gas yetu, wanachochea migogoro ili tupigane waje kuchukua kirahisi.

Nawe mleta mada urudi kwenu Malawi utuachie nchi yetu.
 
Kama umetumwa nenda kawaambie tunasema, wacha ziwa tu, tutaichukuwa Malawi yote iwe himaya ya Tanzania na kama mnabisha mwende mkawaulize Uganda.
Hii mikataba ya kina sultan mangungo wa msovero na Karl Peters bado inatambulika ? haina tofauti na ule wa kutokutumia maji ya mto nile huyu bwana sijui lengo lake nini ?
 
Naona mnamjaribu homeboy, tutalihamisha ziwa lote tulipeleke Chatle.....acha wajipendekeze kwa homeboy. Tutawamiliki wao na ziwa Nyasa [HASHTAG]#BringbackZiwaNyasaFully[/HASHTAG]

Shida kua na feeling Tz its most powerful country....jua vita kwasasa ni (interests ) munaona vita ya countries kama mabodia wapo ring manup.
 
Kua munatembea kuna wa Bongo kibao Mozambique, Zambia,Malawi n.k atlarge ....respect freedom of expression archaic people nyie
Kua mtulivu basi, ndugu zenu tunao hapa kwa maelfu! Binafsi nawafahamu wengi tu! Sidhani kama ni busara sana kutumia lugha mnayotumia?? Halafu wale ndugu zetu mliowakamata muwaachie bila masharti yoyote!
 
Uingereza ni kisiwa tu, lakini alitawala dunia! Unajua kwanini?? Muingereza ndio baba na mama wa fitna dunia hii!

Uzuri wa Waingereza, pamoja na kufanya fitina na maovu yote wametengeneza Upande mwingine wa jamii yao ambao umeshamirisha "Ubinaadamu" yaani Haki.
Hata leo kama kuna mtu ameonewa sehemu yoyote ile duniani, anaweza kwenda huko huko Uingereza na kupata haki yake. Ni jambo ambalo ni shida kupata sehemu nyingi duniani haswa katika nchi nyingi zetu hapa Afrika.
 
Mito yote inayoingia Ziwani inatoka Tanzania. Tuweza kuikausha kiana. Ni kuanzisha irrigation schemes za kufa mtu kutoa maji mto Songwe, Lufilyo na Mbaka.
Malawi waangalie upande wa pili

Halafu ziwa likikauka tunachukua ardhi! Bahati mbaya pombe hajui international pilitics wal diplomacy. Tutapiga tu!
 
Waachie tu maana hata mlima ule mlefu unatushinda mpaka majirn nao wanaotangaza ulaya kuwa wao sasa mshikaa mawili moja humponyoka tukomae na tunachoweza
Hembu mnisaidie nasikia mlima ulikuwa wa jirani sasa enzi hizo sie tulikuwa na bahari kuanzia Tanga mpaka ile ya mombasa ilikuwa yetu ikabidi wakae wazee wakombozi wa hizi nchi mbili ikabidi wa kwetu ampe kipande cha bahari kinachoitwa mombasa kwa sasa na sie wakatupa mlima hii maneno iko na ukweli ndani yake ? Nauliza tu nipate kujua manake wengine vitukuu humu
Hivi siku zote hizo mbona hiyo nyonyo ilikuwa haisumbui?Wamepatwa na nini?Hiyo nyonyo itabakia kama ilivyokuwa siku zote wasilete mchezo.[HASHTAG]#Hatupendagi[/HASHTAG] ujinga sisi#
 
Kama siyo Waingereza Malawi ilipaswa kuwa mojawapo ya mkoa wa Tanzania. Ungekuta leo mkuu wa Mkoa wa Malawi Mh Paul Makonda.. wilaya ya Lilongwe yupo Ally Hapi etc
 
Halafu ziwa likikauka tunachukua ardhi! Bahati mbaya pombe hajui international pilitics wal diplomacy. Tutapiga tu!
Kama munauwezo wakuwadhibiti wapinzan kutumia maji washa, kuwasweka rumande bila sababu n.k siju mbinu zenu mutafanikiwa hata kuisubulu inchi nzima.
 
Hembu mnisaidie nasikia mlima ulikuwa wa jirani sasa enzi hizo sie tulikuwa na bahari kuanzia Tanga mpaka ile ya mombasa ilikuwa yetu ikabidi wakae wazee wakombozi wa hizi nchi mbili ikabidi wa kwetu ampe kipande cha bahari kinachoitwa mombasa kwa sasa na sie wakatupa mlima hii maneno iko na ukweli ndani yake ? Nauliza tu nipate kujua manake wengine vitukuu humu
Mhh wataongea mengi ila bahari ni yetu na mlima ni wetu.Bye bye Kenya.
 
Malawi kama malawi haina ubavu wa kupambana na Tanzania ila hii chokochoko yao ni kutokana na uhakika wa nguvu kubwa kijeshi na silaha ambazo watapewa endapo Tanzania tutateki action sasa wanasalama wetu fanyeni kazi wa kuifokonyoa Malawi
 
Nimesikia kuna mafuta wa Waingereza ndiyo shinikizo usiniulize source.
Wallah nimewahi kuona watu wanafiki lakini hawa watu weupe ni wanafiki mpaka shetani anawaogopa watakuchekea mpaka jino la mwisho huku wakiwasha moto kwa mlango wa nyuma pumzika kwa amani Gadafi, na Mungu akujaalie maisha marefu Rais Robert Mugabe Mungu mpe afya njema Rais wetu baki hapa hapa tusukume gurudumu la maendeleo mwenye shida aje tu hapa tuzungumze.
 
Hawa majirani zetu Malawi naona wanaombea Vita, Ushauri wangu kwa Viongozi wetu wasipuuzie hizi Choko Choko, tujiandae na kujipanga, Akuanzae ....
Malawi waambiwe kabisa sasa hivi Tanzania tupo Busy kujenga Tanzania Mpya, hatuna mpango wa wazo la Vita.
Hatuna haja ya kujua Mkoloni Mweupe alisema nini wala Viongozi wetu wa zamani walisema nini.
Sheria za Kimataifa zinazohusu Mipaka ya Nchi na Nchi zinasemaje.


Sote tunajua kuwa Malawi wamesema ziwa Nyasa, ambalo kwa Malawi linaitwa Ziwa Malawi, ni mali yao na Tanzania haina hata tone moja la maji. Mazungumzo yanayoratibiwa na Tanzania yameshindwa kubadili msimamo wa Malawi. Malawi imejiandaa kwenda mahakamani ya kimataifa, ICJ, kutafuta suluhu ya kile wakisemacho. Uwezekano wa kushinda kesi ni mkubwa, tena mkubwa sana.

Malawi ina ushahidi wa kutosha kuhusu wasemalo: mkataba wa Heligoland 1890 kati ya Mjerumani na Mwingireza uliipa Uingereza (Malawi kwa sasa) ziwa lote. Mjerumani (Tanganyika/Tanzania) iliachiwa Heligoland na makoloni mengine Afrika ya Magharibi.

Kuna ushahidi wa kutosha pia kuwa waziri mkuu wa Tanzania, kwa wakati huo, Kawawa, aliwahi kutoa matamko Bungeni, mara nyingi tu, kuwa Tanganyika/Tanzania haina hata tone moja la maji katika ziwa Nyasa/Malawi. Kwa maneno mengine ziwa Nyasa au Ziwa Malawi ni mali ya Malawi.

Ni mhimu kujua kuwa maneno/matamko yanayotolewa na viongozi wa serikali ya nchi husika, kwa sheria za kimataifa, yanahesabiwa kuwa ni sera ya nchi na hivyo huibana nchi anakotoka kiongozi aliyetoa maneno/matamko hayo. Kwa wafuatiliaji wa mambo, angalia kesi zilizoamuliwa na mahakama ya mbalimbali za kimataifa hasa ICJ. Kuna kesi tatu mhimu kwenye hili: Tamko la Ihleni (Ihlen Declaration), kesi ya Peninsula ya Bakassi na Matamshi ya mwakilishi wa Marekani katika WTO. Kesi mbili za mwanzo ziliamuliwa na mahakama ya kimataifa ya ICJ.
(Pakua na Soma zaidi....liliandikwa siku nyingi)
 
Back
Top Bottom