Mangaline
JF-Expert Member
- May 19, 2012
- 1,045
- 221
Mkuu "Magindu" Kwanza kabisa, nakugongea "LIKE". Naungana na wewe 100%, na naendelea kulaani wote ambao wanaendelea kuhukumu, kabla ya uthibitisho. Hii inaonesha dhahiri kuwa ipo nia ya ndani ya chuki binafsi kwa kamanda Mpiganaji ambaye amekuwa akihatarisha hata maisha yake kupigania haki, usawa na utu wa watanganyika walio wengi, ambao kwa njia moja au nyingine, wameshindwa au hawawezi kupaza sauti zao kutetea utu wao. Wengi wa hao vibwetere wana utashi wao binafsi na wanaingiwa nyongo kwa kamanda huyo kutangaza nia yake ya kikatiba ya kugombea uraisi. Kama hoja yao ni hiyo, basi washindwe na walegee. na Iwapo, chama hicho kitaendelea na chuki za namna hiyo, Nipo tayari kumshawishi kamanda, ahame chama hicho, na kwa gharama yoyote, tuko tayari kushawishi umma, kuunga mkono mageuzi ndani ya chama kipya. Ila, Iwapo, na Ikiwa, Mkuu atakutwa na kashfa ya kula rushwa, nita withdraw statement yangu. "MUNGU ATUHURUMIE"
... yawezekana mengine mengi nimeyasahau. kuna kila sababu ya huyu jamaa kuundiwa mazengwe mbalimbali ili kuondoa credibility yake.
imefahamika pia wapinzani wake wa ndani ya chama chake wameanzisha kikundi maalumu walichokipa jina na OPERESHENI CHAFUA ZITTO..
kwa hayo machache nawatakia mjadala mwema wakuu.
narudia tena:- zitto ni maporomoko ya nile hayazuiliki kwa kifusi.
"MUNGU IBARIKI TANGANYIKA, MUNGU IBARIKI ZANZIBARI, RIP TANZANIA"