Sote tunajua kuwa Malawi wamesema ziwa Nyasa, ambalo kwa Malawi linaitwa Ziwa Malawi, ni mali yao na Tanzania haina hata tone moja la maji. Mazungumzo yanayoratibiwa na Tanzania yameshindwa kubadili msimamo wa Malawi. Malawi imejiandaa kwenda mahakamani ya kimataifa, ICJ, kutafuta suluhu ya kile wakisemacho. Uwezekano wa kushinda kesi ni mkubwa, tena mkubwa sana.
Malawi ina ushahidi wa kutosha kuhusu wasemalo: mkataba wa Heligoland 1890 kati ya Mjerumani na Mwingireza uliipa Uingereza (Malawi kwa sasa) ziwa lote. Mjerumani (Tanganyika/Tanzania) iliachiwa Heligoland na makoloni mengine Afrika ya Magharibi.
Kuna ushahidi wa kutosha pia kuwa waziri mkuu wa Tanzania, kwa wakati huo, Kawawa, aliwahi kutoa matamko Bungeni, mara nyingi tu, kuwa Tanganyika/Tanzania haina hata tone moja la maji katika ziwa Nyasa/Malawi. Kwa maneno mengine ziwa Nyasa au Ziwa Malawi ni mali ya Malawi.
Ni mhimu kujua kuwa maneno/matamko yanayotolewa na viongozi wa serikali ya nchi husika, kwa sheria za kimataifa, yanahesabiwa kuwa ni sera ya nchi na hivyo huibana nchi anakotoka kiongozi aliyetoa maneno/matamko hayo. Kwa wafuatiliaji wa mambo, angalia kesi zilizoamuliwa na mahakama ya mbalimbali za kimataifa hasa ICJ. Kuna kesi tatu mhimu kwenye hili: Tamko la Ihleni (Ihlen Declaration), kesi ya Peninsula ya Bakassi na Matamshi ya mwakilishi wa Marekani katika WTO. Kesi mbili za mwanzo ziliamuliwa na mahakama ya kimataifa ya ICJ.
(Pakua na Soma zaidi....liliandikwa siku nyingi)
Kaka unajichanganya kama Wamalawi wenzio, habari za maziwa yaliyopo mpakani ilikuwa hivi,
1: Miaka ya mwanzo ya Ukoloni, Maziwa yote yaliyopo mpakani hayakuwa ya mtu yalikuwa huru kwa kila nchi zilizo mpakani kuyatumia, ukiangalia ramani zote za mwanzo Maziwa hayakuwa na Mipaka
2: Baadae hao wakoloni waliamua kugawana nchi kwa uhalali na pia kuweka Mipaka kwenye hayo Maziwa
3: Tanganyika likawa chini ya German East Africa (Tanganyika) na Belgium Congo, lake Nyasa lote likawa chini ya British (Malawi)
4: Baada ya kushindwa vita, Waingereza wakapewa Tanganyika, so Wakawa wanatawala, Kenya, Uganda, Tanganyika, Malawi, Zambia na Zimbabwe
5: Uingereza kama ndio Baba wa Malawi na Tanzania kwa maana ya nchi zote ni zake akaweka mipaka mipya ya nchi hizo, ukiangalia Gazete na ripoti zote za makoloni ya Uingereza alikuwa anaielezea Tanganyika kwa mipaka yake kama ilivyo sasa, na Waingereza walifanya hivyo kwa kupeleka ramani na maelezo umoja wa mataifa kwenye miaka ya 1920, na Bunge la Uingereza walionyeshwa hiyomTanganyika walioichukua kutoka kwa Ujerumani iko wapi na ina mipaka gani
6: Miaka ya mwishoni ya 1950, Nyerere alienda UNO kudai uhuru wa Tanganyika, na Waingereza waliielezea UNO hiyo Tanganyika iko wapi na Mipaka yake ni ipi?
7: Mwaka 1961 Tanganyika ikapata uhuru na Waingereza ambao ndio Mabwana zetu (Tanganyika na Malawi) wakatoa hati ya Uhuru wa Tanganyika yenye Mipaka iliyopo sasa, yenye kuonyesha mstari unaopita katikati ya Ziwa Nyasa
VITU VYA KUVIJUA
1: Mkataba wa Holigan ulikuwa kati ya Waingereza na Wajerumani
8: Baada ya Ujerumani kushindwa vita, huo mkataba wa Holigan ukafa automatically kwani nchi zote zikawa chini ya mtu mmoja nae akauvunja physically kwa kuweka mipaka mipya
Waingereza walivyokuwa waroho wa rasilimali wangeshafanya yao ili kuinyanganya Tanzania haki ya Ziwa, wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu wao wenyewe walishaweka mipaka mipya ya Tanganyika na Malawi
Cc:
Barbarosa