Binafsi nitafurahi kama jambo hili la Escrow litashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi.
Kinachokera hivi sasa ni kutafuta umaarufu wa kisiasa. Kwamba baada ya Zitto kugaragazwa vibaya kisiasa na Chadema kiasi cha kuishi ubungeni kwa msaada wa mahakama na kupoteza mashabiki wengi aliokuwa nao, sasa anataka kuwa-retain waliobaki na kupata popularity upya kupitia matukio.
Wakati Zitto ana deni letu la majina ya walioficha fedha uswisi, anakuja na mbwembwe za kutishiwa maisha bila ushahidi.
Fedha za uswis sisi hatukumtuma aziseme. Ni yeye mwenyewe aliyesema anajua majina ya watu walioficha hizo fedha huko. Akafanya safari mbili tatu akapotea kimyaa lakini ilikuwa ni baada ya mbwembwe kama hizi. Maana ilikuwa kila siku ni Zitto na fedha za uswisi. Ikaja tena hekaya kama ya leo kuwa kutokana na fedha ya uswis kubumbuliwa na yeye eti wanataka kumuua. Fedha za uswis hazijaja na majina hatujayapata na kwenye tume ya Werema Zitto kakanusha kuyajua majina.
Hili la Escrow ni dana dana nyingine ya 'nitoke vipi' Ni mwendelezo ule ule wa Zitto kutaka kujiinua tena kwa visibgizio na mbinu za kizamani tena bila ushahidi.
Asubihi leo, zimepandishwa threads tatu za kumsifia Zitto toka kwa mtu mmoja. Thread zenyewe ukiziona ni kama takataka tu lakini kwakuwa ni mkakati maalum zikaanzishwa. Mara eti Zitto ni Mbunge bora wa November. Wapi walianza kutoa hizo tuzo? Kama Zitto ni mbunge bora wa November, wa February ni nani? Mbunge bora kwa Parameters zipi? Zimekubaliwa na nani hizo parameters hadi tukubali Zitto ni mbunge bora wa November? Wenye akili tulipoona thread zinazomsifia Zitto zimeanzishwa tukajua tu kuna kitu kitaibuliwa.
Sasa Zitto amekuja na hadithi njoo utamu kolea. Sisi hatutaki kujua nani katishiwa nani hajatishiwa. Tunataka fedha za Escrow zirudi kwa watanzania wanaokosa dawa, wanaochangishwa michango ya kishenzi ilhali fedha ipo mifukoni mwa wajanja. Hii move pamoja na Kafulila Mnyika aliwahi kuishikia bango. Sasa PAC mnayo, fanyeni kazi zenu mje na matokeo acheni longolongo kama za fedha za uswis. Na mkome kutaka kupata umaarufu binafsi kwenye ishu yenye national interest.
kaka taratibu issue ya uswis kulikuwa na mizengwe mingi hata hao wazungu hawakuwa tayari sana kusaidia ila ili kwakuwa lipo hapa hapa bongo lazima liende na watu tuweni kitu kimoja jambo hili linaweza kulimaliza hili zimwi linalotumaliza
Haujajibu tuhuma hata moja hspo,unapiga kelele tu na unadhihirisha u shalo wako.
Kwanza kwa nini unamjibia huyo ceo wa shell? kwamba sio aliyevujisha mkataba wa statoil balu ni waandishi wa habari?
Na unaizungumzia shell, wewe kana nani shell?
Nilitegemea kama umekuja hapa kujibu tuhuma ujibu tuhuma zako.
Kwa mfano,ungeeleza kwamba matibabu ya marehemu mama yako uliyagharamia kwa pesa zako mwenyewe n.k na haujawahi kuomba pesa directly au in directly kutoka PAP. Na sio kutishia watu na vyombo vya dola.
PAP wanalipwa milioni 400 kila siku, wazalishe umeme wasizalishe.
Utaifa gani kaweka hapo?Bravo Zitto! Naona wengine wanachangia kichama zaidi badala ya taifa.
Sizungumzii report mimi,nazungumzia haya aliyoandika hapa.Wewe ni mtu wa ajabu sana na report itakapo toka utaumbuka! Unaendeshwa na hisia za kichadema na kibavicha kwenye kila jambo! Hauwezi kupambana na Zitto kwa nhoja za kitoto namna hii!
Na kuhakikishia Sangarara mtaumbuka kama mnafukiri Zitto ataingia kwenye mtego wenu! Tarehe 27 si mbali!
Zitto kabwe,
kwanza umefanya vema kujitokeza kujibu tuhuma zinazokukabili lakini unaonekana kutumia akili pana sana kujibu tuhuma zako hasa kwa kutumia maneno ya kulaghai badala ya kumibu hoja asilia,ninashaka na maneno yako hasa kwenye maeneo haya,
kwanza,umesema kampuni ya shell haifanyi biashara hivi kunakampuni ambayo inaweza kuanzishwa siyo kufanya biashara? Kama haifanyi biashara inafanya kazi gani sasa.
Pili utakumbuka kwenye tuhuma zako unatuhumiwa kuazimwa au kukopeshwa kiasi cha milioni sita na kampuni moja wapo hapa nchini pesa hiyo ilitumika kwenda kumtibia mama yako kwanini hujasema hiyo pesa ulipewa kwa makubaliano gani au ulipewa kama msaada au kama mikopo mingine ili urudishe.
suala lako la kupewa hela na ubarozi wa uingeleza siyo jipya hata wakili wako ambaye sote tunamjua anayetokea mkoa wa kaskazini unamtumia sana kwenda kuchukua pesa zako za madili kutoka kwenye makampuni kadhaa unachofanya pesa nyingi huchukui wewe unatuma watu kwaniaba yako.
zipo sehemu mbili ambazo wakili wako amechukua pesa kwa maelekezo yako na amesainishwa siku moja hiyo document utawekewa hapa ila mnamuaibisha sana wakili wako japo hapendi unavyofanya lakini wewe unasema huwezi kuacha kuwasaidia waingeleza umetoka nao mbali.
jambo lingine ni wewe kutumiwa na nimrod mkono kiukweli hili unavyokataa binafsi mimi nakuona kituko mkono hajaanza leo kukutumia mpaka anakununulia ile gari ambayo kwasasa umeikodisha ni katika makubaliano yenu ya baadhi ya kazi unazomfanyia za kutumika kiukweli zitto nilikuwa shabiki wako sana tangu nijue kuwa wewe mla rushwa nakuweka kundi moja na wachumia tumbo wengine na hii tabia ya rushwa na wizi sasa umemfundisha hata deo filikunjombe.
ushauri wangu kwako fanyeni yote mnayofanya watanzania wasije kuwajua lakini siku moja wakijua mtachomwa moto mchana kweupe.