Mkuu
Nashukuru kwa maelekezo yako.
Lakini naomba nikuweke sawa, mimi sichangii hapa kishabiki, Lakini natambua kwamba msimamo wangu juu ya
Zitto ni Negative, na sidhani kama hilo ni Kosa.
Sasa turudi kwenye hoja yako?
Unamaanisha kwamba Mwanasheria wa Bunge aliwapa akina uzito ushauri kwamba wanaweza wakaruka taratibu za kupeleka mahitaji yao kwa speaker ili ayawasilishe serikalini na hata kuruka ngazi zingine za kiserikali na kwenda moja kwa moja polisi? sababu hicho ndio walichokifanya kina
Zitto.
Na Je, lengo lao la kuwaitia jamaa polisi ni nini? Wote tunajua polisi ni njia tu ya kufika mahakamani, sasa PAC walikuwa wamechukua maamuzi ya kuwapeleka jamaa mahakamani?
Ndio maswali yangu hayo, labda ungenijibu na mimi, sababu majibu yako kwa mleta mada nimeyaelewa.
Ama sivyo kama issue imeisha, inabidi tujue lengo lilikuwa ni nini? Sababu kama waliteleza Je, wameanzisha mchakato stahili? Kama hawajaanzisha ni kwa nini? au wameishapewa hiyo mikataba?