Zitto Kabwe: "UKs Aid is reparation for colonial exploits"

Zitto Kabwe: "UKs Aid is reparation for colonial exploits"

Status
Not open for further replies.
Wakuu zangu nimeingia katikati ya Mjadala... Hivi kweli hamuamini maneno aliyoyasema Zitto au mnayo tafsiri yenu?..
Ukoloni haukwisha baada ya kupata uhuru wa bendera, na haujaisha upo bado na utaendelea kuwepo kwa muda mrefu sana ikiwa sisi wenyewe hatujifunza Uzalendo na haki ya Uraia..Hadi leo hii kilichobadilika ni vichwa tu vya watawala toka ngozi nyeupe kuja Nyeusi lakini walijua wataweza fidia vipi kuutoa uhuru kwa nchi nyingi za kiafrika kwa hiari yao. Na kiongozi yeyote anayetambua hilo mapema nadhani tunatakiwa kumpa moyo zaidi kwa sababu msisikie Ukoloni mamboleo ni mbaya kuliko ule wa Kukoloniwa...

Yes Miaka 50 ya Uhuru imetufikisha hapa na wakati wote wa Nyerere, Mkapa Mwinyi na hadi JK tumeona jinsi mkoloni alivyokuwa na mbinu za kila aina utafikri ni part of evolution...they were prepared for changes hizi na wao wako mbele yetu kwa kila hatua ya mageuzi. Ebu jiulizeni mifumo yote hii ya Uchumi tunaisoma toka wapi?.. Elimu yetu inaandikwa na kina nani?.. hawa watu wanajua wanachokitaka na wanajua kuunda policies kwa kutazama watu na mazingira yao we only fit in to solve their puzzle!

Na tusijidanganye kabisa kwamba misaada ya hawa watu inatoka bila masharti, wanatoa misaada wakijua tutafungua milango kadhaa wapenyeze. Why watu kama Chavez hawawapi misaada?..Cuba to be Socialist kwa nini wanyimwe misaada! kama wanaweza kuilipa. Hivyo, bado kabisa tunawatumika wao zaidi ya sisi wenyewe na kama mnamkumbuka mwalimu alipokataa misaada ya hawa wazungu kwa kuwaambia unaponipa msaada usinambie priorities na policies zipi zitumike, wewe sii unataka kulipwa na interest juu, then tuacheni sisi tupange maendeleo yetu..Walianza kumkatia na kumwita kila jina baya duniani, leo tunawaona kina Chavez na Kagame wote hawa ni watu waliotoa matusi kama ya Zitto.

Zitto anaweza kuwa na mapungufu yake lakini on that statement nadhani hawa Waingereza wanatakiwa kuelewa wazi kwamba hawatusaidii chochote kwani kama wangekuwa wanajali haya misaada ingelkoma toka mwaka 2000 wakati kina Zitto wamepeleka malalamiko kibao kwa Tonny Blair na chombo chake cha kuzuia rushwa lakini hawakumsikia ndio kwanza wakam appoint Mkapa kuwa mjumbe wa kamati hiyo...Kwa hiyo tuwe makini sana na tuweke uzalendo mbele ya kusujudia misaada ambayo ina malengo zaidi ya kulinda maslahi ya nchi hizo ktk makoloni haya..
 
Wakuu zangu nimeingia katikati ya Mjadala... Hivi kweli hamuamini maneno aliyoyasema Zitto au mnayo tafsiri yenu?..
Ukoloni haujaisha upo na bdo unaendelea kuwepo isipokuwa kilichobadilika ni vichwa tu vya watawala toka ngozi nyeupe kuja Nyeusi. Na kiongozi yeyote anayetambua hilo mapema nadhani tunatakiwa kumpa moyo zaidi kwa sababu msisikie Ukoloni mamboleo ni mbaya kuliko ule wa Kukoloniwa...

Yes Miaka 50 ya Uhuru imetufiisha hapa na wakati wote wa Nyerere, Mkapa Mwinyi na hadi JK tumeona jinsi mkoloni alivyokuwa na mbinu za kila aina utafikri ni part of evolution...

Na tusijidanganye kabisa kwamba misaada ya hawa watu inatoka bila masharti hivyo tunawatumika wao zaidi ya sisi wenyewe na kama mnamkumbuka mwalimu alipokataa misaada ya hawa wazungu kwa kuwaambia unaponipa msaada usinambie priorities na policies zipi zitumike, wewe sii unataka kulipwa na interest juu, then tuacheni sisi tupange maendeleo yetu..Walianza kumkatia na kumwita kila jina baya duniani, leo tunawaona kina Chavez na Kagame wote hawa ni watu waliotoa matusi kama ya Zitto.

Zitto anaweza kuwa na mapungufu yake lakini on that statement nadhani hawa Waingereza wanatakiwa kuelewa wazi kwamba hawatusaidii chochote kwani kama wangekuwa wanajali haya misaada ingelkoma toka mwaka 2000 wakati kina Zitto wamepeleka malalamiko kibao kwa Tonny Blair na chombo chake cha kuzuia rushwa lakini hawakumsikia ndio kwanza wakam appoint Mkapa kuwa mjumbe wa kamati hiyo...Kwa hiyo tuwe makini sana na tuweke uzalendo mbele ya kusujudia misaada ambayo ina malengo zaidi ya kulinda maslahi ya nchi hizo ktk makoloni haya..

Wewe mtu aliyembaka dadiyo, halafu akampa vishilingi vya kununua chewing gum, dada yako akasema usijisikie umenipa sana, hapa umenilipa ulivyonibaka tu". Utamuona huyo dada yako ana akili kweli?
 
Wewe mtu aliyembaka dadiyo, halafu akampa vishilingi vya kununua chewing gum, dada yako akasema usijisikie umenipa sana, hapa umenilipa ulivyonibaka tu". Utamuona huyo dada yako ana akili kweli?
Inategemea na wewe umemwelewa vipi dadangu..Tatizo ni pale mbakaji anapokuja na Chewing gum mara kwa mara kuitumia kama ndio kioo cha kumvuta dada atoe tena mchezo, safari hii iwe kwa hiyari yake..Unajua wakati wa Nyerere na Ujamaa Chewinggum ilikuwa deal, hivyo wewe ulozaliwa leo huwezi kabisa kuelewa ushawishi wa Bazooka enzi zile!

Dada yangu aliisha msamehe mbakaji sii kwa sababu ya Chewing gum bali ni ile aibu na fedheha ya kitendo cha kubakwa na ndicho kinachotumaliza nchi za kiafrika. Tuliisha wasamehe siku nyingi sana wakoloni lakini tatizo ni pale wanapoitumia hiyo misaada (chewing gum) kutuonyesha kwamba pasipo misaada hatuwezi kutoa mchezo - that was then..Mkuu walitubaka hawa jamaa na chewing gum waliitumia kutulaghai kusogea karibu nao kabla ya kubakwa..

Kwa kuongezea tu hawa jamaa washenzi sana toka enzi ya Mkapa wanatupamba tuu kwa masifa ya uongo, ati Tanzania inaongoza Afrika kwa kupiga hatua ya maendeleo na uzalishaji kila tunapowafungulia milango wakati nchi inaporomoka! wakati wao ndio wawekezaji wakubwa Tanzania wataacha vipi kutusifia!
 
Inategemea na wewe umemwelewa vipi dadangu..Tatizo ni pale mbakaji anapokuja na Chewing gum mara kwa mara kuitumia kama ndio kioo cha kumvuta dada atoe tena mchezo, safari hii iwe kwa hiyari yake..Unajua wakati wa Nyerere na Ujamaa Chewinggum ilikuwa deal, hivyo wewe ulozaliwa leo huwezi kabisa kuelewa ushawishi wa Bazooka enzi zile!

Dada yangu aliisha msamehe mbakaji sii kwa sababu ya Chewing gum bali ni ile aibu ya fedheha ya kitendo cha kubakwa na ndicho kinachotumaliza nchi za kiafrika. Tuliisha wasamehe siku nyingi sana wakoloni lakini tatizo ni pale wanapoitumia hiyo misaada (chewing gum) kutuonyesha kwamba pasipo misaada hatuwezi kutoa mchezo - that was then..Mkuu walitubaka hawa jamaa na chewing gum waliitumia kutulaghai kusogea karibu nao kabla ya kubakwa..

Kwa mkuongezea tu hawa jamaa washenzi sana toka Mkapa wanatupamba tuu kwa masifa ya uongo, ati tanzania inaongoza Afrika kwa kupiga hatua ya uzalishaji kila tunapowafungulia milango wakati nchi inaporomoka!

Zitto mchemfu, kulinganisha misaada na reparation noma. Kuna watu wanadai reparation kikweli wakisikia kuna mtu muafrika anasema hivi watakuwa disappointed kweli.

Wewe unamchukulia Zitto kama defiant, mie namchukulia kama buffoon asiyeweza kuji-control Twitter.

Naona kashakuchota na hiyo dichotomy ya "Wao vs. Sisi".
 
Zitto mchemfu, kulinganisha misaada na reparation noma. Kuna watu wanadai reparation kikweli wakisikia kuna mtu muafrika anasema hivi watakuwa disappointed kweli.

Wewe unamchukulia Zitto kama defiant, mie namchukulia kama buffoon asiyeweza kuji-control Twitter.

Naona kashakuchota na hiyo dichotomy ya "Wao vs. Sisi".
This is what I don't like...why unafiiri kisha nichota.. Of cause dichotomy happened when we got our independence. Na ndio maana wao wanatusema SISI kama waombaji na wao watoa misaada. Unajua mkuu wangu tatizo ni kwamba sisi bado tuna machungu ya kubakwa na tulisha wasamehe, lakini wanapokuja na hizo Chewing gum wakisema come on You loved it..(meaning kubakwa) Sasa wewe usiposema wazi kwamba ilotuponza ni chewing gum huyo mzungu ataendelea kutumendea kutufukuzia..It's about time tuwaambie ukweli..

Zitto ana matatizo yake sikubaliani naye wakati wote lakini ktk jambo lolote linalosisitiza Uzalendo na Uafrika wangu na kujiamini kusimama kama wanaume nipo na yeyote yule anayejiamini, as a fact mimi kama Mhafidhina kwanza niseme wazi ni mbaguzi naye amini ktk Uzawa na uzalendo kwanza na nau enzi utaifa wangu..Nimeshakorofishana na Zitto mara kibao hadi hoja zangu nyingine huwa hazijibu na najua kabisa kachukia lakini anajua Mkandara hana simile kusema mawazo yake..

Naamini kabisa kama wao waliweza sisi pia tunaweza kama tutawezeshwa kwa Policies ambazo zitawajenga kwanza wananchi wake na sio kutegemea wageni iwe kwa misaada au uwekezaji..Kuna matajiri wengi sana Dar nimewaona mimi enzi zetu wakiwa na vibanda (kiosk)vya kuuza urembo wa wanawake, kimbo na sabuni mitaani leo ni mabillionea, Kina Bakhresa walianza kama washona viatu leo mabillionea tena tajiri kuliko mashirika ya wazungu wengi tu..Kwa nini taifa liwe tegemezi kwa wazungu ikiwa tunaweza kabisa kuanza toka ndani..
 
Kiranga,

UTU mzima darasa nitakwambia kitu kimoja hasa kuhusu unafiki wa Watanzania. Nimekutana na watu hunambia don't trust Mbowe, wengine don't trust Dr.Slaa wengine don't trust Mnyika, Lissu, JK, Ndugu zako, and list goes on and on. Sasa hawa walonambia don't trust someone nilipowaamini wao ndio wao walikuja niingiza mjini..

Sasa Utu uzima dawa, nikaja gundua kwamba Tanzania ukitembea na Tapeli watu hawatakushtua hadi siku umeliwa ndio watajitokeza na kusema Aaaah! sisi tulikuona tu ukimwamini jamaa, lakini tulijua atakuingiza mjini... Unabki unajiuliza, sasa kwa nini hawakusema kabla?... kumbe ndio hulka yetu sisi unafiki.. tunafurahi sana mtu anaposhindwa ni sawa na kaa ndani ya kapu. Hivyo maadam hakuna mtu wa kuaminika bora tumia akili zako mwenyewe kufikia maamuzi yoyote - You're all by yourself, na ndicho nachoamini mimi..

Nina hakika kabisa wabaya matapeli na opportunist hawasemwi isipokuwa wale wenye nafasi ya kutoka kweli kama kina Zitto...Ki hulka tunatamani sana watu kama Zitto, Mbowe na Dr.Slaa warudi chini, wasifanikiwe.. na hata kama kuna kweli? kuna tatizo gani kuwaweka ktk mtihani tuone kama kweli wanaweza ama hawawezi!..
 
Ukweli usemwe nani sababu za msingi ya kurudi kwetu nyuma ni miaka 50 kila mmoja analalamika isipokuwa wachache.
 
Kiranga,

UTU mzima darasa nitakwambia kitu kimoja hasa kuhusu unafiki wa Watanzania. Nimekutana na watu hunambia don't trust Mbowe, wengine don't trust Dr.Slaa wengine don't trust Mnyika, Lissu, JK, Ndugu zako, and list goes on and on. Sasa hawa walonambia don't trust someone nilipowaamini wao ndio wao walikuja niingiza mjini..

Sasa Utu uzima dawa, nikaja gundua kwamba Tanzania ukitembea na Tapeli watu hawatakushtua hadi siku umeliwa ndio watajitokeza na kusema Aaaah! sisi tulikuona tu ukimwamini jamaa, lakini tulijua atakuingiza mjini... Unabki unajiuliza, sasa kwa nini hawakusema kabla?... kumbe ndio hulka yetu sisi unafiki.. tunafurahi sana mtu anaposhindwa ni sawa na kaa ndani ya kapu. Hivyo maadam hakuna mtu wa kuaminika bora tumia akili zako mwenyewe kufikia maamuzi yoyote - You're all by yourself, na ndicho nachoamini mimi..

Nina hakika kabisa wabaya matapeli na opportunist hawasemwi isipokuwa wale wenye nafasi ya kutoka kweli kama kina Zitto...Ki hulka tunatamani sana watu kama Zitto, Mbowe na Dr.Slaa warudi chini, wasifanikiwe.. na hata kama kuna kweli? kuna tatizo gani kuwaweka ktk mtihani tuone kama kweli wanaweza ama hawawezi!..
Mkuu Mkandara,
Waingereza wakati wa ukoloni, wameipatia Tanganyika faida kuliko wasingekuwapo.
Tatizo ni wao kutoruhusu watanganyika kushiriki siasa.
 
Ukweli usemwe nani sababu za msingi ya kurudi kwetu nyuma ni miaka 50 kila mmoja analalamika isipokuwa wachache.
sababu na misingi ni UNAFIKI wa Mwafrika!... tunauzana wenyewe kwa kupewa Unyapala.. viongozi wetu wote ni manyapala na ukielewa hilo sidhani kama utaona taabu kuelewa kwa nini sisi maskini.. How can we have Gold yetu ndani ya ardhi yetu waje watu wachimbe watuachie ruzuku ya 3% na tunadai hii inatosha tena kubwa sana ukilinganisha na....Hivi Amerika miaka ya 1700 walipogundua dhahabu waliwaita kina nani kwenda kuichimba?
 
Mkuu Mkandara,
Waingereza wakati wa ukoloni, wameipatia Tanganyika faida kuliko wasingekuwapo.
Tatizo ni wao kutoruhusu watanganyika kushiriki siasa.
Sii kweli vitu karibu vyote vilijengwa na Mjarumani, Muingereza kavikuta vipo tayari vinaelea..Halafu kama wasingekuja kwetu Afrika, hiyo Uingereza isingekuwepo ilivyo leo!.
 
Sii kweli vitu karibu vyote vilijengwa na Mjarumani, Muingereza kavikuta vipo tayari vinaelea..
Hapo ndipo tulipofaidika,
Kwa sababu tulikuwa protectorate, kazi yao ilkuwa kututayarisha tujitawale na tulikuwa chini ya UN.
Kwa hiyo waingereza walikuwa wanaripoti UN.
Pili jiulize kwanini Hongkong na Macau zilikuwa na maisha bora na uchumi bora kuliko China au Korea ambao walipata uhuru miaka mingi mno kabla yao?
Au South Africa.
 
Kiranga,

UTU mzima darasa nitakwambia kitu kimoja hasa kuhusu unafiki wa Watanzania. Nimekutana na watu hunambia don't trust Mbowe, wengine don't trust Dr.Slaa wengine don't trust Mnyika, Lissu, JK, Ndugu zako, and list goes on and on. Sasa hawa walonambia don't trust someone nilipowaamini wao ndio wao walikuja niingiza mjini..

I could have told you that son. First thing first, don't trust anyone.

Sasa Utu uzima dawa, nikaja gundua kwamba Tanzania ukitembea na Tapeli watu hawatakushtua hadi siku umeliwa ndio watajitokeza

Watu wako wa karibu wanaweza kukuangalia mkeo anakuchezea hata wasikwambie, na hili si Tanzania tu to be fair to our country.

na kusema Aaaah! sisi tulikuona tu ukimwamini jamaa, lakini tulijua atakuingiza mjini... Unabki unajiuliza, sasa kwa nini hawakusema kabla?... kumbe ndio hulka yetu sisi unafiki.. tunafurahi sana mtu anaposhindwa ni sawa na kaa ndani ya kapu. Hivyo maadam hakuna mtu wa kuaminika bora tuia akili zako mwenyewe kufikia maamuzi yoyote - You all by yourself na ndicho nachoamini mimi..

I could have told you that, in fact I told you that even before reading this part.

The trouble with your boy is that he is not even "by himself". he is shooting himself in the foot like Plaxico. Anybody serious who was taking him seriously just a few years ago is bound to see right through the facade, the pretension, the usurpation, the caricaturing of such a grave issue!

Nina hakika kabisa wabaya matapeli na opportunist hawasemwi

Unapowasema opportunists usimsahau na huyo Zitto anayetumia habari za reparation kushinia some brownie points for cheap politics.

Na nitajie hao matapeli na opportunists ambao hawasemwi ni kina nani hapa tu deal na specifics na kuacha ku generalize mambo.

isipokuwa wale wenye nafasi ya kutoka kweli kama kina Zitto...

Tatizo si nani ana nafasi ya kutoka, tatizo wote wenye nafasi ya kutoka wameoza, kwa sababu system ilivyokuwa designed huwezi kupata nafasi ya kutoka bila ku compromise integrity. And that is a truism.

Ki hulka tunatamani sana watu kama Zitto,

Labda wewe, mie siwezi kutamani mtu asiye na discipline ya kujua nini cha kusema Twitter na nini cha kuacha.

Mbowe na Dr.Slaa warutudi chini wasifanikiwe na hata kama kweli kuna tatizo gani kuwaweka ktk mtihani tuone kweli wanaweza hao hawawezi!..

Hii habari ya "RussianRoulette" leadership ni kichaa tu anaweza kui entertain.

Eti, ngoja niweke bunduki against kichwa na nipige risasi kwa kutegemea chamber ya risasi itakuwa haina risasi?

Hebu tuwape tu kwa sababu tunawajaribu tu, hatujui chochote? Ndicho kinachowashinda wabongo hicho, wanaona "bora zimwi likujualo, tusije ku Chilubwa bure".

Na ingawa siwapendi CCM, this is hardly about a party.
 
Tunalelewa na kuaminishwa kwamba bila kusiaidiwa hatuwezi kufanya lolote huo ni ujinga unaopandikizwa na viongozi wenye mawazo potofu...yani wanatutia aibu sana hawa jamaa..kazi kuomba omba na nyingi katika hizo wanaiba wanarudisha ulaya kutunza na haya mambwa ya Ulaya ni amanafiki tu...
 
Zitto na yeye anaanza kuimba huu wimbo wa wanasiasa walioshindwa kufanya kazi? Sio muda mrefu Zitto alikuwa Malaysia na alifanya mazungumzo na aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo. Ameona jinsi Malaysia walivyopiga hatua. Singapore nako hivyo hivyo na nchi hizi mbili zilikuwa chini ya ukoloni wa mwingereza na walipata uhuru around the same time na sisi. Sasa, wao wamefanya nini hadi wakapiga hatua?

Hivi ni kweli umaskini wa Tanzania ni kwa sababu ya misaada ya UK? Nani ni mwombaji na nani ni mtoaji? Wanasiasa acheni kutufanya sisi wananchi mazuzu. Ni nyie ndio mnaingia mikataba ya kinyonyaji, ni nyie ndio mnaacha kukusanya kodi, ni nyie ndio mnaacha wizi (hadi kwenye bank kuu) sasa leo mnataka tujadili 'colonial exploits?
 
Hapo ndipo tulipofaidika,
Kwa sababu tulikuwa protectorate, kazi yao ilkuwa kututayarisha tujitawale na tulikuwa chini ya UN.
Kwa hiyo waingereza walikuwa wanaripoti UN.
Pili jiulize kwanini Hongkong na Macau zilikuwa na maisha bora na uchumi bora kuliko China au Korea ambao walipata uhuru miaka mingi mno kabla yao?
Au South Africa.
Kwa sababu wakoloni walijua faida ya kila kitu kilichopo chini ya ardhi ya hawa watawaliwa kwa mahitaji yao huko Ulaya (Demand and Supply) Hongokong ilikuwa maarufu kwa Opium na ndio utajiri ulipoanzia, wakati wachina na Ujamaa wao walifikiria hawana kitu wanakihitaji kutoka nje isipokuwa tahadhali kubwa ilikuwa kutokoloniwa tena maana athari zake wameisha ziona..

Hivyo, Waingereza walijenga makazi yao kwa biashara haramu, in return walijenga makazi yao haya mapya sehemu hizo kuanza biashara na nchi zao. On the otherside, Sisi na Ujamaa ulitupumbaza kuogopa kutawaliwa tukaogopa hata kufanya nao biashara..hatukuwa na uhakika na Uhuru tuloupata zaidi ya kuhakikisha tunajilinda dhidi yao.. Mkuu wangu hata wewe ukitaka kutajirika fanya biashara uza Unga kesho tutakuona siye yule.. lakini kama nafsi inakusuta utachukua muda mrefu sana kufanikiwa..

HongKong ikapiga hatua kuendelea wakati China ikabakia nyuma wakijilinda. Mkuu it's logic mtu yeyote anayejishughulisha na biashara siku zote ana nafasi nzuri ya kuendelea kuliko yule mwoga wa kujiingiza ktk biashara. Ukulima wa kutumikia tumbo hata siku moja hauwezi kukupeleka mbele isipokuwa pale unapotoka na kuanza kufanya Transactions..Unalima kwa ajili ya bishara unalima kwa ajili ya demand iliyopo nje.. hivyo kigezo kinakuwa nje ya tumbo lako. Na katika biashara hizo utagundua mbinu tofauti na kuona mengi ambayo kama ungekaa nyumbani suingeweza kuyaelewa.

Sisi wote, China, Korea na nchi zote za kiafrika tulichoshindwa kufanya ni biashara kwa hofu ya Ukoloni na madhara walotuachia na nchi kama Hongkong waliendelea kwa sababu the feared ones ndio walikuwa wakijiendeleza na kujipanua. Na Wachina walipoondoa ule woga na kuanza biashara na hawa watawala umeona matokeo ya kutojifungia ndani?.

Leo hii China signs business deals na partnership na makoloni kama walivyokuwa wakifanya Hongkong miaka ile, lakini sisi wakoloni hawataki tusign business deals bali waje wachukue wanachokitaka karibu na bure na watuuzie finished product. Tunanunua zaidi toka kwao kuliko wao wanavyonunua kwetu kwanza hawanunui bali wanachukua kwa bei yao.. Hawakufanya hivyo Hongkong wala South Afrika..
 
Ndugu zangu. Nadhani ni hekima kujua Jambo kwa kina kabla ya kuanza kulitolea maneno na hukumu. Ninaomba kueleza kifupi sana nini kilitokea huko twitter.

Kuna mama anaitwa Sarah. Mwingereza ambaye pamoja na mume wake waligombana na Benjamin Mengi kuhusu mashamba yanayoitwa sasa Silverdale Farms.

Ugomvi huu ulikuwa mkubwa na kuripotiwa mpaka katika Bunge la Uingereza. Huyu mama sasa hivi ameufanya Ugomvi ule binafsi na wa kibiashara kati yake na kina Mengi kuwa ni Ugomvi dhidi ya Watanzania wote. Amekuwa akiandika makala mbalimbali za kuichafua Tanzania. Amekuwa akitaka Serikali ya Tanzania imlipe yeye na mumewe fidia kwa makosa ya raia mmoja wa Tanzania anaitwa Benjamin Mengi.

Huyu mama na mumuewe hakuwahi kujiandikisha TIC ili kujua uwekezaji wake kwenye shamba na hata kupata protection ya kisheria. Sasa juzi kaandika makala kuhusu aid dependence ya Tanzania (Jambo ambalo ni la kweli) lakini akaweka takwimu nyingi sana za uwongo ambazo Watanzania wamezidaka na kuzizungumza Kama za kweli hivi. Baadhi yetu tukamwambia through twitter kwamba takwimu sake sio sahihi.

Pili tukamwambia alipaswa kusema Kama note katika makala yake kwamba yeye ana kesi na Serikali ya Tanzania. Kwamba yeye amekuwa akiilazimisha nchi yake ya Uingereza iinyime muswada Tanzania mpaka hapo Serikali ya Tanzania itakapomlipa fidia!

Mimi naongozwa na msimamo wa wazi kabisa kwamba 'right or wrong my country first' na hivyo siwezi kuruhusu mtu, tena mzungu anayejiita mwekezaji kuitukana nchi nchi yangu kwa sababu tu wamerushana na wafanyabiashara wenzake.

Hatuweziweka rehani kwa sababu ya magomvi ya watu binafsi.

Nimemwambia huyu mama na ninarudia kusema, muswada hii ni sehemu ya kurejesha Mali zilizonyonywa na ukoloni.

Nimemwambia huyu mama kwamba hata Waingereza wakitaka kuondoa misaada Yao waondoe na wala hatutakufa kwa kukosa misaada Yao. Nimemwambia hivyo na ninarudia hapa. That's me, what you see is what you get.

Huyu aliyeleta hii thread alete mtiririko wote wa mjadala na sio kipande kimoja tu cha mjadala na kuspin atakavyo yeye na wengi humu mmeingia katika mtego wake bila hata kuhoji.
 
Angeanzia kwenye corridors of power kushusha hizo nondo ili aeleweke.
 
I could have told you that son. First thing first, don't trust anyone.



Watu wako wa karibu wanaweza kukuangalia mkeo anakuchezea hata wasikwambie, na hili si Tanzania tu to be fair to our country.



I could have told you that, in fact I told you that even before reading this part.

The trouble with your boy is that he is not even "by himself". he is shooting himself in the foot like Plaxico. Anybody serious who was taking him seriously just a few years ago is bound to see right through the facade, the pretension, the usurpation, the caricaturing of such a grave issue!



Unapowasema opportunists usimsahau na huyo Zitto anayetumia habari za reparation kushinia some brownie points for cheap politics.

Na nitajie hao matapeli na opportunists ambao hawasemwi ni kina nani hapa tu deal na specifics na kuacha ku generalize mambo.



Tatizo si nani ana nafasi ya kutoka, tatizo wote wenye nafasi ya kutoka wameoza, kwa sababu system ilivyokuwa designed huwezi kupata nafasi ya kutoka bila ku compromise integrity. And that is a truism.



Labda wewe, mie siwezi kutamani mtu asiye na discipline ya kujua nini cha kusema Twitter na nini cha kuacha.



Hii habari ya "RussianRoulette" leadership ni kichaa tu anaweza kui entertain.

Eti, ngoja niweke bunduki against kichwa na nipige risasi kwa kutegemea chamber ya risasi itakuwa haina risasi?

Hebu tuwape tu kwa sababu tunawajaribu tu, hatujui chochote? Ndicho kinachowashinda wabongo hicho, wanaona "bora zimwi likujualo, tusije ku Chilubwa bure".

Na ingawa siwapendi CCM, this is hardly about a party.
All said ukweli utabakia kwamba hii misaada wanayoitoa ni aibu yao wenyewe kama reparation...Can't fool me! huwezi nambia Muingereza ana huruma saaana kutusaidia sisi wakati anatumia - When we were rulers they were better off! Hizi ndio story nazisikia sana kuhusu Oman na Zanzibar ati Zanzibar ilikuwa imeendelea sana chini ya Sultan na wajinga wanaamini wanataka kuvunja muungano bora warudi kwa Sultan. Hii misaada yote anayoahidi ni aibu ya kukoloni watu ati huruma!.

Siwezi kumsemea Zitto lakini size yake kuwaambia They can stick that shit in their ashakum!...huwezi kumsaidia mtu na matusi juu ukitegemea sisi tutakaa kimya kama tulivyotukanwa na Israel..
 
FJM

Tafadhali soma background ya Jambo hili kabla hujahukumu. Nimeeleza nini kilileteleza mjadala kati ya mimi na mwanamama wa kiingereza Sarah kiasi cha kumwambia wakitaka waondoe misaada Yao.

Ninaamini ukoloni uliofanyika Afrika ulikuwa na madhara zaidi kuliko Malaysia, Singapore na kwingine kokote. Ukoloni uliofanyika Afrika una madhara makubwa zaidi ya Kisaikolojia kuliko mahala pengine au jamii nyingine duniani.

Ukoloni uliofanyika Afrika mizizi yake bado haijakatwa. Bado mfumo wa uchumi wa dunia umelifanya bar a la Adrika kuwa Soko la malighafi. Bado wakoloni wana ushahiwishi mkubwa sana katika sera zetu mbalimbali.

Miaka 50 Baada ya Uhuru tusiendelee kusema matatizo yetu yanatokana na ukoloni. Hii ndio lugha wakoloni wanapenda kuisikia kutoka kwetu. Lugha inayowaondoa kwenye picha. Lugha inayowaonyesha wao wanatusaidia kwa usamaria mwema. Lugha hii sitaisema kamwe maana najua bado nchi hii imeshikwa na makucha ya ukoloni.

Leo hii Barrick kwa mfano hawakulipa kodi Tanzania mwaka 2010 lakini wamelipa kodi UK. Kuna Mgodi kule Uingereza? City of London is the largest tax haven. Tax dodging investors have camped within the ring fenced cityn of London exploiting developing countries billions of USD every year through tax avoidance.

Hivi vi misaada hivi ni vi reparation tu ambayo haipo kwenye makubaliano tu. Unaweza kuiita vingine. Lakini nchi Kama Uingereza wala isijidai au kujitapa na misaada Yao kwetu. Wanachukua zaidi kutoka kwetu kuliko tunavyopata katika misaada. Wakitaka wachukue misaada Yao. Tutabaki Kama Taifa
 
Mimi naongozwa na msimamo wa wazi kabisa kwamba 'right or wrong my country first' na hivyo siwezi kuruhusu mtu, tena mzungu anayejiita mwekezaji kuitukana nchi nchi yangu kwa sababu tu wamerushana na wafanyabiashara wenzake.

"Tena mzungu"? Angekuwa si "mzungu" je?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom