Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, zikiwemo Kamati zake mbalimbali za Kudumu, linaongozwa na Katiba, Sheria na Kanuni za Kudumu za Bunge hilo. Kila jambo Bungeni husimamiwa na sheria tajwa. Hivi karibuni, kumetokea sintofahamu kati ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika na Taasisi za Umma (PAC) na viongozi wa TPDC.
Iliripotiwa kuwa viongzi husika waliagizwa na Kamati ya
Zitto kuwasilisha nyaraka mbalimbali mbele ya Kamati hiyo. Ikaripotwa tena kuwa kufuatia kukaidi kwa viongozi hao kuwasilisha nyaraka,walikamatwa na polisi na baadaye kuachiwa baada ya kuhojiwa.
Bunge linapewa nguvu kupitia Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge ya 1988 iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2004 kupitia Sheria Nambari 3 ya 2004. Binafsi nimevutiwa na kifungu cha 17(2) cha Sheria tajwa ya 1988 ambacho hakikuguswa na marekebisho ya 2004. Sakata la viongozi wa TPDC linahusiana nacho.Kifungu kinasomeka hivi:
17 (2) Where any person ordered to attend or to give evidence or produce any document before any committee refuses to answer any question that
may be put to him or to produce any such document on the ground that. the same is of aprivate nature and does not affect the subject of inquiry,
the chairman of the committee may report such refusal to the Speaker with the reasons therefor; and the Speaker may thereupon excuse the
answering of such question or the production thereof.
Ni wazi, kama ilivyoripotiwa kuwa viongozi wa TPDC waliagizwa na Kamati ya Zitto kuwasilisha nyaraka.Pili, kwa maneno au matendo hawakuwasilish na hivyo kuonekana wamekataa. Mwenyekiti wa PAC angeweza kuripoti kwa Spika wa Bunge akiainisha sababu za kuripoti kwake na mwisho mwishoni Spika angeweza kusamehe kutolewa kwa nyaraka hizo.Yaani, Spika angeweza kulazimsha au kusamehe uwasilishwaji wa nyaraka husika.Hapo nimetafsiri kifungu cha hapo juu pamoja na kilichoripotiwa.
Hivyobasi, PAC haina na haikuwa na mamlaka ya kuwakamata au kusababisha kukamatwa kwa viongozi wa TPDC. Kama ilifanyika kinyume na utaratibu uliowekwa na Sheria, PAC iliteleza.