Zitto na PAC yake waliteleza?

Zitto na PAC yake waliteleza?

wa Tz wengi ni simple minded mara nyingi hatujadili matatizo na kuyatafutia suluhisho ila tunajadili watu. Na viongozi wetu wamegeuza matatizo yetu ndo mtaji wao kisiasa.

Kulalamika tumeshalalamika sn, huu ni wakati wa kuchukua hatua. MSD wamegoma kuziuzia madawa hospital za selikali kwa sababu wanaidai serikali wakati watu wachache wananufaika na jasho letu!

Viongoz wanatumia bajet kubwa kufanya ziara nchi za nje wakati hospital hazina madawa, akina mama wajawazito wazito wanakufa ila watz tunaona sawa! Tukiambiwa taifa halina hela tunakubali kirahisi kabisa. Tumegeuzwa mtaji bila sisi kujijua na tumeikubali hali hii.

Nchi hii inawanufaisha wachache ila watz wao hilo ni sawa!
 
Well said mkuu, kula likes zangu. Hili ndilo tatizo letu kuu, tumeacha hoja kuu ya TPDC kugomea mikataba ya rasilimali za nchi tumeng'ang'ana na Zitto as if hiyo kamati ni yeye peke yake!
Nchi ina hali mbaya sana shauri ya mambo haya haya badala ya kuendesha mijadala humu mitandaoni na kwingineko kuiunga kamati mkono na kuibana serikali mikataba itolewe ili tujue wanaotuhujumi tuko bize kulumbana wenyewe kwa wenyewe.
Kama akina Chenge walipewe mabilioni kwenye dili la rada ni nini kitazuia hawa watendaji wa TPDC na wizara wasihongwe ili kuingia mikataba isiyo na maslahi na nchi yetu?? Jiulize kwa nini wanaifanya siri hata kwa kamati za bunge?? 2 yrs now hawataki kabisa kuitoa why??



/

mkuu mimi nipo nafanya kampuni moja ya umme ambayo tunalipa kapacity charge nzuri tu hata kama mitambo haitembei hawa jamaa wanaweza kuendelea kulipa mkopo walio kopa bank na bado faida wakapata, TPDC hawasaini mkataba nachojua ni kiongozi mwenye dhamana na nchi ndio anasign mkataba
 
Ni Kweli waliteleza ...walitakiwa kupata Kibali cha spika ...kabla ya kuwatia ndani wale Jamaa ...,Sioni kwanini hawakuomba kile kibali ..week Moja kabla ..unless walikuwa na mashaka kuwa spika angepitisha wakamatwe ..
Wamefanya kazi nzuri though Jamaa wanaweza KUDAI fidia...UJUMBE umefika .....though Kisiasa wanaweza Kuiweka Kama vile wajumbe walitaka kupata faida ya kisiasa

Na huo ndo ukweli Zitto alikuwa anatafuta "comeback" imegoma!
 
kwanza inaonyesha kila dalili kuwa wale jamaa waliandaliwa kiaina kabisa kwamba watapelekwa polisi then wataachiwa, inaonyesha huo mpango uliandaliwa mahsusi tangu awali ili kuanza kuliinua jina la msaliti juu, bahati mbaya halijainuka,

ni kweli na ndio maana unamjadili.
hahahaaaaaa. BAVICHA akili zao ziko kama BAWACHA.. mnafikiri kwa kutumia jinsia ya kike hahahahahahaaaa
 
Tatizo la MM ni ukurupukaji.Ukiacha issue ya Buzwagi aliyoihandla vema,zingine amekurupuka sana.
Hii inazidi kumpunguzia credibility na kuaminika kwa umma.
 
Katika hili naipongeza kamati ya PAC chini ya mwenyekiti wake Ndg Zitto na Ndg Filikunjombe. Wameonesha ni kwa jinsi gani wanachukizwa na uzembe, ujinga na ubinafsi wa watu wachache ambao kwa ubinafsi wao wameisababibishia nchi umaskini huku wao wakineemeka kwa mikataba bibovu. Nasema hivi kwa sababu kuna ulazima gani wa mikataba kama hiyo kufichwa. Nilitegemea mikataba ya rasilimali za taifa iwe public document ili kila mmoja ajue nani analipa nini kwa muda gani. Lakini pia nilijifinza kitu kimoja kwenye maojianao ya Zitto na Mkurugenzi wa TPDC. Kwamba mkurugenzi wa TPDC ama bado hajaelimika au ni ulimbukeni. Eti hawezi kutoa mikataba mpaka apate ruhusa ya wazungu wawekezaji. Hivi hata kama kipengele hicho kimo, ili hitaji kuwa amemaliza darasa la saba ili kuweza kugundua na kukikataa kifungu hicho kabla ya kusign!!! Huu si mwendelezo wa utumwa na mikataba ya Chief Magungo wa Msovero. Yeye anatofauti gani na huyo Chief??? Nachukizwa na watu amabao bado wanawanyenyekea wazungu wakidhani bila wao mambo hayaendi. Rasilimali ni zetu hivyo mdundo wowote unaochezwa lazima uwe ule tunaouchagua sisi. Kamati ya PAC imeonesha mwanzo wa huko tunakoelekea. Kwamba huko tunakoelekea watu watataka kuona kila kitu kweupe. Haya mambo ya kuficha ficha mnaficha nini. Na siku tukigundua kuwa kuna watu wachache walijinufaisha kwa mikataba ya kijinga si wao wala watoto wala wajukuu na vitukuu watakuwa salama. Wako salama kwa muda tu. Tumechoka na hivyo tumeanza kusaka watu wanaotuibia na kuwawekea dot. Kazi ikianza ya kuwashughulikia, si muda neema itakuwa kwa wananchi.
 
Last edited by a moderator:
Pinda aliyatoa hayo baada ya sheria kuvunjwa, kwa utetezi wake akazidi kuvunja sheria. Kina sita wamevunja sheria kuhalalisha maslahi ya kikundi chao tena ya watu wachache, viongozi wamekuwa wakivunja sheria kwa namna nyingi na tofauti tofauti kwa maslahi yao au ya familia au mitandao yao sio kwa manufaa ya nchi. Kote huko hakuna hatua yoyote tangible mloichukua. Kibaya zaidi wataendelea kuvunja sheria hizi tena kwa maslahi yao na hamtawafanya chochote. Leo hii zitto anapindisha taratibu kwa kutetea maslahi katika rasilimali zenu, mnamuona scrapegoat?

Huwezi kusimamia sheria moja kwa kuvunja sheria nyingine, harafu unatumia lugha rahisi "zito kapindisha sheria" hii haikubaliki katika demokrasia za kweli, hapa naona unaungana na kina makamba kuutaka udikteta ila kwa kuwa makamba upo CCM huwezi kusema moja kwa moja kuwa unamuunga mkono. Zitto na kamati yake wamevunja sheria, waombe radhi kwa kuvunja sheria za nchi. Hatutegemei kamati ya Bunge kuvunja sheria, ni aibu kwamba wanatunga sheria halafu wenyewe hawazielewi.
 
Huwezi kusimamia sheria moja kwa kuvunja sheria nyingine, harafu unatumia lugha rahisi "zito kapindisha sheria" hii haikubaliki katika demokrasia za kweli, hapa naona unaungana na kina makamba kuutaka udikteta ila kwa kuwa makamba upo CCM huwezi kusema moja kwa moja kuwa unamuunga mkono. Zitto na kamati yake wamevunja sheria, waombe radhi kwa kuvunja sheria za nchi. Hatutegemei kamati ya Bunge kuvunja sheria, ni aibu kwamba wanatunga sheria halafu wenyewe hawazielewi.

Je kuna watu wanaruhusiwa kusimamia sheria kwa kuvunja sheria ila wengine ndo hawaruhusiwi? Huyo uliyequote, pinda, alivunja sheria pia akidhani anasimamia sheria. By the way, kama kweli una mtazamo wa sheria itawale kila sehemu unawezaje kusema waliovunja sheria waombe radhi? Au ndo unaendeleza kile kizazi cha EPA kilichoomba msamaha? Kama ni utawala wa sheria ufatwe na watu wote kwa kila jambo, sio wengine waonekane wanaruhusiwa na wengine sio.
 
Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, zikiwemo Kamati zake mbalimbali za Kudumu, linaongozwa na Katiba, Sheria na Kanuni za Kudumu za Bunge hilo. Kila jambo Bungeni husimamiwa na sheria tajwa. Hivi karibuni, kumetokea sintofahamu kati ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Mashirika na Taasisi za Umma (PAC) na viongozi wa TPDC.

Iliripotiwa kuwa viongzi husika waliagizwa na Kamati ya Zitto kuwasilisha nyaraka mbalimbali mbele ya Kamati hiyo. Ikaripotwa tena kuwa kufuatia kukaidi kwa viongozi hao kuwasilisha nyaraka,walikamatwa na polisi na baadaye kuachiwa baada ya kuhojiwa.

Bunge linapewa nguvu kupitia Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge ya 1988 iliyofanyiwa Marekebisho mwaka 2004 kupitia Sheria Nambari 3 ya 2004. Binafsi nimevutiwa na kifungu cha 17(2) cha Sheria tajwa ya 1988 ambacho hakikuguswa na marekebisho ya 2004. Sakata la viongozi wa TPDC linahusiana nacho.Kifungu kinasomeka hivi:

17 (2) Where any person ordered to attend or to give evidence or produce any document before any committee refuses to answer any question that

may be put to him or to produce any such document on the ground that. the same is of aprivate nature and does not affect the subject of inquiry,

the chairman of the committee may report such refusal to the Speaker with the reasons therefor; and the Speaker may thereupon excuse the

answering of such question or the production thereof.

Ni wazi, kama ilivyoripotiwa kuwa viongozi wa TPDC waliagizwa na Kamati ya Zitto kuwasilisha nyaraka.Pili, kwa maneno au matendo hawakuwasilish na hivyo kuonekana wamekataa. Mwenyekiti wa PAC angeweza kuripoti kwa Spika wa Bunge akiainisha sababu za kuripoti kwake na mwisho mwishoni Spika angeweza kusamehe kutolewa kwa nyaraka hizo.Yaani, Spika angeweza kulazimsha au kusamehe uwasilishwaji wa nyaraka husika.Hapo nimetafsiri kifungu cha hapo juu pamoja na kilichoripotiwa.

Hivyobasi, PAC haina na haikuwa na mamlaka ya kuwakamata au kusababisha kukamatwa kwa viongozi wa TPDC. Kama ilifanyika kinyume na utaratibu uliowekwa na Sheria, PAC iliteleza.


Kumbuka kuwa sio Zitto au kamati ya PAC waliochukua hatua hizo wao pia walishirikisha wanasharia wa bunge na hata walipokamatwa na kuwekwa ndani mwanasharia wa bunge alifafanua kwa kina kuwa walikuwa na mamlaka hayo.

Hebu pitia maelezo ya mwanasharia wa bunge aliyotoa kabla kutolewa amri ya kukamatwa kwa viongozi hao.

Lakin kwa upande mwingine kama viongozi hao wataona hawakutendewa haki na kamati hiyo ya PAC wana HAKI YA KWENDA MAHAKAMANI KUDAI HAKI YAO.

Tuvute subra tuona kama watakwenda mahakamani kudai haki yao ya kudhalilishwa na PAC

 
Je kuna watu wanaruhusiwa kusimamia sheria kwa kuvunja sheria ila wengine ndo hawaruhusiwi? Huyo uliyequote, pinda, alivunja sheria pia akidhani anasimamia sheria. By the way, kama kweli una mtazamo wa sheria itawale kila sehemu unawezaje kusema waliovunja sheria waombe radhi? Au ndo unaendeleza kile kizazi cha EPA kilichoomba msamaha? Kama ni utawala wa sheria ufatwe na watu wote kwa kila jambo, sio wengine waonekane wanaruhusiwa na wengine sio.

Kwangu mimi wote hao wanamakosa, Pinda, Zito na genge lake, makamba na wengine. Tofauti yangu na wewe ni kuwa wewe unaona Zitto yupo sahihi ila kina pinda na ndo wamekosea. Hapa ndo shida yetu. Pinda, Zitto na genge lake hawawezi kusimami sheria kwa kuvunja sheria, tu ahatupaswi kumsifia Zito na genge lake kwa uovu huu. Kama tulivolaani kwa Pinda ndo tunapaswa kulaani kwa Zitto. I am using my head, and I can see your using your "heart" its ok to use your heart to look for a wife, not in choosing political leaders.
 
Ni kweli akina ZITTO wamekosea haiwezekani popote duniani eti kila mbunge akitaka document anapewa Watanzania tuache ushabiki tuangalie Uzalendo na usalama wa taifa letu hivi akina Zitto au Kamati yao kazi yao ni kukagua mikataba au Kazi yao kukagua mahesabu ya Mashirika na taasisi za Serikali na hasa katika maeneo yenye matatizo ya kimahesabu? vile vile Zitto na wenzake hawana mamlaka hata kidogo ya kuamuru kupewa mikataba kwani utaratibu unatakiwa spika wa bunge ndiyo anayeandikiwa barua na kamati au mbunge kuombwa aombe mikataba au document zozote kutoka katika mhimili mwingine wa dola yaani Serikali au Mahakama. lakini kuna jambo moja la ajabu sana kwa wabunge wetu eti wamejigeuza ni kundi fulani la watu ambao ndiyo wenye haki na kila kitu na wasiguswe ila ukiwagusa wao unaambiwa umekiuka sheria kwa sababu wana kinga.vile vile mbona kila siku tunasikia wabunge wakiishambulia Serikali ambayo ndiyo mhimili mmojawapo wa dola mbona hawashambulii au kuihoji mahakama?
 
Kumbuka kuwa sio Zitto au kamati ya PAC waliochukua hatua hizo wao pia walishirikisha wanasharia wa bunge na hata walipokamatwa na kuwekwa ndani mwanasharia wa bunge alifafanua kwa kina kuwa walikuwa na mamlaka hayo.

Hebu pitia maelezo ya mwanasharia wa bunge aliyotoa kabla kutolewa amri ya kukamatwa kwa viongozi hao.

Lakin kwa upande mwingine kama viongozi hao wataona hawakutendewa haki na kamati hiyo ya PAC wana HAKI YA KWENDA MAHAKAMANI KUDAI HAKI YAO.

Tuvute subra tuona kama watakwenda mahakamani kudai haki yao ya kudhalilishwa na PAC


Mwanasheria wa Bunge alisemaje? Kwa nini tusubiri hao jamaa waende Mahakamani badala ya kusubiri Polisi wawafikishe mahakamani? Kwani kazi ya Polisi inaishia kuwakamata watu na kuwapeleka Polisi?

Tunachosubiri ni PAC iwafikishe mahakamani hao Jamaa, na ni update ya hatua hiyo ndio iliyonifanya leo niutembelee uzi huu.

Ama sivyo, Bunge linapaswa kukachukulia hatua ka Zitto kwa kujibebesha mamlaka ambayo PAC haina.

umenielewa?
 
Kwangu mimi wote hao wanamakosa, Pinda, Zito na genge lake, makamba na wengine. Tofauti yangu na wewe ni kuwa wewe unaona Zitto yupo sahihi ila kina pinda na ndo wamekosea. Hapa ndo shida yetu. Pinda, Zitto na genge lake hawawezi kusimami sheria kwa kuvunja sheria, tu ahatupaswi kumsifia Zito na genge lake kwa uovu huu. Kama tulivolaani kwa Pinda ndo tunapaswa kulaani kwa Zitto. I am using my head, and I can see your using your "heart" its ok to use your heart to look for a wife, not in choosing political leaders.

Safi sana.

Lakini HEAD ndio HEART. Kwa basis ya maelezo yako.
 
Katika hili naipongeza kamati ya PAC chini ya mwenyekiti wake Ndg Zitto na Ndg Filikunjombe. Wameonesha ni kwa jinsi gani wanachukizwa na uzembe, ujinga na ubinafsi wa watu wachache ambao kwa ubinafsi wao wameisababibishia nchi umaskini huku wao wakineemeka kwa mikataba bibovu. Nasema hivi kwa sababu kuna ulazima gani wa mikataba kama hiyo kufichwa. Nilitegemea mikataba ya rasilimali za taifa iwe public document ili kila mmoja ajue nani analipa nini kwa muda gani. Lakini pia nilijifinza kitu kimoja kwenye maojianao ya Zitto na Mkurugenzi wa TPDC. Kwamba mkurugenzi wa TPDC ama bado hajaelimika au ni ulimbukeni. Eti hawezi kutoa mikataba mpaka apate ruhusa ya wazungu wawekezaji. Hivi hata kama kipengele hicho kimo, ili hitaji kuwa amemaliza darasa la saba ili kuweza kugundua na kukikataa kifungu hicho kabla ya kusign!!! Huu si mwendelezo wa utumwa na mikataba ya Chief Magungo wa Msovero. Yeye anatofauti gani na huyo Chief??? Nachukizwa na watu amabao bado wanawanyenyekea wazungu wakidhani bila wao mambo hayaendi. Rasilimali ni zetu hivyo mdundo wowote unaochezwa lazima uwe ule tunaouchagua sisi. Kamati ya PAC imeonesha mwanzo wa huko tunakoelekea. Kwamba huko tunakoelekea watu watataka kuona kila kitu kweupe. Haya mambo ya kuficha ficha mnaficha nini. Na siku tukigundua kuwa kuna watu wachache walijinufaisha kwa mikataba ya kijinga si wao wala watoto wala wajukuu na vitukuu watakuwa salama. Wako salama kwa muda tu. Tumechoka na hivyo tumeanza kusaka watu wanaotuibia na kuwawekea dot. Kazi ikianza ya kuwashughulikia, si muda neema itakuwa kwa wananchi.

Kwani tunaingia hasara gani KWA SABABU TU Mikataba imefichwa?
 
Kwani tunaingia hasara gani KWA SABABU TU Mikataba imefichwa?

Kama mwananchi wa kawaida ninatakiwa kujua nchi yangu ananufaika vipi na mikataba inayoingia na wawekezaji. N apengine kwa kujijua tungeweza kuiboresha ili kuleta tija zaidi. Lakini kama mikataba inafichwafichwa namna hii basi ni dhahiri tunaendeleza hasara ambazo tumezipata kwenye mikataba ya madini. Nadhani tunaowataalam wengi nami nikiwepo, kama mikataba ya kitaifa ingekuwa ni public document basi kila mmoja angekuwa anajua ni kiasi gani tunapata. Nakama tunakosa / tunapata hasara kwasababu ya vipingele vya mikataba basi vingerekebishwa kwa mikataba mingine. Kuna nini nyuma ya kuficha mikataba kama si uovu uliopitishwa ama kwa makusudi baada ya kupata mlungula ili mambo yaende na hivyo kutusababishia hasara ya mapato kama nchi. Kama kila kitu kiko sawa kuna uoga gani wa kuiweka wazi. "Eti mpaka tupate ridhaa ya wawekezaji" Hiyo kweli ni akili, kama ulionakipengele hicho ulishindwa nini kukiondoa au kukikataaa kabla ya kusign huo mkataba. Ilitakiwa wajiulize kuna nini cha kufichaficha. Kwanini??? Kuna mambo mengi ya kujiuliza, hata mengine ni aibu kutamkwa na hao tunaowahita wasomi na wanasheria. Eti nao waliridhia!!! Pengine serikali imepunjwa mapato, baada ya hao wawakilishi kupewa mlingula na kuandaa mkatana wa hovyo. Au wameweka loop holes za kwemwezesha mwekezaji kukweka mapato baada ya kukatiwa chao na wao kukubaliana na vipengele vya kijinga. Ni ujinga kukumbatia mtu mpumbavu hata yeye atakuona ni mpumbavu hata kama hakwambiii.
 
Hivi mikataba nani anasign? Ni rais au waziri kwa niaba ya rais kama yule waziri aliye safiri na mihuri mpaka ulaya kuweka saini hotelini.
 
Safi sana.

Lakini HEAD ndio HEART. Kwa basis ya maelezo yako.

Sangara natumaini akili zako nyingi kuliko samaki sangara (no offence Mtanzania is meant), hapa namaanisha ni imani kuwa unaweza pia kumudu maisha ya nchi kavu (to decode hidden meangs of the words) sio kama samaki sangara anayemudu maisha ya kwenye maji tu (to undersant only the diretct meaning of the words).

Using your "head or sometimes referred to as brain" would mean being rational as informed by facts, which is contrally to using your "heart" where feelings driven by love lead your action or deeds.

Unaweza pia kusikiliza wimbo wa Lady JD - usiusemee moyo au Lauren Hill - zion. utapata vitu humo juu ya tofauti kati ya kutumia "moyo" na kutumia "akili".
 
..hivi kwanini ACT hawachukui hoja hii ya mwenyekiti wao mtarajiwa.

..hiki chama kinatakiwa kiwe kiungo kati ya harakati za Zitto bungeni na wananchi huku mitaani.
 
Sangara natumaini akili zako nyingi kuliko samaki sangara (no offence Mtanzania is meant), hapa namaanisha ni imani kuwa unaweza pia kumudu maisha ya nchi kavu (to decode hidden meangs of the words) sio kama samaki sangara anayemudu maisha ya kwenye maji tu (to undersant only the diretct meaning of the words).

Using your "head or sometimes referred to as brain" would mean being rational as informed by facts, which is contrally to using your "heart" where feelings driven by love lead your action or deeds.

Unaweza pia kusikiliza wimbo wa Lady JD - usiusemee moyo au Lauren Hill - zion. utapata vitu humo juu ya tofauti kati ya kutumia "moyo" na kutumia "akili".

Kwani hatu LOVE kwa kupitia Brain? au feelings zetu hazi originate from the brain? The Heart is meant for pumping blood around only, the thinking, loving and the so you called feelings originate from the brain.

Before we derail this thread, My point was that, the other guy's comment are being driven by some vested interests and not free thinking as you approached it.
 
Kama mwananchi wa kawaida ninatakiwa kujua nchi yangu ananufaika vipi na mikataba inayoingia na wawekezaji. N apengine kwa kujijua tungeweza kuiboresha ili kuleta tija zaidi. Lakini kama mikataba inafichwafichwa namna hii basi ni dhahiri tunaendeleza hasara ambazo tumezipata kwenye mikataba ya madini. Nadhani tunaowataalam wengi nami nikiwepo, kama mikataba ya kitaifa ingekuwa ni public document basi kila mmoja angekuwa anajua ni kiasi gani tunapata. Nakama tunakosa / tunapata hasara kwasababu ya vipingele vya mikataba basi vingerekebishwa kwa mikataba mingine. Kuna nini nyuma ya kuficha mikataba kama si uovu uliopitishwa ama kwa makusudi baada ya kupata mlungula ili mambo yaende na hivyo kutusababishia hasara ya mapato kama nchi. Kama kila kitu kiko sawa kuna uoga gani wa kuiweka wazi. "Eti mpaka tupate ridhaa ya wawekezaji" Hiyo kweli ni akili, kama ulionakipengele hicho ulishindwa nini kukiondoa au kukikataaa kabla ya kusign huo mkataba. Ilitakiwa wajiulize kuna nini cha kufichaficha. Kwanini??? Kuna mambo mengi ya kujiuliza, hata mengine ni aibu kutamkwa na hao tunaowahita wasomi na wanasheria. Eti nao waliridhia!!! Pengine serikali imepunjwa mapato, baada ya hao wawakilishi kupewa mlingula na kuandaa mkatana wa hovyo. Au wameweka loop holes za kwemwezesha mwekezaji kukweka mapato baada ya kukatiwa chao na wao kukubaliana na vipengele vya kijinga. Ni ujinga kukumbatia mtu mpumbavu hata yeye atakuona ni mpumbavu hata kama hakwambiii.

Namna Nchi inavyofaidika na mikataba husika ni kwa njia ya Kodi, namna ingine zimeandikwa kwenye sheria ya nishati na madini na sera ya uwekezaji katika sekta hiyo.

Kila Siku J.J Mnyika anazungumzia swala la sera ya Mafuta na Gas kupelekwa Bungeni Kujadiliwa, ni hapo ndio wananchi tunapaswa kushiriki.

Ni kwenye sheria na sera ndio tunapaswa kuwa makini na kuishauri serikali sio wakati wa kuingia mikataba, watu wanaong'ang'ana na mikataba ni wala rushwa tu, na kutafuta sifa za kijinga.

Ni kweli kwenye utoaji wa haki za uwekezaji katika sekta ya Mafuta, Gas na Madini KUNA RUSHWA, LAKINI NI RUSHWA AMBAYO HATA KAMA ISINGETOLEWA SIO KWAMBA INGEINGIA SERIKALINI.

Kuna Maamuzi fulani hivi yanayotegemea Mtu mwenye mamlaka ya japo kushauri tu,anatumia busara, hisia na uelewa wake binafsi kufanya maamuzi, ndio maana serikalini kuna wasomi wa kila namna, wanategemewa kutumia usomi wao katika wakati huo.

Sasa hapo ndio wanapewa TIP, Na sio kwamba eti kuna fee ilitakiwa kulipwa, mtu apewe rushwa ili fee isilipwe, Kila kitu kinachotakiwa kufanywa katika utaratibu fulani kinafanywa lakini on top of that, ili mtu asicheleweshe mambo au basi tu ampendelee fulani, ANAPEWA RUSHWA, Ama sivyo mwisho wa siku hata asingepewa Rushwa angesign tu.

Narudia, NI RUSHWA AMBAZO ZIKITOLEWA AMA ZISIPOTOLEWA HAKUNA KITU SERIKALI YETU INAPOTEZA, Unless kama kuna makosa mengine ya kiufundi yamefanyika wakati wa mchakato wa kutiliana mkataba.

SASA KELELE ZOOOOTE ZA WATU AINA YA Zitto ni Kupata mgao, ndio maana akina Maswi huwa wanakatukana ka Zitto sababu kanataka kula kwenye dili ambazo hakahusiki, kanataka na kenyewe kapewe u consultant kapige hela.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom