Zitto na PAC yake waliteleza?

Zitto na PAC yake waliteleza?

hawa jamaa kukamatwa ni hatua moja kupelekwa mahakamani ni hatua nyingine , msingi mubwa ni kuhakikisha suala hili halijadiliwi bungeni maana litakuwa kwenye muhimili mwingine basi.
 
mimi nilishangaa sana yaani unamkamata mtu aliyeteuliwa na mkuu wakati all the instruction anazipata kutoka juu

Kingmairo kalijibu vizuri swali unalouliza. Mbona wale punda wa unga kule China wanaozea jela wao wenyewe baada ya kushikwa na si wale waliowatuma??
Kamati imeshughulika na waliopewa dhamana full stop! Ndiyo maana kwenye haya mawizara wakurugenzi na viongozi makini ni wale wanaopokea maelekezo in writting, hata kama ni kimemo cha maandishi ya mkono!! Wale wachumia tumbo ndo wanapokea maelekezo nyeti kwa simu na saa hiyo hiyo anakurupuka kutekeleza, mambo yakibuma aliyempa instructions anamruka maili mia!!
 
Nasikia Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati E. Maswi aliingilia kati na kusema kua Zitto na kamati yake hawana mamlaka ya kuwaweka ndani kwa hiyo ni makosa kuwaweka ndani.

Mimi sina tatizo kabisa na ilicho fanya Kamati ya Zitto Kabwe. Kama Polisi na Vyombo vya Mashtaka vimeshindwa kuchukua hatua hilo ni tatizo la Sheria zetu na Uwajibikaji. Ni mwendelezo wa siasa zetu za kijinga. Ni mwendelezo wa ujinga wa Waziri na Katibu wake Mkuu wa Wizara ambao wamejenga kiburi kama hiyo ni Ofisi yao binafsi! Ni mwendelezo wa ujinga wetu kulalamikia mtu wa pembeni badala ya mhusika! Ni udhaifu wa utawala wa Kikwete umesababisha hawa wasilale ndani na wanao wazuia wasitoe Mikataba wakatimuliwa
 
Tanzanian. Mko busy kutizama weaknesses za individuals, badala ya kuangalia masuala muhimu. Inshu sio kukamatwa, Inshu ni MIKATABA iwasilishwe kwenye kamati ya PAC. Nadhan swali la kujiuliza ni kwann inafanywa siri kiasi hicho? Wanaficha nn na kwann?

Wananchi nadhan tungewapokea wajumbe wa PAC, Kwa kudemonstrate na kushinikiza serikali iweke wazi hiyo mikataba, ili Mafisadi wajukikane... Tuache kushambuliana, we r Loosing the Big Target here... Halafu, humans tunakosea, we deserve second Chances, Let us not Loose hope completely kwa Mh. Zitto, Mimi binafsi naona anafanya kazi nzuri... Tumpe support. Tuache Ujuaji, Na unabii wa kijinga.

Well said mkuu, kula likes zangu. Hili ndilo tatizo letu kuu, tumeacha hoja kuu ya TPDC kugomea mikataba ya rasilimali za nchi tumeng'ang'ana na Zitto as if hiyo kamati ni yeye peke yake!
Nchi ina hali mbaya sana shauri ya mambo haya haya badala ya kuendesha mijadala humu mitandaoni na kwingineko kuiunga kamati mkono na kuibana serikali mikataba itolewe ili tujue wanaotuhujumi tuko bize kulumbana wenyewe kwa wenyewe.
Kama akina Chenge walipewe mabilioni kwenye dili la rada ni nini kitazuia hawa watendaji wa TPDC na wizara wasihongwe ili kuingia mikataba isiyo na maslahi na nchi yetu?? Jiulize kwa nini wanaifanya siri hata kwa kamati za bunge?? 2 yrs now hawataki kabisa kuitoa why??



/
 
Hata kama wameteleza kwangu ni sawa. Kwa kiburi na ukaidi wa watendaji wa serikali ni bora tu mtu uzivuke taratibu kuwakomesha wapuuzi wanaolinyonya taifa. Mtu mikataba ni ya rasilimali za nchi sio document za ndoa zao kwanini hawataki wawakilishi wetu sie wenye nchi wazione? Ni nini wanaficha kwenye hiyo mikataba? Wameshazoea kutumia uzoefu wao kwenye mapungufu ya hizi sheria kutufunga midomo. Hii ndo dawa yao.

Pinda alipotoa kauli kuwa watu wanaowaua zerezeru nao pia wauliwe tulipiga kelele ajiuzulu! Pinda aliposema wapinzani nwanasumbua wapigwe tu, tukamtaka ajiuzulu. Sita na ndugu zake wanapovunja sheria bunge la katiba tunalalamika hadi hamu ya kula hatupati Leo zitto na kamati yake wanavunja sheria tunamwona mashujaa, wametumia udikteta kulinda mali ya umma ehheeee?

Juzi makamba (na wengine) wmesema tunahitaji raisi dikteta kila mtu humu kalia naye hadi CCM wenzake wamelia!!!! Zito na kamati yake ni wakosaji kwa hili na wanapaswa kuoma radhi kwa udhalilishaji na uvunjifu wa sheria.

Sheria haziendeshwi na mapenzi na ushabiki hata siku moja. sio sahihi kumshabikia zito hata kama nia njema, afuate sheria.
 
Pinda alipotoa kauli kuwa watu wanaowaua zerezeru nao pia wauliwe tulipiga kelele ajiuzulu! Pinda aliposema wapinzani nwanasumbua wapigwe tu, tukamtaka ajiuzulu. Sita na ndugu zake wanapovunja sheria bunge la katiba tunalalamika hadi hamu ya kula hatupati Leo zitto na kamati yake wanavunja sheria tunamwona mashujaa, wametumia udikteta kulinda mali ya umma ehheeee?

Juzi makamba (na wengine) wmesema tunahitaji raisi dikteta kila mtu humu kalia naye hadi CCM wenzake wamelia!!!! Zito na kamati yake ni wakosaji kwa hili na wanapaswa kuoma radhi kwa udhalilishaji na uvunjifu wa sheria.

Sheria haziendeshwi na mapenzi na ushabiki hata siku moja. sio sahihi kumshabikia zito hata kama nia njema, afuate sheria.

mikataba inatoka lini? acha kujivua akili wewe
 
Wakuu hii hoja tumsimtazame Zitto as Zitto but tuntazame Zitto kama mwenyekiti wa PAC, ili hoja iende vizuri.
Back to topic: kwangu mimi naona kama suala hili endapo litapelekwa mahakamani basi ndio utakuwa mwisho wa mjadala huu kwa kisingizio cha kulinda uhuru wa mahakama, by conclude hapa kamati ya PAC itakuwa haijasaidia kitu zaidi ya kuizamisha hoja hii shimoni.
 
Kingmairo kalijibu vizuri swali unalouliza. Mbona wale punda wa unga kule China wanaozea jela wao wenyewe baada ya kushikwa na si wale waliowatuma??
Kamati imeshughulika na waliopewa dhamana full stop! Ndiyo maana kwenye haya mawizara wakurugenzi na viongozi makini ni wale wanaopokea maelekezo in writting, hata kama ni kimemo cha maandishi ya mkono!! Wale wachumia tumbo ndo wanapokea maelekezo nyeti kwa simu na saa hiyo hiyo anakurupuka kutekeleza, mambo yakibuma aliyempa instructions anamruka maili mia!!

siku hizi maagizo au malalamiko ni kwa njia ya email na barua,hii inafuta utata,njia kama simu au maneno ya ana kwa ana hayana ushahidi,sijuh lini watakuwa smart
 
Bunge limetoa go ahead kwa jamaa kukamatwa,ushahd uko wazi,kama siasa hazitaingia hawa jamaa watapigwa miaka miwili jela
 
kwanza inaonyesha kila dalili kuwa wale jamaa waliandaliwa kiaina kabisa kwamba watapelekwa polisi then wataachiwa, inaonyesha huo mpango uliandaliwa mahsusi tangu awali ili kuanza kuliinua jina la msaliti juu, bahati mbaya halijainuka,

Uko smart mkuu ile ni drama huyu msaliti anatumia kila njia kujibua lakini ndio keshapima kina cha tope kwa miguu miwili, atajaribu kila aina ya u-senge lakini hataweza kujiokoa.
 
Pinda alipotoa kauli kuwa watu wanaowaua zerezeru nao pia wauliwe tulipiga kelele ajiuzulu! Pinda aliposema wapinzani nwanasumbua wapigwe tu, tukamtaka ajiuzulu. Sita na ndugu zake wanapovunja sheria bunge la katiba tunalalamika hadi hamu ya kula hatupati Leo zitto na kamati yake wanavunja sheria tunamwona mashujaa, wametumia udikteta kulinda mali ya umma ehheeee?

Juzi makamba (na wengine) wmesema tunahitaji raisi dikteta kila mtu humu kalia naye hadi CCM wenzake wamelia!!!! Zito na kamati yake ni wakosaji kwa hili na wanapaswa kuoma radhi kwa udhalilishaji na uvunjifu wa sheria.

Sheria haziendeshwi na mapenzi na ushabiki hata siku moja. sio sahihi kumshabikia zito hata kama nia njema, afuate sheria.
Pinda aliyatoa hayo baada ya sheria kuvunjwa, kwa utetezi wake akazidi kuvunja sheria. Kina sita wamevunja sheria kuhalalisha maslahi ya kikundi chao tena ya watu wachache, viongozi wamekuwa wakivunja sheria kwa namna nyingi na tofauti tofauti kwa maslahi yao au ya familia au mitandao yao sio kwa manufaa ya nchi. Kote huko hakuna hatua yoyote tangible mloichukua. Kibaya zaidi wataendelea kuvunja sheria hizi tena kwa maslahi yao na hamtawafanya chochote. Leo hii zitto anapindisha taratibu kwa kutetea maslahi katika rasilimali zenu, mnamuona scrapegoat?
 
siku hizi maagizo au malalamiko ni kwa njia ya email na barua,hii inafuta utata,njia kama simu au maneno ya ana kwa ana hayana ushahidi,sijuh lini watakuwa smart

Hao wanaowaita maboss wao ndo wapo smart kuliko watendaji. Kamwe hawaandiki email wala barua. Wanajua wanachoelekeza ni nje ya taratibu na hawataki kuja kuwa mbuzi wa kafara.
 
Wakuu hii hoja tumsimtazame Zitto as Zitto but tuntazame Zitto kama mwenyekiti wa PAC, ili hoja iende vizuri.
Back to topic: kwangu mimi naona kama suala hili endapo litapelekwa mahakamani basi ndio utakuwa mwisho wa mjadala huu kwa kisingizio cha kulinda uhuru wa mahakama, by conclude hapa kamati ya PAC itakuwa haijasaidia kitu zaidi ya kuizamisha hoja hii shimoni.

umenigusa kiaina
 
Mimi sina tatizo kabisa na ilicho fanya Kamati ya Zitto Kabwe. Kama Polisi na Vyombo vya Mashtaka vimeshindwa kuchukua hatua hilo ni tatizo la Sheria zetu na Uwajibikaji. Ni mwendelezo wa siasa zetu za kijinga. Ni mwendelezo wa ujinga wa Waziri na Katibu wake Mkuu wa Wizara ambao wamejenga kiburi kama hiyo ni Ofisi yao binafsi! Ni mwendelezo wa ujinga wetu kulalamikia mtu wa pembeni badala ya mhusika! Ni udhaifu wa utawala wa Kikwete umesababisha hawa wasilale ndani na wanao wazuia wasitoe Mikataba wakatimuliwa

TUKIO hili na ufisadi wa aina hii ni mfano hai wa kuthibitisha na kutumotisha kwa nini tutetee RASIMU YA KATIBA YA WANANCHI (almaarufu RASIMU YA WARIOBA) vs. Katiba ya CCM inayopendekezwa (ambayo inaendeleza uozo huu). Haya yote yalikuwa yamepewa ibara katika rasimu ya katiba ya wananchi. Kikwete, Sitta, na Chenge hawapendi kusikia uwajibikaji juu ya mali za umma. Inaumiza sana.
 
Pinda aliyatoa hayo baada ya sheria kuvunjwa, kwa utetezi wake akazidi kuvunja sheria. Kina sita wamevunja sheria kuhalalisha maslahi ya kikundi chao tena ya watu wachache, viongozi wamekuwa wakivunja sheria kwa namna nyingi na tofauti tofauti kwa maslahi yao au ya familia au mitandao yao sio kwa manufaa ya nchi. Kote huko hakuna hatua yoyote tangible mloichukua. Kibaya zaidi wataendelea kuvunja sheria hizi tena kwa maslahi yao na hamtawafanya chochote. Leo hii zitto anapindisha taratibu kwa kutetea maslahi katika rasilimali zenu, mnamuona scrapegoat?

Badala ya kushughulikia kupukutisha majani ya mti, tungemwona wa maana kama angeunga na wapiganaji na wanaharakati wa UKAWA kushughulikia kung'oa mizizi ya ufisadi kwa kudai katiba ya wananchi ambayo kama ingepitishwa haya yote yangekuwa yamepatiwa mwarobaini come next year! Lakini sasa anafanya usanii wa kuwasweka ndani vidagaa huku akibeza juhudi za UKAWA. Ni msanii tu kama alivyo propesa jk.
 
mpeni pole kachanganyikiwa jamn,mtu hajui hata separation of power anakurupuka tu kimaamuzi,lazima ujue na uheshimu kazi ya kila mhimili wa setikali
 
Well said mkuu, kula likes zangu. Hili ndilo tatizo letu kuu, tumeacha hoja kuu ya TPDC kugomea mikataba ya rasilimali za nchi tumeng'ang'ana na Zitto as if hiyo kamati ni yeye peke yake!
Nchi ina hali mbaya sana shauri ya mambo haya haya badala ya kuendesha mijadala humu mitandaoni na kwingineko kuiunga kamati mkono na kuibana serikali mikataba itolewe ili tujue wanaotuhujumi tuko bize kulumbana wenyewe kwa wenyewe.
Kama akina Chenge walipewe mabilioni kwenye dili la rada ni nini kitazuia hawa watendaji wa TPDC na wizara wasihongwe ili kuingia mikataba isiyo na maslahi na nchi yetu?? Jiulize kwa nini wanaifanya siri hata kwa kamati za bunge?? 2 yrs now hawataki kabisa kuitoa why??



/

Si ajubu tupo compromised! Nadhan kuna watu humu ndani wameletwa kwa lengo la kuhamisha akili zetu from the Big Picture' wanatusumbua na kutulazimisha kutizama kivuli cha picha, kisha wanatuacha tunatapa tapa kumjua the 'Real Enemy' and Yes we have Fallen into the Trap.

Watanzania tuna unafki mwingi sana. Tunajitangaza wazalendo, but in 'reality' wengi wetu ni wachumia tumbo, wenye madaraka mpaka mwananchi wa kawaida. Both are Looking for Opportunities na wao washibe.... Tuamke wadau, hakuna wakutuletea maendeleo zaidi ya sisi wenyewe... Serikali haina hofu na sisi, becouse we can easy be manipulated any time, any how. 'POOR WE'.

Boss wangu Mkenya alinitukana hivi 'Tatizo lenu nyie watanzania mnajua tuu kulalamika, kisha mnarudi ndani mnafuta machozi mnaendelea... You don't ACT, you don't STRIKE... Mpo mpo kama............! Sikujali katukana nn, nilichokuwa natafakari ni contents za hayo maneno yake.. Nikaona Ukweli Mwingi, Nikakausha.

Sisi ndio Mabalozi wa kuleta mabadiliko. Kila mtu kwa nafasi yake, perhaps some Yearz ahead huko, tutaanza kuiona aina ya TANZANIA TUNAYOITAKA.... Kuna Network kubwa Sana ya hawa MAFISADI, kuivunja vunja yote na kuisambaratisha we must UNIT, sisi Wananchi, Ni lazima tuwe na GOAL moja... Lakini nachoona hapa ni aibu tupu. Like this, we have a Long F@#¥£$*KING WAY to go. Like I said.... POOR WE.
 
"POOR WE". Twiga wanasafirishwa, wanauzwa nje kama karanga, Tupo kimya. Madawa ya kulevya, Bangi, Pembe za Ndovu, kucha za Simba n.k vinakamatwa kila iitwayo LEO lakin, sijawahi kusikia Serikali inazifanyia nn hizo vitu? Je watavichoma? Ama wataviuza? Wanajua Mpaka bei, lakin hatujui wamejuaje? Soko ni lipi? Wapi?.... Kuna Ujinga Mwingi Serikali inafanya. Na tumenyamaza kabisa.... Sasa wanapeana nchi ki ndugu, Tumenyamaza, Tsh inazidi ku depreciate tupo kimya. Wanapandisha nauli Bei ya mafuta ikipanda, Yakishuka bei wanakausha... Yakipanda tena kwenye rate ile ile ya mwanzo, ama yakizidi kidooogo tuu, wanapandisha tena Nauli... Tunaumia mimi na ww, Yet bado Tunashabikia Ujinga. "POOR WE"...

Nadhani WaTz hatuko sawa Mentally....
 
Zito ni mzuri sana wa kujenga hoja lakini mara nyingi ni mzushi na mwongo. Na mara nyingi hufanya mambo mengi kwaajili ya personal political gains kuliko faida ya umma.

Hata tukilazimisha vipi, ukweli hubakia kuwa Duniani kote mikataba ya kibiashara huru ni siri kati ya wale wahusika wakuu. Tatizo kubwa hapa kwetu siyo usiri wa mikataba bali uadilifu wa wanaosaini mikataba kwa niaba ya Taifa.
 
Bado Zitto anaendeleza undumi la kuwili kwa kutumika kuhalalisha mikataba hii! Na ndicho alichokuwa anafanya tangu awali alipokuwa CDM, kuna msemo usemao kuwa ukiwa mnafiki ujanani ukiwa mzee utakuwa mchawi!
 
Back
Top Bottom